< Numbers 13 >
1 Then Yahweh spoke to Moses. He said,
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, “tuma watu waende kuipeleleza nchi ya Kanani, ambayo nimewapa wana wa Israeli.
2 “Send some men to examine the land of Canaan, which I have given to the people of Israel. Send a man from every tribe of their ancestors. Each man must be a leader among them.”
Tuma mwanamume mmoja kutoka kila jamaa ya kabila. Kila mwanamume awe kiongozi katika kabila lake.”
3 Moses sent them from the wilderness of Paran, so that they might obey Yahweh's command. All of them were leaders among the people of Israel.
Musa akawatuma kutoka jangwa la Parani, ili watii amri ya BWANA. Watu wote hao walikuwa viongozi wa watu wa Israeli.
4 These were their names: from the tribe of Reuben, Shammua son of Zaccur;
Majina yao yalikuwa haya yafuatayo: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5 from the tribe of Simeon, Shaphat son of Hori;
Kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6 from the tribe of Judah, Caleb son of Jephunneh;
Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7 from the tribe of Issachar, Igal son of Joseph;
Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
8 from the tribe of Ephraim, Hoshea son of Nun;
Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 from the tribe of Benjamin, Palti son of Raphu;
Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
10 from the tribe of Zebulun, Gaddiel son of Sodi;
kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
11 from the tribe of Joseph (that is to say, from the tribe Manasseh), Gaddi son of Susi;
kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
12 from the tribe of Dan, Ammiel son of Gemalli;
kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
13 from the tribe of Asher, Sethur son of Michael;
kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
14 from the tribe of Naphtali, Nahbi son of Vophsi;
kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
15 from the tribe of Gad, Geuel son of Maki.
kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
16 These were the names of the men whom Moses sent to examine the land. Moses called Hoshea son of Nun by the name of Joshua.
Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
17 Moses sent them to examine the land of Canaan. He said to them, “Approach from the Negev and go up into the hill country.
Musa akawatuma kwenda kuipeleleza ile nchi ya Kanani. Naye akawaambia, “Mkaanzie Negebu hadi mahali pa milima.
18 Examine the land to see what it is like. Observe the people who live there, whether they are strong or weak, and whether they are few or many.
Kaipelelezeni nchi kujua ni nchi ya namna gani. Wachunguzeni watu wake, kama ni watu wenye nguvu au dhaifu, kama ni wachache au ni wengi.
19 See what the land is like where they live. Is it good or bad? What cities are there? Are they like camps, or are they fortified cities?
Chunguzeni nchi hiyo wanayoishi ni nchi ya namna gani. Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje? Je iko kama kambi au ni miji yenye ngome?
20 See what the land is like, whether it is good for growing crops or not, and whether there are trees there or not. Be brave and bring back samples of the land's produce.” Now the time was the season for the first ripe grapes.
Chunguzeni ni nchi ya namna gani, kama ni njema kwa mazao au la kama kuna miti au hapana. Mwe hodari mkalete sampuli za mazao ya nchi,” Sasa ni muda wa msimu wa malimbuko ya mizabibu.
21 So the men went up and examined the land from the wilderness of Zin to Rehob, near Lebo Hamath.
Kwa hiyo wale wanaume wakaenda kuipeleleza ile nchi kutoka jangwa la Sini mpaka Rehobi, karibu na Lebo Hamati.
22 They went up from the Negev and arrived at Hebron. Ahiman, Sheshai, and Talmai, clans descended from Anak, were there. Now Hebron had been built seven years before Zoan in Egypt.
Walienda kutoka Negebu nao wakafika Hebroni. Ahimani, Sheshai, na Talmai, Uzao wa Anaki nao walikuweko, Sasa Hebroni ilikuwa imejengwa miaka saba iliyokuwa imepita kabla ya Zoani wa Misri.
23 When they reached the Valley of Eshkol, they cut down a branch with a cluster of grapes. They carried it on a staff between two of their group. They also brought pomegranates and figs.
Nao walipofika katika bonde la Eshikoli, walikata matawi ya mizabibu lenye kishada cha zabibu. Na makundi mawili ya wapelelezi wakakibeba kwenye mti. Pia wakaleta makomamanga na mtini.
24 That place was named the Valley of Eshkol, because of the grape cluster that the people of Israel cut down there.
Mahali pale paliitwa Eshikoli, kwa sababu ya kishada cha mizabibu ambacho wana wa Israeli walikata kule.
25 After forty days, they returned from examining the land.
Baada ya siku arobaini, wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
26 They came back to Moses, Aaron, and all the community of the people of Israel in the wilderness of Paran, at Kadesh. They brought back word to them and to all the community, and showed them the produce from the land.
Wakaja kwa Musa, Haruni na kwa watu wote wa Israeli katka jangwa la Parani, kule Kadeshi. Wakaleta taarifa kwao na kwa Waisraeli wote, na kuwaonyesha matunda ya nchi ile.
27 They told Moses, “We reached the land to which you sent us. It certainly flows with milk and honey. Here is some produce from it.
Wakamwambia Musa, “Tulifika katika ile nchi uliyotutuma. Kwa hakika ni nchi ya kutiririka maziwa na asali. Na baadhi ya matunda yake ni haya hapa.
28 However, the people who make their homes there are strong. The cities are fortified and very large. We also saw descendants of Anak there.
Hata hivyo, watu wanaoishi huko ni wenye nguvu. Miji yao ni mikubwa tena ina maboma. Pia tuliwaona wana wa Anaki huko.
29 The Amalekites live in the Negev. The Hittites, Jebusites, and Amorites have their homes in the hill country. The Canaanites live by the sea and along the Jordan River.”
Waamaleki wanaishi Negebu. Wahiti, Wayebusi, na Waamori nao wanaishi katika milima ya hiyo nchi. Wakanaani wanaishi kando ya bahari na mto Yorodani.”
30 Then Caleb silenced the people who were before Moses and said, “Let us go up and take possession of the land, for we are certainly able to conquer it.”
Kisha Kalebu akawatuliza watu waliokuwa mbele ya Musa, akasema, “Twendeni tukaiteke nyara hiyo nchi, kwa kuwa tuna uhakika wa kuikamata.”
31 But the other men who had gone with him said, “We are not able to attack the people because they are stronger than we are.”
Lakini wale watu waliokuwa wameenda naye walisema, “Hatutaweza kuwashinda hao watu kwa kuwa wao ni hodari kuliko sisi.”
32 So they spread around a discouraging report to the people of Israel about the land that they had examined. They said, “The land that we looked at is a land that eats up its inhabitants. All the people whom we saw there are people of great height.
Kwa hiyo wakasambaza taarifa za kukatisha tamaa kwa Wana wa Israeli juu ya nchi ile waliyoipeleleza. Walisema, “Ile nchi tuliyoiona ni nchi inayowala watu wake. Watu wote tuliowaona ni watu warefu.
33 There we saw giants, descendants of Anak, people who came from giants. In our own sight we were like grasshoppers in comparison with them, and this is what we were in their sight, too.”
Kule tuliiona majitu, wana wa uzao wa Anaki, ambao nii uzao wa majitu. Sisi tulionekana kama panzi machoni mwao tulipojilingsnisha nao, hivyo ndivyo tulivyoonekana machoni mwao pia.”