< Luke 23 >
1 The whole company of them rose up and brought Jesus before Pilate.
Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
2 They began to accuse him, saying, “We found this man perverting our nation, forbidding to give tribute to Caesar, and saying that he himself is Christ, a king.”
Wakaanza kumshtaki wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme.”
3 Pilate asked him, saying, “Are you the King of the Jews?” Jesus answered him and said, “You say so.”
Pilato akamwuliza Yesu, “Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
4 Pilate said to the chief priests and the multitudes, “I find no fault in this man.”
Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, “Sioni kosa lolote katika mtu huyu.”
5 But they were insisting, saying, “He stirs up the people, teaching throughout all Judea, beginning from Galilee even to this place.”
Lakini wao wakasisitiza wakisema: “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa.”
6 So when Pilate heard this, he asked whether the man was a Galilean.
Pilato aliposikia hayo, akauliza, “Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?”
7 When he discovered that he was under Herod's authority, he sent Jesus to Herod, who himself also was at Jerusalem in those days.
Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
8 When Herod saw Jesus, he was very glad, because he had wanted to see him for a long time. He had heard about him and he hoped to see some miracle done by him.
Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
9 Herod questioned Jesus in many words, but Jesus answered him nothing.
Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
10 The chief priests and the scribes stood, violently accusing him.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11 Herod with his soldiers insulted Jesus and they mocked him. Then they dressed him in elegant clothes and sent him back to Pilate.
Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
12 For Herod and Pilate had become friends with each other that very day, for before this they had been enemies with each other.
Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
13 Pilate then called together the chief priests and the rulers and the crowd of people,
Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
14 and said to them, “You brought to me this man like a man who is leading the people to act badly, and see, I, having questioned him before you, find no fault in this man concerning those things of which you accuse him.
akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
15 No, nor does Herod, for he sent him back to us, and see, nothing worthy of death has been done by him.
Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
16 I will therefore punish him, and release him.”
Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.”
Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18 But they cried out all together, saying, “Away with this man, and release to us Barabbas!”
Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!”
19 Barabbas was a man who had been put into prison for a certain rebellion in the city and for murder.
(Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20 Pilate addressed them again, desiring to release Jesus.
Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21 But they shouted, saying, “Crucify him, crucify him.”
lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
22 He said to them a third time, “Why, what evil has this man done? I have found nothing deserving the death penalty in him. Therefore after punishing him, I will release him.”
Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”
23 But they were insistent with loud voices, demanding for him to be crucified. Their voices convinced Pilate.
Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
24 So Pilate decided to grant their demand.
Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
25 He released the one they asked for who had been put in prison for rioting and murder. But he delivered up Jesus to their will.
Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
26 As they led him away, they seized one Simon of Cyrene, coming from the country, and they laid the cross on him to carry, following Jesus.
Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
27 A great crowd of the people, and of women who grieved and mourned for him, were following him.
Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
28 But turning to them, Jesus said, “Daughters of Jerusalem, do not weep for me, but weep for yourselves and for your children.
Yesu akawageukia, akasema, “Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
29 For see, the days are coming in which they will say, 'Blessed are the barren and the wombs that did not bear, and the breasts that did not nurse.'
Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
30 Then they will begin to say to the mountains, 'Fall on us,' and to the hills, 'Cover us.'
Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
31 For if they do these things while the tree is green, what will happen when it is dry?”
Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?”
32 Other men, two criminals, were led away with him to be put to death.
Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
33 When they came to the place that is called “The Skull,” there they crucified him, and the criminals—one on his right and one on his left.
Walipofika mahali paitwapo, “Fuvu la Kichwa,” ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
34 Jesus said, “Father, forgive them, for they do not know what they are doing.” Then they cast lots, dividing up his garments.
Yesu akasema, “Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya.” Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
35 The people stood watching while the rulers also were mocking him, saying, “He saved others. Let him save himself, if he is the Christ of God, the chosen one.”
Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: “Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!”
36 The soldiers also ridiculed him, approaching him, offering him vinegar,
Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
37 and saying, “If you are the King of the Jews, save yourself.”
wakisema: “Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
38 There was also a sign over him, “This is the King of the Jews.”
Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: “Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi.”
39 One of the criminals who was hanging there insulted him by saying, “Are you not the Christ? Save yourself and us.”
Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: “Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia.”
40 But the other rebuked him, saying, “Do you not fear God, since you are under the same sentence?
Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: “Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
41 We indeed are here justly, for we are receiving what we deserve for our deeds. But this man did nothing wrong.”
Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
42 Then he said, “Jesus, remember me when you come into your kingdom.”
Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.”
43 Jesus said to him, “Truly I say to you, today you will be with me in paradise.”
Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”
44 It was now about the sixth hour, and darkness came over the whole land until the ninth hour
Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
45 as the sun's light failed. Then the curtain of the temple was split in two.
na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
46 Crying with a loud voice, Jesus said, “Father, into your hands I commit my spirit.” Having said this, he died.
Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako.” Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
47 When the centurion saw what was done, he glorified God, saying, “Surely this was a righteous man.”
Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: “Hakika huyu alikuwa mtu mwema.”
48 When all the multitudes who came together to witness this sight saw the things that were done, they returned beating their breasts.
Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
49 But all those who knew him, and the women who followed him from Galilee, stood at a distance, watching these things.
Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
50 Behold, there was a man named Joseph, who was a member of the Council. He was a good and righteous man.
Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
51 This man had not agreed with the decision of the Council and their action. He was from the Judean town of Arimathea; and he was looking for the kingdom of God.
Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
52 This man, approaching Pilate, asked for the body of Jesus.
Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53 He took it down, wrapped it in fine linen, and placed it in a tomb that was cut in stone, where no one had ever been laid.
Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
54 It was the Day of the Preparation, and the Sabbath was about to begin.
Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
55 The women who had come with Jesus out of Galilee followed and saw the tomb and how his body was laid.
Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
56 They returned, and prepared spices and ointments. Then on the Sabbath they rested according to the commandment.
Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.