< Numbers 18 >

1 Yahweh said to Aaron, “You, your sons, and your ancestor's clan will be responsible for all sins committed against the sanctuary. But only you and your sons with you will be responsible for all sins committed by anyone in the priesthood.
BWANA akamwambia Haruni, “Wewe, wana wako, na uzao wa baba yako watawajibika kwa dhambi zote zilizotendwa mahali patakatifu. Lakini wewe na wana wako pekee mtawajibika kwa uovu uliofanywa na yeyote mahali patakatifu.
2 As for your fellow members of the tribe of Levi, your ancestors' tribe, you must bring them with you so they may join you and help you when you and your sons serve in front of the tent of the covenant decrees.
Na ndugu zako nao wa kabila ya Lawi, kabila la ukoo wako, utawaleta pamoja na wewe ili kwamba waweze kuungana na wewe ili wakusaidie wakati wewe na wanao mnapokuwa mnatumikia mbele ya hema ya amri ya agano.
3 They must serve you and the whole tent. However, they must not come near to anything in the holy place or connected with the altar, or they and also you will die.
Watakutumikia wewe na hema yote. Hata hivyo, wasisogee karibu na chochote ndani ya mahali patakatifu au kitu chochote kilichounganishwa na madhabahu, vinginevyo wewe na wao mtakufa.
4 They must join you and take care of the tent of meeting, for all the work connected with the tent. A foreigner must not come near you.
Wataungana na wewe na kuitunza hema ya kukutania, kwa kazi zote zinazohusiana na hema. Mtu mgeni asikusogelee.
5 You must take responsibility for the holy place and for the altar so that my anger does not come on the people of Israel again.
Wewe utaajibika kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya madhabahu ili kwamba hasira yangu isiwajilie watu wa Israeli tena.
6 Look, I myself have chosen your fellow members of the Levites from among the descendants of Israel. They are a gift to you, given to me to do the work connected to the tent of meeting.
Tazama, Mmi mwenyewe nimewachagua ndugu zako wa kabila ya Walawi kutoka mioingoni mwa uzao wa Israeli. Wao ni zawadi kwako. walitolewa kwangu ili waifanye kazi inayohusiana na hema ya kukutania.
7 But only you and your sons may exercise the priesthood regarding everything connected with the altar and everything inside the curtain. You yourselves must fulfill those responsibilities. I am giving you the priesthood as a gift. Any foreigner who approaches must be put to death.”
Lakini ni wewe pekee yako na wanao ndio mnaoruhusiwa kufanya kazi ya ukuhani kuhusiana na kila kitu kilichounganishwa na madhabahu na kitu chochote ndani ya lile pazia. Wewe mwenyewe lazima ukamilishe majukumu hayo. Mimi ninakupa ukuhani kama zawadi. Mgeni yeyote anayekaribia atauawa.”
8 Then Yahweh said to Aaron, “Look, I have given you the duty of handling the offerings raised up to me, and all the holy offerings that the people of Israel give to me. I have given these offerings to you and your sons as your ongoing share.
Kisha BWANA akamwambia Haruni, “Tazama, Nimekupa majukumu ya kusimamia sadaka za kuinuliwa kwangu, na sadaka zengine takatifu ambazo wana wa Israeli wanatoa kwangu. Nimekupa sadaka hizi wewe na wana wako kuwa haki yako milele.
9 This will belong to you from the most holy things that is kept from the fire. From every offering of theirs—every grain offering, every sin offering, and every guilt offering—they are set apart to you and to your sons.
Hivi ni vitu vitakatifu sana, amabavyo visiteketezwe kwa moto: kutoka kwenye sadaka zao-kila sadaka ya unga, kila sadaka ya dhambi, na kila sadaka ya hatia- ni vitu vitakatifu sana kwa ajili yako na wana wako.
10 These offerings are very holy; every male must eat it, for they are holy to you.
Sadaka hizi ni takatifu sana; kila mume lazima aile, kwa kuwa ni vitakatifu kwako.
11 These are the offerings that will belong to you, set apart out of all their gifts of the wave offerings of the people of Israel. I have given them to you, your sons, and your daughters, as your portion forever. Everyone who is ceremonially clean in your family may eat any of these offerings.
Hizi ni sadaka ambazo zitakuwa zako: Sadaka zao, sadaka zote za kuinuliwa za wana wa Israeli. Nimekupa wewe, wana wako na binti zako kuwa gawio lako la milele. Kila mmoja ambaye ni msafi katika familia yako anaweza kula sadaka zozote katika hizi.
12 All the best of the oil, all the best of the new wine and grain, the firstfruits that the people give to me—all these things I have given to you.
Mafuta yote mazuri, ile divai nzuri yote mpya na unga, malimbuko ambyo watu hutoa kwangu- vitu hivi vyote nimekupa wewe.
13 The first ripe produce of all that is in their land, which they bring to me, will be yours. Everyone who is clean in your family may eat these things.
Mavuno ya kwanza yaliyoiva yaliyo katika ardhi yao ambayo wanaleta kwangu, yatakuwa yako. Kila mtu aliye msafi kwenye famila yako anaweza kula vitu hivi.
14 Every devoted thing in Israel will be yours.
Kila kitu kilichotolewa wakfu katika Israeli kitakuwa chako.
15 Everything that opens the womb, all the firstborn which the people offer to Yahweh, both of man and animal, will be yours. Nevertheless, the people must certainly buy back every firstborn son, and they must buy back the firstborn male of unclean animals.
Kila kitu kinachofungua tumbo, kila limbuko ambalo watu hutoa kwa BWANA, vyote vya watu na wanyama, vitakuwa vyako. Hata hivyo, watu lazima wawakomboe wazaliwa wa kwanza wa kiume, na watawakomboa wazaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi.
16 Those that are to be bought back by the people must be bought back after becoming one month old. Then the people may buy them back, for the price of five shekels, by the standard weight of the sanctuary shekel, which equals twenty gerahs.
Wale ambao wanahitaji kukombolewa na watu watakombolewa wakiwa na umri wa mwezi mmoja. Ndipo watu watawakomboa kwa bei ya shekeli tano, kwa kiwango cha shekeli za mahali patakatifu, ambacho ni sawa na gera ishirini.
17 But the firstborn of a cow, or the firstborn of a sheep, or the firstborn of a goat—you must not buy back these animals; they are set apart to me. You must sprinkle their blood on the altar and burn their fat as an offering made by fire, an aroma pleasing to Yahweh.
Lakini mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe, au mzaliwa wa kwana wa kondoo, au mzaliwa wa kwanza wa mbuzi-msiwakomboe hawa wanyama, wametengwa kwa ajili yangu. Utanyunyizia damu yake madhabahuni na kuteketeza mafuta yao kama sadaka ya moto, ambayo ni harufu nzuri ya kumpendeza BWANA.
18 Their meat will be yours. Like the raised breast and the right thigh, their meat will be yours.
Nyama yao itakuwa yako. Kama kidali cha kuinuliwa na paja la kulia, nyama yao itakuwa yako.
19 All the holy offerings that the people of Israel present to Yahweh, I have given to you, and to your sons and to your daughters with you, as a continual share. It is an everlasting covenant of salt, a binding covenant forever, before Yahweh for both you and your descendants with you.”
Sadaka yote takatifu ambayo watu wa Israeli wanaitoa kwa BWANA, nimekupa wewe, na wana wako na binti zako walio pamoja nawe. Kama gawio la kudumu. Hili ni agano la milele la chumvi, agano linalofunga milele, mbele za BWANA kwako wewe na uzao wako walio pamoja na wewe.”
20 Yahweh said to Aaron, “You will have no inheritance in the people's land, nor will you have any share of property among the people. I am your share and inheritance among the people of Israel.
BWANA akasema na Haruni. “hautakuwa na urithi katika ardhi ya watu, wala hautakuwa na gawio miongoni mwa watu. Mimi ndimi gawiio lenu na urithi wenu miongoni mwa watu wa Israeli.
21 To the descendants of Levi, look, I have given all the tithes in Israel as their inheritance in return for the service that they provide in working at the tent of meeting.
Tazama, Nimewapatia uzao wa Lawi, zaka zote za Israeli kuwa urithi wao kwa sababu ya huduma wanayotoa katika hema ya kukutania.
22 From now on the people of Israel must not come near the tent of meeting, or they will be responsible for this sin and die.
Kuanzi a sasa, watu wa Israeli wasisogee karibu na hema ya kukutania, vinginevyo wataajibika kwa dhambi hii na kufa.
23 The Levites must do the work connected to the tent of meeting. They will be responsible for any sin regarding it. This will be a permanent law throughout your people's generations. Among the people of Israel they must have no inheritance.
Walawi wafanya kazi inayohusiana na hema ya kukutania. Wataajibika kwa dhambi inyohusiana na hema. Hii itakuwa sheri ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Na miongoni mwa watu wa Israeli hawa hawatakuwa na urithi.
24 For the tithes of the people of Israel, which they offer as a contribution to me—it is these that I have given to the Levites as their inheritance. That is why I said to them, 'They must have no inheritance among the people of Israel.'”
Kwa kuwa zaka za wana wa Israeli, wanazotoa kama mchango kwangu -ndivyo hivyo ambavyo nimewapa Walawi kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu ya kuwaambia, Kuwa hawatakuwa na urithi kati ya watu wa Israeli.
25 Yahweh spoke to Moses and said,
BWANA akanena na Musa, akamwambia,
26 “You must speak to the Levites and say to them, 'When you receive from the people of Israel the tenth that I have given to you from them for your inheritance, you will present a contribution from it to Yahweh, a tenth of the tithe.
“Inakupasa ukaseme na Walawi uwaambie, 'Mnapopokea zaka toka kwa watu ambayo BWANA amewapa kutoka kwao kuwa urithi, ndipo na nyie mtakapotoa sehemu ya kumi ya zaka hizo.
27 Your contribution must be considered by you as if it were a tenth of the grain from the threshing floor or of the production from the winepress.
Zaka yenu itahesabika kama moja ya mapato ya sakafu ya kupuria nafaka ya mazao yenu au mazao ya vinu vya kukamulia zabibu.
28 So you also must make a contribution to Yahweh from all the tithes that you receive from the people of Israel. From them you must give his contribution to Aaron the priest.
Kwa hiyo na ninyi lazima mtoe mchango wenu kwa BWANA kutokana na zaka mnazopata kutoka kwa watu wa Israeli. Kutokana na hizo mtatoa matoleo yenu kwa Haruni yule kuhani.
29 Out of all the gifts you receive, you must make every contribution to Yahweh. You must do this from all the best and the holiest things that have been given to you.'
Kwa kila sadaka mnayopata, mtatoa matoleo yenu kwa BWANA. Mtafanya hivi kutokana na vitu vizuri na vitakatifu sana ambavyo mmepewa.
30 Therefore you must say to them, 'When you present the best of it, then it must be credited to the Levites as the product from the threshing floor and the winepress.
Kwa hiyo utawaambia, 'Mnapotoa hayo matoleo mazuri, ndipo itahesabika kwa Walawi kuwa ni mazao yao kutoka kwenye sakafu za kupuria na vinu vyao vya kukamulia.
31 You may eat the rest of your gifts in any place, you and your families, because it is your pay in return for your work in the tent of meeting.
Ndipo matakapokula nafaka zote zinazobaki mahali popote, ninyi na famailia zenu kwa sababu ndiyo malipo yenu ya kazi y a kwenye hema ya kukutania.
32 You will not incur any guilt by eating and drinking it, if you have presented to Yahweh the best of what you have received. But you must not profane the holy offerings of the people of Israel, or you will die.'”
Hamtakuwa na hatia yeyote kwa kuvila na kuvinywa, kama mtatoa kwa BWANA matoleo yenu mazuri mliyopokea. Lakini msizinajisi sadaka takatifu za wana wa Israeli, vinginevyo mtakufa.,”

< Numbers 18 >