< Numbers 10 >

1 Yahweh spoke to Moses. He said,
Bwana akamwambia Mose:
2 “Make two silver trumpets. Hammer the silver to make them. You must use the trumpets to call the community together and to call the community to move their camps.
“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
3 The priests must blow the trumpets to call all the community together in front of you at the entrance to the tent of meeting.
Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
4 If the priests blow only one trumpet, then the leaders, the heads of the clans of Israel, must gather to you.
Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
5 When you blow a loud signal, the camps on the east side must begin their journey.
Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
6 When you blow a loud signal the second time, the camps on the south side must begin their journey. They must blow a loud signal for their journeys.
Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
7 When the community gathers together, blow the trumpets, but not loudly.
Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
8 The sons of Aaron, the priests, must blow the trumpets. This will always be a regulation for you throughout your people's generations.
“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
9 When you go to war in your land against an adversary who oppresses you, then you must sound an alarm with the trumpets. I, Yahweh your God, will call you to mind and save you from your enemies.
Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
10 Also, at the times of celebration, both your regular festivals and at the beginnings of the months, you must blow the trumpets over your burnt offerings and over the sacrifices for your fellowship offerings. These will act as a reminder of you to me, your God. I am Yahweh your God.”
Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
11 In the second year, in the second month, on the twentieth day of the month, the cloud was lifted from the tabernacle of the covenant decrees.
Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
12 The people of Israel then went on their journey from the wilderness of Sinai. The cloud stopped in the wilderness of Paran.
Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
13 They made their first journey, following Yahweh's command given through Moses.
Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
14 The camp under the banner of Judah's descendants went out first, moving out their individual armies. Nahshon son of Amminadab led Judah's army.
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
15 Nethanel son of Zuar led the army of the tribe of Issachar's descendants.
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
16 Eliab son of Helon led the army of the tribe of Zebulun's descendants.
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
17 The descendants of Gershon and of Merari, who cared for the tabernacle, took down the tabernacle and then set out on their journey.
Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
18 Next, the armies under the banner of Reuben's camp set out on their journey. Elizur son of Shedeur led Reuben's army.
Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
19 Shelumiel son of Zurishaddai led the army of the tribe of Simeon's descendants.
Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
20 Eliasaph son of Deuel led the army of the tribe of Gad's descendants.
naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
21 The Kohathites set out. They carried the sanctuary's holy equipment. Others would set up the tabernacle before the Kohathites arrived at the next camp.
Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
22 The armies under the banner of Ephraim's descendants set out next. Elishama son of Ammihud led Ephraim's army.
Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
23 Gamaliel son of Pedahzur led the army of the tribe of Manasseh's descendants.
Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
24 Abidan son of Gideoni led the army of the tribe of Benjamin's descendants.
naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
25 The armies that camped under the banner of Dan's descendants set out last. Ahiezer son of Ammishaddai led Dan's army.
Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
26 Pagiel son of Okran led the army of the tribe of Asher's descendants.
Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
27 Ahira son of Enan led the army of the tribe of Naphtali's descendants.
naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
28 This is the way that the armies of the people of Israel set out on their journey.
Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
29 Moses spoke to Hobab son of Reuel the Midianite. Reuel was the father of Moses' wife. Moses spoke to Hobab and said, “We are traveling to a place that Yahweh described. Yahweh said, 'I will give it to you.' Come with us and we will do you good. Yahweh has promised to do good for Israel.”
Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
30 But Hobab said to Moses, “I will not go with you. I will go to my own land and my own people.”
Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
31 Then Moses replied, “Please do not leave us. You know how to camp in the wilderness. You must watch out for us.
Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
32 If you go with us, we will do for you the same good that Yahweh does to us.”
Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
33 They journeyed from the mountain of Yahweh for three days. The ark of the covenant of Yahweh went before them for three days to find a place for them to rest.
Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
34 Yahweh's cloud was over them by daylight as they journeyed.
Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
35 Whenever the ark set out, Moses would say, “Rise up, Yahweh. Scatter your enemies. Make those who hate you run from you.”
Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
36 Whenever the ark stopped, Moses would say, “Return, Yahweh, to Israel's many tens of thousands.”
Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”

< Numbers 10 >