< Nahum 1 >

1 The declaration about Nineveh. The book of the vision of Nahum, the Elkoshite.
Maono kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono ya Nahumu, Mwelkoshi.
2 Yahweh is a jealous God and avenges; Yahweh avenges and is full of wrath; Yahweh takes vengeance on his adversaries, and he continues his anger for his enemies.
Yehova ni Mungu mwenye wivu na analipa kisasi; Yehova hulipa kisasi na amejaa ghadhabu; Yohova analipiza kisasi kwa adui zake, na huiendeleza hasira yake kwa adui zake.
3 Yahweh is slow to anger and great in power; he will not allow the wicked to go unpunished. Yahweh makes his way in the whirlwind and the storm, and the clouds are the dust of his feet.
Yehova ni mwenye nguvu nyingi na mpole wa hasira; hatakuwa na namna ya kuacha kuwahesabia hatia adui zake. Yehova hufanya njia yake kwenye upepo wa kisulisuli na dhoruba, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.
4 He rebukes the sea and makes it dry; he dries up all the rivers. Bashan is weak, and Carmel also; the flowers of Lebanon are weak.
Huikemea bahari na kuifanya ikauke; hukausha mito yote. Bashani ni dhaifu, na Karmeli pia; maua ya Lebanoni ni dhaifu.
5 The mountains shake in his presence, and the hills melt; the earth collapses in his presence, indeed, the world and all people who live in it.
Milima hutetema kwenye uwepo wake, na vilima huyeyuka; dunia huanguka mbele zake, kabisa, dunia na watu wote wanaoishi ndani yake.
6 Who can stand before his wrath? Who can resist the fierceness of his anger? His wrath is poured out like fire, and the rocks are broken apart by him.
Ni nani anaweza kusimama mbele ya ghadhabu yake? Nani anaweza kuzuia ukali wa hasira yake? Ghadhabu yake imemwagwa kama moto, na miamba ameibomoa mbalimbali.
7 Yahweh is good, a stronghold in the day of trouble; and he is faithful to those who take refuge in him.
Yehova ni mwema, boma katika siku ya taabu; na yeye ni mwaminifu kwa wale wanaomkimbilia.
8 But he will make a full end to his enemies with an overwhelming flood; he will pursue them into darkness.
Lakini atafanya mwisho wa adui zake kwa mafuriko ya kutisha; atawawinda kwenye giza.
9 What are you people plotting against Yahweh? He will make a full end to it; trouble will not rise up a second time.
Watu wanapanga nini dhidi ya Yehova? Yeye atakomesha; taabu haitainuka mara ya pili.
10 For they will become tangled up like thornbushes; they will be saturated in their own drink; they will be completely devoured by fire like dry stubble.
Maana watakuwa wamevurugika kama michongoma; wataloweshwa katika kinywaji chao mwenyewe; wataharibiwa kabisa kwa moto kama mashina ya mabua.
11 Someone arose among you, Nineveh, who planned evil against Yahweh, someone who promoted wickedness.
Mtu mmoja aliinuka miongoni mwenu, Ninawi, aliyepanga ubaya dhidi ya Yehova, mtu ambaye aliimarisha uovu.
12 This is what Yahweh says, “Even if they are at their full strength and full numbers, they will nevertheless be sheared; their people will be no more. But you, Judah: Though I have afflicted you, I will afflict you no more.
Hivi ndivyo anavyosema Yehova, “Hata kama wananguvu zao timilifu na idadi timilifu, hata hivyo watanyolewa, watu wao hawatakuwepo tena. Bali wewe, Yuda: Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.
13 Now will I break that people's yoke from off you; I will break your chains.”
Sasa nitaivunja ile nira ya watu kutoka kwako; nitaikata minyororo yako.
14 Yahweh has given a command about you, Nineveh: “There will be no more descendants bearing your name. I will cut off the carved figures and the cast metal figures from the houses of your gods. I will dig your graves, for you are contemptible.”
Yehova ametoa amri juu yako, Ninawi: “Hakutakuwa na kizazi tena chenye kubeba jina lako. Nitazizuia sanamu zilizochongwa na kuziondoa sanamu za chuma kutoka kwenye nyumba za miungu yenu. Nitachimba makaburi yenu, kwa kudharauliwa kwenu.”
15 Look, on the mountains there are the feet of someone who is bringing good news, who is announcing peace! Celebrate your festivals, Judah, and keep your vows, for the wicked one will invade you no more; he is completely cut off.
Tazama, juu ya milima kuna miguu ya mtu aletaye habari njema, anayetangaza amani! Sherehekeeni sikukuu zenu, Yuda, na tunzeni nadhiri zenu, kwa maana mwovu hatawavamia tena; ameondolewa kabisa.

< Nahum 1 >