< Obadiah 1 >
1 The vision of Obadiah. The Lord Yahweh says this concerning Edom: We have heard a report from Yahweh and an ambassador has been sent among the nations, saying, “Rise up! Let us rise up against her for battle!”
Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
2 Behold, I will make you small among the nations, you will be greatly despised.
“Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
3 The pride of your heart has deceived you, you who live in the clefts of the rock, in your lofty home; who say in your heart, “Who will bring me down to the ground?”
Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
4 Though you soar high like the eagle and though your nest is set among the stars, I will bring you down from there, says Yahweh.
Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
5 If thieves came to you, if robbers came by night—how you will be ruined!—would they not steal only as much as they needed? If grape gatherers came to you, would they not leave the gleanings?
“Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
6 How Esau has been ransacked, his hidden treasures will be searched out!
Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
7 All the men of your alliance will send you on your way to the border. The men who were at peace with you have deceived you, and prevailed against you. They who eat your bread have set a trap under you. There is no understanding in him.
Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
8 “Will I not on that day,” says Yahweh, “destroy the wise men from Edom and understanding out of the mountain of Esau?
“Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
9 Your mighty men will be dismayed, Teman, so that every man may be cut off from the mountain of Esau by slaughter.
Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
10 Because of the violence done to your brother Jacob, you will be covered with shame, and you will be cut off forever.
Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
11 On the day you stood aloof, on the day strangers carried away his wealth, and foreigners entered into his gates, and cast lots for Jerusalem, you were like one of them.
Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
12 But do not gloat over your brother's day, in the day of his misfortune, and do not rejoice over the people of Judah in the day of their destruction; do not boast in the day of their distress.
Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
13 Do not enter my people's gate in the day of their calamity; do not gloat over their affliction in the day of their disaster, do not loot their wealth in the day of their ruin.
Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
14 Do not stand at the crossroads to cut down his fugitives, and do not deliver up his survivors in the day of distress.
Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
15 For the day of Yahweh is near upon all the nations. As you have done, it will be done to you; your deeds will return on your own head.
“Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
16 For as you have drunk on my holy mountain, so will all the nations drink continually. They will drink and swallow and it will be as though they had never existed.
Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
17 But in Mount Zion there will be those that escape and it will be holy; and the house of Jacob shall possess their own possessions.
Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
18 The house of Jacob will be a fire, and the house of Joseph a flame, and the house of Esau will be stubble, and they will burn them, and consume them. There will be no survivors to the house of Esau, for Yahweh has spoken it.”
Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
19 Those from the Negev will possess the mount of Esau and those of the Shepelah will possess the land of the Philistines. They will possess the land of Ephraim and the land of Samaria; and Benjamin will possess Gilead.
Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
20 The exiles of this host of the people of Israel will possess the land of Canaan as far as Zarephath. The exiles of Jerusalem, who are in Sepharad, will possess the cities of the Negev.
Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
21 Deliverers will go up to Mount Zion to rule over the hill country of Esau, and the kingdom will belong to Yahweh.
Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.