< Micah 6 >

1 Now listen to what Yahweh says, “Arise and state your case before the mountains; let the hills hear your voice.
Sasa sikilizeni kile ambacho Yahwe asemacho, “Inuka na ueleze kesi yako mbele ya milima; acha milima isikie sauti yako.
2 Listen to Yahweh's lawsuit, you mountains, and you enduring foundations of the earth. For Yahweh has a lawsuit with his people, and he will fight in court against Israel.”
Sikilizeni madai ya Yahwe, enyi milima, na ninyi misingi mivumilivu ya dunia. Kwa kuwa Yahwe anavumilia pamoja na watu wake, na atapigana katika mahakama juu ya Israeli.”
3 “My people, what have I done to you? How have I wearied you? Testify against me!
Watu wangu, nimefanya nini kwenu? nimewachosha mara ngapi? shuhudieni dhidi yangu!
4 For I brought you up out of the land of Egypt and rescued you out of the house of bondage. I sent Moses, Aaron, and Miriam to you.
Kwa kuwa niliwaleta kutoka nchi ya Msiri na kuwaokoa kutoka kwenye nyumba ya utumwa. Nawatuma Musa, Aruni, na Mariamu kwako.
5 My people, remember what Balak king of Moab devised, and how Balaam son of Beor answered him as you went from Shittim to Gilgal, so you may know the righteous acts of Yahweh.”
Watu wangu, kumbukeni ambavyo Balaki mfalme wa Moabu alivyotunga, na vile ambavyo Balamu mwana wa Beori alivyomjibu kama ulipokuwa ukienda kutoka kwa Gilgali, hivyo mnaweza kujua matendo ya haki ya Yahwe.”
6 What should I bring to Yahweh, as I bow down to the high God? Should I come to him with burnt offerings, with calves a year old?
Je nilete nini kwa Yahwe, ninapoenda kumwinamia Mungu aliye juu? Je ninaweza kuja kwake na sadaka za kuteketeza, pamoja na ndama wenye mwaka mmoja?
7 Will Yahweh be pleased with thousands of rams, or with ten thousand rivers of oil? Should I give my firstborn for my transgression, the fruit of my body for my own sin?
Je Yahwe atapendezwa na maelfu ya kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, tunda la mwili wangu kwa ajili ya dhambi yangu mwenyewe?
8 He has told you, man, what is good, and what Yahweh requires from you: Act justly, love kindness, and walk humbly with your God.
Amekwambia, mtu, kile kilicho bora, na kile ambacho Yahwe atakacho kutoka kwako: Kutenda haki, kupenda ukarimu, na kutembea kwa unyenyekevu pamoja na Mungu wako.
9 The voice of Yahweh is making a proclamation to the city— even now wisdom acknowledges your name: “Pay attention to the rod, and to the one who has put it in place.
Sauti ya Yahwe inatangaza kwenye mji-hata sasa hekima hukukiri jina lako: “Kaa tayari kwa ajili ya fimbo, na kwa yule aliyeiweka.
10 There is wealth in the houses of the wicked that is dishonest, and false measures that are abominable.
Kuna utajiri katika nyumba za waovu, na kipimo cha uongo hilo ni chukizo mno.
11 Should I consider a person to be innocent if he uses fraudulent scales, with a bag of deceptive weights?
Ningeweza kumfikira mtu kuwa hana hatia kama anatumia kipimo cha ulaghai, pamoja na mfuko wa kipimo wa udanganyifu?
12 The rich men are full of violence, the inhabitants have spoken lies, and their tongue in their mouth is deceitful.
Matajiri wamejaa uharibifu, makazi yao yamesema uongo, na ulimi wao katika midomo yao unaudanganyifu.
13 Therefore I will strike you with a terrible blow, and I will make you desolate because of your sins.
Kwa hiyo nimekupiga kwa pigo linaloumiza, nimekufanya gofu kwa sababu ya dhambi zako.
14 You will eat but not be satisfied; your emptiness will remain inside you. You will store goods away but not save, and what you do save I will give to the sword.
Utakula lakini hutatosheka; utupu wako utabakia ndani yako. Utatunza mizigo mbali lakini hutahifadhi, na kile unachokihifadhi nitakitoa kwa upanga.
15 You will sow but not reap; you will tread the olives but not anoint yourselves with oil; you will press grapes but drink no wine.
Utapanda lakini huatavuna; utazikusanya zaituni lakini hutajipaka mafuta; utasindika zabibu lakini hutakunywa divai.
16 The regulations made by Omri have been kept, and all the deeds of the house of Ahab. You walk by their advice. So I will make you, city, a ruin, and you inhabitants an object of hissing, and you will bear the reproach of my people.”
Kanuni zilizotengenezwa na Omri zimetunzwa, na matendo yote ya nyumba ya Ahabu. Mnatembea kwa ushauri wao. Hivyo nitakufanya wewe, mji, gofu, na makazi yako jambo la zomeo, na matabeba dharau kama watu wangu.”

< Micah 6 >