< Nehemiah 9 >

1 Now on the twenty-fourth day of the same month the people of Israel were assembled and they were fasting, and they were wearing sackcloth, and they put dust on their heads.
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
2 The descendants of Israel separated themselves from all the foreigners. They stood and confessed their own sins and the evil actions of their ancestors.
Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
3 They stood up in their places, and for one-fourth of the day they read from the book of the law of Yahweh their God. For another fourth of the day they were confessing and bowing down before Yahweh their God.
Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
4 The Levites, Jeshua, Bani, Kadmiel, Shebaniah, Bunni, Sherebiah, Bani, and Kenani, stood on the stairs and they called out with a loud voice to Yahweh their God.
Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
5 Then the Levites, Jeshua, and Kadmiel, Bani, Hashabneiah, Sherebiah, Hodiah, Shebaniah, and Pethahiah said, “Stand up and give praise to Yahweh your God forever and ever.” “May they bless your glorious name, and may it be exalted above every blessing and praise.
Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
6 You are Yahweh. You alone. You have made heaven, the highest heavens, with all their host, and the earth and everything on it, and the seas and all that is in them. You give life to them all, and the host of heaven worship you.
Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
7 You are Yahweh, the God who chose Abram, and brought him out of Ur of the Chaldees, and gave him the name Abraham.
“Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
8 You found his heart was faithful before you, and you made with him the covenant to give to his descendants the land of the Canaanites, the Hittites, the Amorites, the Perizzites, the Jebusites, and the Girgashites. You have kept your promise because you are righteous.
Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
9 You saw the affliction of our forefathers in Egypt and you heard their cry by the Sea of Reeds.
“Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
10 You gave signs and wonders against Pharaoh, and all his servants, and on all the people of his land, for you knew that the Egyptians acted with arrogance against them. But you made a name for yourself which stands to this day.
Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
11 Then you divided the sea before them, so that they went through the middle of the sea on the dry land; and threw those who pursued them into the depths, as a stone into deep waters.
Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
12 You led them by a pillar of cloud during by day, and by a pillar of fire during the night to light the way for them to go.
Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
13 On Mount Sinai you came down and you spoke with them from heaven and gave to them righteous decrees and true laws, good statutes and commandments.
“Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
14 You made your holy Sabbath known to them, and you gave them commandments and statutes and a law through Moses your servant.
Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
15 You gave them bread from heaven for their hunger, and water from a rock for their thirst, and you said to them to go in to possess the land you swore on oath to give them.
Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
16 But they and our ancestors acted disrespectfully, and they were stubborn, and did not listen to your commandments.
“Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
17 They refused to listen, and they did not think about the wonders that you had done among them, but became stubborn, and in their rebellion they appointed a leader to return to their slavery. But you are a God who is full of forgiveness, gracious and compassionate, slow to anger, and abounding in steadfast love. You did not abandon them.
Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
18 Even when they had cast a calf out of molten metal and said, 'This is your God who brought you up out of Egypt,' and had committed great blasphemies,
hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
19 you, in your compassion, did not abandon them in the wilderness. The pillar of cloud to lead them on the way did not leave them during day, neither did the pillar of fire by night to light the way for them to go.
“Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
20 Your good Spirit you gave them to instruct them, and your manna you did not withhold from their mouths, and water you gave them for their thirst.
Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
21 For forty years you provided for them in the wilderness, and they lacked nothing. Their clothes did not wear out and their feet did not swell.
Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
22 You gave them kingdoms and peoples, assigning to them every corner of the land. Then they took possession of the land of Sihon king of Heshbon and the land of Og king of Bashan.
“Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
23 You made their children as numerous as the stars of heaven, and you brought them into the land that you told their ancestors to go in and possess.
Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
24 So the people went in and possessed the land and you subdued before them the inhabitants of the land, the Canaanites. You gave them into their hands, with their kings and the peoples of the land, that Israel might do with them as they pleased.
Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
25 They captured the fortified cities and a productive land, and they captured houses full of all good things, cisterns already cut out, vineyards and olive orchards, and fruit trees in abundance. So they ate and were satisfied and grew fat and enjoyed themselves in your great goodness.
Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
26 Then they became disobedient and they rebelled against you. They threw your law behind their backs. They murdered your prophets who had warned them to turn back to you, and they committed great blasphemies.
“Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
27 So you gave them into the hand of their enemies, who made them suffer. In the time of their suffering, they cried out to you, and you heard them from heaven, and because of your great mercies you sent them rescuers who rescued them out of the hand of their enemies.
Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
28 But after they had rest, they did evil again before you, and you abandoned them to the hand of their enemies, so their enemies ruled over them. Yet when they returned and cried out to you, you heard from heaven, and many times because of your compassion you rescued them.
“Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
29 You warned them so they might turn back to your law. Yet they acted arrogantly and did not listen to your commands. They sinned against your decrees which give life to anyone who obeys them. They gave the stubborn shoulder-blade and stiffened their neck and refused to listen.
“Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
30 For many years you put up with them and warned them by your Spirit through your prophets. Yet they did not listen. So you gave them into the hand of the neighboring peoples.
Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
31 But in your great mercies you did not make a complete end of them, or forsake them, for you are a gracious and merciful God.
Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
32 Now therefore, our God—you great, mighty, and awesome God who keep your covenant and steadfast love—do not let all this hardship seem little to you that has come on us, on our kings, on our princes, and on our priests, and on our prophets, and on our ancestors, and on all your people from the days of the kings of Assyria until today.
“Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
33 You are just in everything that has come on us, for you have dealt faithfully, but we have acted wickedly.
Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
34 Our kings, our princes, our priests, and our ancestors have not kept your law, nor paid attention to your commandments or your covenant decrees by which you warned them.
Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
35 Even in their own kingdom, while they enjoyed your great goodness to them, in the large and productive land you set before them, they did not serve you or turn away from their evil ways.
Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
36 Now we are slaves in the land you gave our ancestors to enjoy its fruit and its good gifts, and behold, we are slaves in it!
“Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
37 The rich yield from our land goes to the kings you have set over us because of our sins. They rule over our bodies and over our livestock as they please. We are in great distress.
Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
38 Because of all this, we make a firm covenant in writing. On the sealed document are the names of our princes, Levites, and priests.”
“Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”

< Nehemiah 9 >