< Numbers 12 >

1 Then Miriam and Aaron spoke against Moses because of the Cushite woman whom he had married.
Kisha Miriamu na Haruni wakasema kinyume na Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi ambaye alikuwa amemwoa.
2 They said, “Has Yahweh spoken only with Moses? Has he not spoken also with us?” Now Yahweh heard what they said.
Walisema. “Hivi BWANA amesema na Musa tu? Ni kweli hajawahi kusema nasi pia? Sasa BWANA akasikia kile walichokuwa wanaongea. Sasa
3 Now the man Moses was very humble, humbler than anyone else on earth.
Musa alikuwa mtu mpole sana, mpole kuliko mtu yeyote duniani.
4 Right away Yahweh spoke to Moses, Aaron, and Miriam: “Come out, you three, to the tent of meeting.” So the three of them went out.
Wakati huo, BWANA akanena na Musa, Haruni na Miriamu: “tokeni nje ninyi watatu kwenye hema ya kukutania.” kwa hiyo wale watatu wakatokanje.
5 Then Yahweh came down in a pillar of cloud. He stood at the entrance to the tent and called Aaron and Miriam. They both came forward.
Kisha BWANA akashuka katika nguzo ya wingu. Akasimama kwenye lango la hema na akamwita Haruni na Miriamu. wote wakaja mbele.
6 Yahweh said, “Now listen to my words. When a prophet of mine is with you, I will reveal myself to him in visions and speak to him in dreams.
BWANA akasema, “Sasa sikilizeni maneo yangu, Nabii wangu anapokuwa nanyi, Mimi nitajifunua kwake kwa maono na kusema naye katika ndoto.
7 My servant Moses is not like that. He is faithful in all my house.
Lakini si hivyo kwa mtumishi wangu Musa. Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote.
8 I speak to Moses directly, not with visions or riddles. He sees my form. So why are you unafraid to speak against my servant, against Moses?”
Mimi huongea na Musa moja kwa moja, si kwa maono wala mafumbo. Yeye huniona umbo langu. Kwa hiyo, kwa nini hamuogoopi kumnenea kinyume, mtumishi wangu Musa?”
9 Yahweh's anger burned against them, and then he left them.
Hasira ya BWANA ikawawakia, kisha akawaacha.
10 The cloud rose from over the tent, and Miriam was suddenly leprous—she was as white as snow. When Aaron turned toward Miriam, he saw that she had leprosy.
Lile wingu likainuka juu ya hema, Miriamu akapata ukoma ghafla - akawa mweupe kama theluji. Naye Haruni alipogeuka kumwona Miriamu, akamwona amepata ukoma.
11 Aaron said to Moses, “Oh, my master, please do not hold this sin against us. We have spoken foolishly, and we have sinned.
Haruni akamwambia Musa, “Bwana wangu, usituadhibu kwa uovu wetu huu. Tumenena katka upumbuvu, na tumetenda dhambi.
12 Please do not let her be like a dead newborn whose flesh is half consumed when it emerges from its mother's womb.”
Tafadhali nakuomba usimwache akawa kama mtoto mchanga aliyekufa ambaye nusu ya nyama yake imeoza tangu kuzaliwa”
13 So Moses called out to Yahweh. He said, “Please heal her, God, please.”
Kwa hiyo Musa akamwomba BWANA, akasema, “Mungu ninakusihi umponye tafadhali.”
14 Yahweh said to Moses, “If her father had spit in her face, she would be disgraced for seven days. Shut her outside the camp for seven days. After that bring her in again.”
BWANA akamwambia Musa, “kama baba yake angemtemea usoni angepata aibu kwa muda wa siku saba. Umfungie nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Kisha umrejeshe ndani tena.”
15 So Miriam was shut outside the camp for seven days. The people did not journey until she had returned to the camp.
Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba. Watu hawakusafiri mpaka aliporudi kambini.
16 After that, the people journeyed from Hazeroth and camped in the wilderness of Paran.
Kisha watu wakasafiri kutoka Hazeroti na kuweka kambi kwenye jangwa la Parani.

< Numbers 12 >