< Numbers 35 >

1 Yahweh spoke to Moses on the plains of Moab by the Jordan at Jericho and said,
Bwana akamwambia Mose katika nchi tambarare ya Moabu, kando ya Mto Yordani kuvukia Yeriko,
2 “Command the people of Israel to give some of their own shares of land to the Levites. They must give them cities to live in and pastureland surrounding those cities.
“Waagize Waisraeli kuwapa Walawi miji ya kuishi kutoka urithi ambao Waisraeli wataumiliki. Wape maeneo ya malisho kuzunguka hiyo miji.
3 The Levites will have these cities to live in. The pastureland will be for their cattle, their flocks, and all their animals.
Kisha watakuwa na miji ya kuishi na maeneo ya malisho kwa ajili ya ngʼombe zao, mbuzi, kondoo na mifugo yao mingine yote.
4 The pasturelands around the cities that you will give to the Levites must extend from the city walls for one thousand cubits in every direction.
“Maeneo ya malisho kuzunguka miji hiyo ambayo mtawapa Walawi yataenea mita 450 kutoka kwenye ukuta wa miji.
5 You must measure two thousand cubits from outside the city on the east side, and two thousand cubits to the south side, two thousand cubits to the west side, and two thousand cubits to the north side. This will be the pasturelands for their cities. The cities will be in the center.
Nje ya mji, pima mita 900 upande wa mashariki, upande wa kusini mita 900, upande wa magharibi mita 900, na upande wa kaskazini mita 900, na mji utakuwa katikati. Eneo hili litakuwa lao kwa ajili ya malisho.
6 Six of the cities that you will give to Levites must serve as cities of refuge. You must provide these as places to which a person who has killed someone can flee. Also provide forty-two other cities.
“Miji sita mtakayowapa Walawi itakuwa ya makimbilio, ambayo mtu anayemuua mwenzake aweza kukimbilia humo. Zaidi ya hiyo, wapeni miji mingine arobaini na miwili.
7 The cities that you give to the Levites will total forty-eight. You must give their pasturelands with them.
Kwa jumla inawapasa kuwapa Walawi miji arobaini na minane, pamoja na maeneo ya malisho yao.
8 The larger tribes of the people of Israel, the tribes that have more land, must provide more cities. The smaller tribes will provide fewer cities. Each tribe must provide for the Levites according to the share that it has received.”
Miji ambayo mtawapa Walawi kutoka nchi ambayo Waisraeli wanamiliki itatolewa kwa uwiano wa urithi wa kila kabila. Chukua miji mingi kutoka lile kabila lenye miji mingi, lakini uchukue miji michache kutoka kwa kabila lile lenye miji michache.”
9 Then Yahweh spoke to Moses and said,
Kisha Bwana akamwambia Mose:
10 “Speak to the people of Israel and say to them, 'When you cross over the Jordan into the land of Canaan,
“Sema na Waisraeli, uwaambie: ‘Mtakapovuka Yordani kuingia Kanaani,
11 then you must choose cities to serve as cities of refuge for you, a place to which a person who has killed someone unintentionally may flee.
chagueni baadhi ya miji iwe miji yenu ya makimbilio, ambayo mtu ambaye ameua mwenzake bila kukusudia aweza kukimbilia humo.
12 These cities must be your refuge from the avenger, so that the accused man will not be killed without first standing trial before the community.
Itakuwa mahali pa kukimbilia kutoka mlipiza kisasi, ili kwamba mtu aliyeshtakiwa kwa mauaji asife kabla ya kujitetea mbele ya mkutano.
13 You must choose six cities as cities of refuge.
Miji hii sita mtakayoitoa itakuwa miji yenu ya makimbilio.
14 You must provide three cities beyond the Jordan and three in the land of Canaan. They will be cities of refuge.
Mtatoa miji mitatu ngʼambo hii ya Yordani na miji mingine mitatu upande wa Kanaani kama miji ya makimbilio.
15 For the people of Israel, for the foreigners, for anyone living among you, these six cities will serve as a refuge to which anyone who kills someone unintentionally can flee.
Miji hii sita itakuwa mahali pa makimbilio kwa ajili ya Waisraeli, wageni na watu wengine wanaoishi katikati yenu, ili kwamba mtu yeyote ambaye ameua mtu mwingine pasipo kukusudia aweze kukimbilia humo.
16 But if an accused man has struck his victim with an instrument of iron, and if his victim dies, then the accused is indeed a murderer. He must certainly be put to death.
“‘Kama mtu akimpiga mwenzake kwa chuma naye mtu huyo akafa, mtu huyo ni muuaji; muuaji sharti atauawa.
17 If an accused man has struck his victim with a stone in his hand that might kill the victim, and if his victim dies, then the accused is indeed a murderer. He must certainly be put to death.
Au kama mtu analo jiwe mkononi mwake ambalo laweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
18 If an accused man has struck his victim with a wooden weapon that might kill the victim, and if the victim dies, then the accused is indeed a murderer. He must certainly be put to death.
Au kama mtu ana chombo cha mti mkononi mwake ambacho chaweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
19 The avenger of blood may put the murderer to death. When he meets him, the avenger of blood must put him to death.
Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji; wakati akikutana naye, atamuua.
20 If he strikes another in hatred or throws something at him, while hiding to ambush him, so that the victim dies,
Ikiwa mtu ana chuki ya siku nyingi na mwenzake akamsukuma au akamtupia kitu kwa kukusudia naye akafa,
21 or if he strikes him down in hatred with his hand so that the victim dies, then the accused who struck him must surely be put to death. He is a murderer. The avenger of blood may put the murderer to death when he meets him.
au ikiwa katika uadui akampiga ngumi naye akafa, mtu yule sharti atauawa; yeye ni muuaji. Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji atakapokutana naye.
22 But if an accused man suddenly hits a victim without premeditated hate or throws something that hits the victim without lying in wait
“‘Lakini kama mtu akimsukuma mwenziwe ghafula pasipo chuki, au kumtupia kitu pasipo kukusudia,
23 or if he throws a stone that could kill a victim without seeing the victim, then the accused was not the victim's enemy; he was not trying to hurt the victim. But this is what to do if the victim dies anyway.
au, pasipo kumwona, akimwangushia jiwe ambalo laweza kumuua naye akafa, basi kwa kuwa hakuwa adui yake naye hakukusudia kumuumiza,
24 In that case, the community must judge between the accused and the avenger of blood on the basis of these rules.
kusanyiko lazima liamue kati yake na mlipiza kisasi wa damu kufuatana na sheria hizi.
25 The community must rescue the accused from the power of the avenger of blood. The community must return the accused to the city of refuge to which he had originally fled. He must live there until the death of the current high priest, the one who was anointed with the holy oil.
Kusanyiko ni lazima limlinde yule anayeshtakiwa kuua kutoka kwa mlipiza kisasi wa damu, na kumrudisha katika mji wa makimbilio alikokuwa amekimbilia. Lazima akae humo mpaka atakapokufa kuhani mkuu ambaye alikuwa amepakwa mafuta matakatifu.
26 But if the accused man at any time goes beyond the border of the city of refuge to which he fled,
“‘Lakini kama mshtakiwa atatoka nje ya mipaka ya mji wa makimbilio ambao amekimbilia,
27 and if the avenger of blood finds him outside the border of his city of refuge, and if he kills the accused man, the avenger of blood will not be guilty of murder.
na mlipiza kisasi wa damu akamkuta nje ya mji, mlipiza kisasi wa damu anaweza kumuua mshtakiwa huyo bila kuwa na hatia ya kuua.
28 This is because the accused man should have remained in his city of refuge until the death of the high priest. After the death of the high priest, the accused may return to the land where he has his own property.
Mshtakiwa lazima akae katika mji wake wa makimbilio mpaka atakapokufa kuhani mkuu; atarudi tu kwenye mali yake baada ya kifo cha kuhani mkuu.
29 These laws must be statutes for you through all your people's generations in all the places where you live.
“‘Hizi ndizo kanuni za sheria zitakazohitajiwa kwenu na katika vizazi vyenu vijavyo, popote mtakapoishi.
30 Whoever kills any person, the murderer must be killed, as testified to by the words of witnesses. But one witness' word alone may not cause any person to be put to death.
“‘Yeyote anayeua mtu atauawa kama muuaji ikiwa tu kuna ushuhuda wa mashahidi. Lakini hakuna mtu atakayeuawa kwa ushuhuda wa shahidi mmoja tu.
31 Also, you must not accept ransom for the life of a murderer who is guilty of murder. He must certainly be put to death.
“‘Usikubali fidia yoyote ya kuokoa uhai wa muuaji ambaye anastahili kufa. Mtu huyo hakika lazima auawe.
32 You must not accept ransom for the one who has fled to a city of refuge. You must not in this way allow him to reside on his own property until the high priest dies.
“‘Usikubali fidia ya mtu yeyote ambaye amekimbilia katika mji wa makimbilio na kumruhusu kurudi kuishi katika nchi yake kabla ya kifo cha kuhani mkuu.
33 Do not pollute in this way the land where you live, because blood from murder pollutes the land. No atonement can be made for the land when blood has been shed on it, except by the blood of the one who shed it.
“‘Msiinajisi nchi mnayoishi. Umwagaji damu hunajisi nchi, na upatanisho hauwezekani kufanyika katika nchi ambayo damu imemwagwa, isipokuwa tu kwa damu ya yule aliyeimwaga damu.
34 So you must not defile the land in which you live because I am living in it. I, Yahweh, live among the people of Israel.'”
Msiinajisi nchi mnayoishi, ambayo nami ninakaa, kwa kuwa Mimi, Bwana, ninakaa katikati ya Waisraeli.’”

< Numbers 35 >