< Nehemiah 7 >
1 When the wall was finished and I had set up the doors in place, and the gatekeepers and singers and Levites had been appointed,
Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
2 I gave my brother Hanani charge over Jerusalem, along with Hananiah who had oversight of the fortress, for he was a faithful man and feared God more than many.
Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
3 I said to them, “Do not open the gates of Jerusalem until the sun is hot. While the gatekeepers are on guard, you may shut the doors and bar them. Appoint guards from those who live in Jerusalem, some at the place of their guard station, and some in front of their own homes.”
Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
4 Now the city was wide and large, but there were few people within it, and no houses had yet been rebuilt.
Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
5 My God put into my heart to gather together the nobles, the officials, and the people to enroll them by their families. I found the book of the genealogy of those who returned at the first and found the following written in it.
Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
6 “These are the people of the province who went up out of the captivity of those exiles whom Nebuchadnezzar the king of Babylon took into exile. They returned to Jerusalem and to Judah, each to his city.
Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
7 They came with Zerubbabel, Jeshua, Nehemiah, Azariah, Raamiah, Nahamani, Mordecai, Bilshan, Mispereth, Bigvai, Nehum, and Baanah. The number of the men of the people of Israel included the following.
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
8 The descendants of Parosh, 2,172.
wazao wa Paroshi 2,172
9 The descendants of Shephatiah, 372.
wazao wa Shefatia 372
10 The descendants of Arah, 652.
wazao wa Ara 652
11 The descendants of Pahath-Moab, through the descendants of Jeshua and Joab, 2,818.
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
12 The descendants of Elam, 1,254.
wazao wa Elamu 1,254
13 The descendants of Zattu, 845.
wazao wa Zatu 845
14 The descendants of Zakkai, 760.
wazao wa Zakai 760
15 The descendants of Binnui, 648.
wazao wa Binui 648
16 The descendants of Bebai, 628.
wazao wa Bebai 628
17 The descendants of Azgad, 2,322.
wazao wa Azgadi 2,322
18 The descendants of Adonikam, 667.
wazao wa Adonikamu 667
19 The descendants of Bigvai, 2,067.
wazao wa Bigwai 2,067
20 The descendants of Adin, 655.
wazao wa Adini 655
21 The descendants of Ater, of Hezekiah, 98.
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
22 The descendants of Hashum, 328.
wazao wa Hashumu 328
23 The descendants of Bezai, 324.
wazao wa Besai 324
24 The descendants of Hariph, 112.
wazao wa Harifu 112
25 The descendants of Gibeon, 95.
wazao wa Gibeoni 95
26 The men from Bethlehem and Netophah, 188.
watu wa Bethlehemu na Netofa 188
27 The men from Anathoth, 128.
watu wa Anathothi 128
28 The men of Beth Azmaveth, 42.
watu wa Beth-Azmawethi 42
29 The men of Kiriath Jearim, Kephirah, and Beeroth, 743.
watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
30 The men of Ramah and Geba, 621.
watu wa Rama na Geba 621
31 The men of Michmas, 122.
watu wa Mikmashi 122
32 The men of Bethel and Ai, 123.
watu wa Betheli na Ai 123
33 The men of the other Nebo, 52.
watu wa Nebo 52
34 The people of the other Elam, 1,254.
wazao wa Elamu 1,254
35 The men of Harim, 320.
wazao wa Harimu 320
36 The men of Jericho, 345.
wazao wa Yeriko 345
37 The men of Lod, Hadid, and Ono, 721.
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
38 The men of Senaah, 3,930.
wazao wa Senaa 3,930
39 The priests: The descendants of Jedaiah (of the house of Jeshua), 973.
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
40 The descendants of Immer, 1,052.
wazao wa Imeri 1,052
41 The descendants of Pashhur, 1,247.
wazao wa Pashuri 1,247
42 The descendants of Harim, 1,017.
wazao wa Harimu 1,017
43 The Levites: The descendants of Jeshua, of Kadmiel, of Binnui, and of Hodevah, 74.
Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
44 The singers: The descendants of Asaph, 148.
Waimbaji: wazao wa Asafu 148
45 The gatekeepers of the descendants of Shallum, the descendants of Ater, the descendants of Talmon, the descendants of Akkub, the descendants of Hatita, the descendants of Shobai, 138.
Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
46 The temple servants: The descendants of Ziha, the descendants of Hasupha, the descendants of Tabbaoth,
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
47 the descendants of Keros, the descendants of Sia, the descendants of Padon,
wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
48 the descendants of Lebana, the descendants of Hagaba, the descendants of Shalmai,
wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
49 the descendants of Hanan, the descendants of Giddel, the descendants of Gahar.
wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
50 The descendants of Reaiah, the descendants of Rezin, the descendants of Nekoda,
wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
51 the descendants of Gazzam, the descendants of Uzza, the descendants of Paseah,
wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
52 the descendants of Besai, the descendants of Meunim, the descendants of Nephushesim.
wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
53 The descendants of Bakbuk, the descendants of Hakupha, the descendants of Harhur,
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
54 the descendants of Bazluth, the descendants of Mehida, the descendants of Harsha,
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
55 the descendants of Barkos, the descendants of Sisera, the descendants of Temah,
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
56 the descendants of Neziah, the descendants of Hatipha.
wazao wa Nesia na Hatifa.
57 The descendants of Solomon's servants: the descendants of Sotai, the descendants of Sophereth, the descendants of Perida,
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
58 the descendants of Jaala, the descendants of Darkon, the descendants of Giddel,
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
59 the descendants of Shephatiah, the descendants of Hattil, the descendants of Pochereth Hazzebaim, the descendants of Amon.
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
60 All the temple servants, and the descendants of Solomon's servants, were 392.
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
61 These were the people who went up from Tel Melah, Tel Harsha, Kerub, Addon, and Immer. But they could not prove that they or their ancestors' families were descendants from Israel:
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
62 the descendants of Delaiah, the descendants of Tobiah, and the descendants of Nekoda, 642.
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
63 Those who were from the priests: the descendants of Habaiah, Hakkoz, and Barzillai (who took his wife from the daughters of Barzillai of Gilead and was called by their name).
Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
64 These sought their records among those enrolled by their genealogy, but they could not be found, so they were excluded from the priesthood as unclean.
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
65 Then the governor said to them that they should not be allowed to eat the priests' share of food from the sacrifices until there rose up a priest with Urim and Thummim.
Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
66 The whole assembly together was 42,360,
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
67 besides their male servants and their female servants, of whom there were 7,337. They had 245 singing men and women.
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
68 Their horses were 736 in number, their mules, 245,
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
69 their camels, 435, and their donkeys, 6,720.
ngamia 435 na punda 6,720.
70 Some from among the heads of ancestors' families gave gifts for the work. The governor gave to the treasury one thousand darics of gold, 50 basins, and 530 priestly garments.
Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
71 Some of the heads of ancestors' families gave into the treasury for the work twenty thousand darics of gold and 2,200 minas of silver.
Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
72 The rest of the people gave twenty thousand darics of gold, and two thousand minas of silver, and sixty-seven priestly garments.
Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
73 So the priests, the Levites, the gatekeepers, the singers, some of the people, the temple servants, and all Israel lived in their cities. By the seventh month the people of Israel were settled in their cities.”
Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,