< Numbers 4 >
1 Yahweh spoke to Moses and to Aaron. He said,
BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
2 “Conduct a census of the male descendants of Kohath from among the Levites, by their clans and families.
Fanya sensa ya uzao waume wa Kohathi kutoka kwa Walawi, kwa kufuata jamaa na na familia za koo.
3 Count all the men who are thirty to fifty years old. These men must join the company to serve in the tent of meeting.
Uwahesabu wanaume ambao wana umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Hawa wataungana na kundi linalotumika kutoa huduma kwenye hema ya kukutania.
4 The descendants of Kohath must take care of the most holy things reserved for me in the tent of meeting.
Uzao wa Kohathi watalinda vile vitu vitakatifu zaidi vilivyohifadhiwa kwa ajili yangu katika hema ya kukutania.
5 When the camp prepares to move forward, Aaron and his sons must go into the tent, take down the curtain that separates the most holy place from the holy place and cover the ark of the testimony with it.
Wakati kambi inapojiandaa kusonga mbele, Haruni na wanawe lazima waende hemani, kulishusha pazia linalotenganisha mahali patakatifu na kulifunika sanduku la ushuhuda kwa pazia hilo. Watalifunika hilo sanduku kwa ngozi za pomboo.
6 They must cover the ark with sea cow skins. They must spread a blue cloth over it. They must insert the poles to carry it.
Watatandika juu yake nguo za rangi ya samawi. Watachomeka hiyo miti ya kubebea.
7 They are to spread a blue cloth on the table of the bread of the presence. On it they must put the dishes, spoons, bowls, and jars for pouring. Bread must always continue to be on the table.
Watatandika nguo ya rangi ya samawi kwenye meza ya mikate ya wonyesho. Juu yake wataweka sahani, vijiko, mabakuli na vikombe vya kumiminia. Mikate itakuwepo daima mezani.
8 They must cover them with a scarlet cloth and again with sea cow skins. They must insert poles to carry the table.
Wataifunika na nguo ya rangi nyekundu na ngozi za pomboo. na kuweka miti ya kubebea.
9 They must take a blue cloth and cover the lampstand, along with its lamps, tongs, trays, and all the jars of oil for the lamps.
Watachukua nguo ya rangi ya samawi na kukifunika kinara, pamoja na taa zake, na koleo zake, na sahani zake na vikombe vyake vya kuwekea mafuta ya taa.
10 They must put the lampstand and all its accessories into a covering of sea cow skins, and they must put it on a carrying frame.
Wataweka kinara na vifaa vyake vikiwa vimefunikwa na ngozi ya pomboo, na wataweka kwenye miti ya kukibebea.
11 They must spread a cloth of blue on the gold altar. They must cover it with a covering of sea cow skins, and then insert the carrying poles.
Watafunika na nguo ya samawi katika madhabau ya dhahabu. Wataifunika na ngozi za pomboo, na kuweka ile miti ya kubebea.
12 They must take all the equipment for the work in the holy place and wrap it in a blue cloth. They must cover it with sea cow skins and put the equipment on the carrying frame.
Watavichukua vyombo vyote vya kazi takatifu na kuvizonga kwenye hiyo nguo ya rangi ya samawi. Watavifunika na ngozi za pomboo na kuviweka hivyo vyombo kwenye miti ya kubebea.
13 They must remove the ashes from the altar and spread a purple cloth on the altar.
Watayaondoa majivu kwenye madhabahu na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake.
14 They must put on the carrying frame all the equipment that they use in the work of the altar. These objects are the firepans, forks, shovels, bowls, and all the other equipment for the altar. They must cover the altar with sea cow skins and then insert the carrying poles.
Watavieka kwenye miti ya kubebea vyombo vyote wanavyovitumia kwa kazi ya madhabahuni. Vyombo hivi ni vyetezo, majembe, mabakuli na vitu vingine vya madhabahuni. Wataifuniks madhabahu na ngozi za pomboo na kuweka ile miti ya kubebea.
15 When Aaron and his sons have completely covered the holy place and all its equipment, and when the camp moves forward, then the descendants of Kohath must come to carry the holy place. If they touch the holy instruments, they must die. This is the work of the descendants of Kohath, to carry the furnishings in the tent of meeting.
Wakati Haruni na wanawe walipokuwa wamekamilisha kupafunika mahali patakatifu na vyombo vyote, na kambi itakapoanza kuendelea mbele, ndipo wana wa Kohathi watakapokuja kubeba vitu vya mahali patakatifu. Kama watagusa vyombo vitakatifu, lazima watakufa. Hii ni kazi ya wana wa uzao wa Kohathi, kubeba mapambo ya hema ya kukutania.
16 Eleazar son of Aaron the priest oversees the care of the oil for the light, the sweet incense, the regular grain offering, and the anointing oil. He oversees the care of the entire tabernacle and all that is in it, the holy place and its equipment.”
Eliazari mwana wa Haruni kuhani atalinda na kusimamia mafuta ya taa, ubani mzuri, sadaka za mara kwa mara na mafuta ya upako. Atasimamia ulinzi wa hema lote na vyote vilivyomo, mahali patakatifu na vyombo vyake.”
17 Yahweh spoke to Moses and to Aaron. He said,
BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
18 “Do not allow the Kohathite tribal clans to be removed from among the Levites.
Usiruhusu kabila la Wakohathi kuondolewa kati ya Walawi.
19 Protect them, that they may live and not die, by doing this. When they approach the most holy things
Walinde waishi ili wasije wakafa, kwa kufanya hivi. Wanapokuwa wanasogelea
20 they must not go in to see the holy place even for a moment, or they must die. Aaron and his sons must go in, and then Aaron and his sons must assign each of the Kohathites to his work, to his special tasks.”
wasije wakaingia ndani ili kuona eneo takatifu hata kwa kitambo, vinginevyo watakufa. Bali Haruni na wanawe wanaweza kuingia, ndipo Haruni na Wanawe watakapowapangia Wakohathi kazi maalumu ya kufanya, kwa kila mmoj.”
21 Yahweh spoke again to Moses. He said,
BWANA akanena na Musa tena, Akasema, “Fanya sensa kwa wana Gerishoni pia, kwa kufuata familia za mababu zao, koo zao.
22 “Conduct a census of the descendants of Gershon also, by their ancestor's families and by their clans.
Uwahesabu wale wenye umri wa mika thelathini hadi miaka hamsini.
23 Count those who are thirty years old to fifty years old. Count all of them who will join the company to serve in the tent of meeting.
Uwahesabu wote ili waje kuungana na wale wanaotumika katika hema ya kukutania.
24 This is the work of the clans of the Gershonites, when they serve and what they carry.
Hii ndiyo itakuwa kazi ya koo za Gerishoni, wanapotumikia na wanachobeba.
25 They must carry the curtains of the tabernacle, the tent of meeting, its covering, the covering of sea cow skin that is on it, and the curtains for the entrance to the tent of meeting.
Watabeba pazia la masikani, hema la kukutania, na vifunikio vyake, vifuniko vya ngozi ya pomboo ambvyo viko juu yake, na pazia kwenye lango la hema ya kukutania.
26 They must carry the curtains of the court, the curtain for the doorway of the court's gate, which is near the tabernacle and near the altar, their ropes, and all the instruments for their service. Whatever should be done with these things, they must do it.
Watabeba pazia la ua, pazia la kwenye mlango wa ua, ambao uko karibu na maskani karibu na madhabahu, kamba zake na vifaa vyote vya utumishi wake. Chochote kinachotakiwa kufanywa kutokana na vitu hivi, wao ndio watakaofanya.
27 Aaron and his sons must direct all the service of the descendants of the Gershonites, in everything that they transport, and in all their service. You must assign them to all their responsibilities.
Haruni na wanawe ndio watakaongoza utumishi wa uzao wa Wagerishoni, kwa vitu vyote vile vya kusafirisha, na katika utumishi wao wote. Lazima uwagawie majukumu yao yote.
28 This is the service of the clans of the descendants of the Gershonites for the tent of meeting. Ithamar son of Aaron the priest must lead them in their service.
Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa wana wa Wagerishoni katka hema ya kukutania. Ithamari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza katika utumishi.
29 You must count the descendants of Merari by their clans, and order them by their ancestor's families,
Utawahesabu uzao wa Merari kwa koo zao, na uwapange katika familia za mabau zao,
30 from thirty years old and older up to fifty years old. Count everyone who is going to join the company and serve in the tent of meeting.
kuanzia wenye umri wa miaka thelatini hadi miaka hamsini. Umuhesabu kila atakayeungana na kundi lenye utumishi katika hema ya kukutania.
31 This is their responsibility and their work in all their service for the tent of meeting. They must care for the framing of the tabernacle, its crossbars, posts, and sockets,
Huu ndio wajibu na kazi yao katika utumishi wao kwenye hema ya kukutania. Watazilinda mbao za maskani, mataluma yake, nguzo na makalishio yake,
32 along with the posts of the courtyard around the tabernacle, their sockets, pegs, and their ropes, with all their hardware. List by name the articles they must carry.
pamoja na nguzo za ua zinazozunguka masikani, makalishio yake, vigingi na kamba zake, na vifaa vinginevya ujenzi. Waorodheshe kwa majina na majukumu yao.
33 This is the service of the clans of the descendants of Merari, what they are to do for the tent of meeting, under the direction of Ithamar son of Aaron the priest.”
Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa Merari, ambao wanatakiwa kufanya katika hema ya kukutania, chini ya uongozi wa Ithmari mwana wa Haruni kuhani.”
34 Moses and Aaron and the leaders of the community counted the descendants of the Kohathites by the clans of their ancestor's families.
Musa na Haruni na viongozi wa watu waliwahesabu wana wa uzao wa Wakohathi kwa kufuata koo za familia za mababu zao.
35 They counted them from thirty years old and older up to fifty years old. They counted everyone who would join the company to serve in the tent of meeting.
Waliwahesabu wale wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Walimhesabu kila mmoja aliyepaswa kuungana na kundi linalotoa huduma ya utumishi kwenye hema ya kukutania.
36 They counted 2,750 men by their clans.
Waliwahesabu wanaume 2, 750 kwa kufuata koo zao.
37 Moses and Aaron counted all the men in the clans and families of the Kohathites who serve in the tent of meeting. In doing this, they obeyed what Yahweh had commanded them to do through Moses.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote kutoka koo na familia za Wakohathi ambao hutumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi kwa kumtii BWANA aliyewaagiza kupitia kwa Musa.
38 The descendants of Gershon were counted in their clans, by their ancestor's families,
Uzao wa Gerishoni walihesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao,
39 from thirty to fifty years old, everyone who would join the company to serve in the tent of meeting.
kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kwa kila mmoja aliyetakiwa kuungana na watu wanaotoa huduma kwenye hema ya kukutania.
40 All the men, counted by their clans and their ancestor's families, numbered 2,630.
Wanaume wote waliohesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao walikuwa 2, 630.
41 Moses and Aaron counted the clans of the descendants of Gershon who would serve in the tent of meeting. In doing this, they obeyed what Yahweh had commanded them to do through Moses.
Musa na Haruni walizihesabu koo za uzao wa Gerishoni ambao watatumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi ili kutii ambacho BWANA aliwaamuru kufanya kuptia kwa Musa.
42 The descendants of Merari were counted in their clans by their ancestor's families,
Uzao wa Merari walihesabiwa kwa koo kupitia familia za mababu zao,
43 from thirty to fifty years old, everyone who would join the company to serve in the tent of meeting.
kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kila anayepaswa kuungana na watu wanaotumika kwenye hema ya kukutania.
44 All the men, counted by their clans and their ancestor's families, numbered 3,200.
Wanaume wote waliohesabiwa kupitia koo za familia za mababu zao walikuwa 3. 200.
45 Moses and Aaron counted all these men, the descendants of Merari. In doing this, they obeyed what Yahweh had commanded them to do through Moses.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume hawa, uzao wa Merari. Kw kufanya hivi walitii amri ya BWANA aliyowaaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
46 So Moses, Aaron, and the leaders of Israel counted all the Levites by their clans in their ancestral families
Kwa hiyo Musa na Haruni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kw kufuata koo na familia za mababu zao
47 from thirty to fifty years old. They counted everyone who would do work in the tabernacle, and who would carry and care for the items in the tent of meeting.
kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. walimhesabu kila aliyepaswa kufanya kazi kwenye masikani, na kila aliyepaswa kubeba na kulinda vitu vya kwenye hema ya kukutania.
48 They counted 8,580 men.
Waliwahesabu wanaume 8, 580.
49 At Yahweh's command, Moses counted each man, keeping count of each by the type of work he was assigned to do. He counted each man by the kind of responsibility he would bear. In doing this, they obeyed what Yahweh had commanded them to do through Moses.
Kwa agizo la BWANA, Musa alimhesabu kila mwanamume na kutunza kumbukumbu ya kazi ambayo kila mmoja anaweza kufanya. Kwa hivyo, walitii kile ambacho BWANA alikuwa amewaagiza kufanya kupitia kwa Musa.