< Leviticus 17 >

1 Yahweh spoke to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 “Speak to Aaron and to his sons, and to all the people of Israel. Tell them what Yahweh has commanded:
“Sema na Aroni na wanawe, pamoja na Waisraeli wote, uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana aliloagiza:
3 'Any man from Israel who kills an ox, lamb, or goat in the camp, or who kills it outside the camp, in order to sacrifice it—
Mwisraeli yeyote atakayetoa dhabihu ya maksai, mwana-kondoo au mbuzi ndani ya kambi au nje yake,
4 if he does not bring it to the entrance of the tent of meeting to offer it as a sacrifice to Yahweh before his tabernacle, that man is guilty of bloodshed. He has shed blood, and that man must be cut off from among his people.
badala ya kuileta kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili kuileta kama sadaka kwa Bwana mbele ya Maskani ya Bwana, mtu huyo atahesabiwa kuwa na hatia ya kumwaga damu; ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
5 The purpose of this command is so that the people of Israel will bring their sacrifices to Yahweh at the entrance to the tent of meeting, to the priest to be sacrificed as fellowship offerings to Yahweh, instead of offering sacrifices in an open field.
Hii ni ili Waisraeli wamletee Bwana dhabihu wanazozifanya sasa mahali pa wazi mashambani. Ni lazima wazilete kwa makuhani, yaani kwa Bwana, katika ingilio la Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu kama sadaka za amani.
6 The priest will sprinkle the blood on Yahweh's altar at the entrance to the tent of meeting; he will burn the fat for it to produce a sweet aroma for Yahweh.
Kuhani atanyunyiza damu kwenye madhabahu ya Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania, na kuyateketeza mafuta ya hiyo dhabihu kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
7 The people must no longer offer their sacrifices to goat idols, for which they act as prostitutes. This will be a permanent statute for them throughout their people's generations.'
Hawatatoa kamwe dhabihu zao kwa sanamu za mbuzi ambazo wamekuwa wakijifanyia nazo ukahaba. Hili litakuwa agizo la kudumu kwao na kwa ajili ya vizazi vijavyo.’
8 You must say to them, 'Any man of Israel, or any foreigner who lives among them, who offers a burnt offering or sacrifice
“Waambie: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi miongoni mwao atakayetoa sadaka ya kuteketezwa au dhabihu
9 and does not bring it to the entrance of the tent of meeting in order to sacrifice it to Yahweh, that man must be cut off from his people.
bila kuileta kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili kutoa dhabihu kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
10 If any person of the house of Israel, or any foreigner who lives among them consumes any blood, I will set my face against that person who consumes blood and I will cut him off from among his people.
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi miongoni mwao ambaye atakunywa damu yoyote, nitakuwa kinyume cha mtu huyo atakayekunywa damu na kumkatilia mbali na watu wake.
11 For the life of an animal is in its blood. I have given its blood to you to make atonement on the altar for your lives, because it is the blood that makes atonement, for it is the blood that atones for the life.
Kwa kuwa uhai wa kiumbe uko ndani ya damu, nami nimewapa hiyo damu ili mfanyie upatanisho kwa ajili yenu wenyewe juu ya madhabahu; damu ndiyo ifanyayo upatanisho kwa ajili ya maisha ya mtu.
12 Therefore I said to the people of Israel that no one among you must eat blood, neither may any foreigner who lives among you eat blood.
Kwa hiyo, ninawaambia Waisraeli, “Hakuna hata mmoja wenu anayeruhusiwa kunywa damu, wala mgeni anayeishi miongoni mwenu haruhusiwi kunywa damu.”
13 Anyone of the people of Israel, or any of the foreigners who live among them, who hunts and kills an animal or bird that may be eaten, that person must pour out its blood and cover the blood with earth.
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye atamwinda mnyama au ndege anayeruhusiwa kuliwa ni lazima aimwage damu na kuifunika kwa udongo,
14 For the life of each creature is its blood. That is why I said to the people of Israel, “You must not eat the blood of any creature, for the life of every living creature is its blood. Whoever eats it must be cut off.”
kwa sababu uhai wa kila kiumbe ni katika damu yake. Ndiyo sababu nimewaambia Waisraeli, “Kamwe msinywe damu ya kiumbe chochote, kwa sababu uhai wa kila kiumbe ni katika damu yake; yeyote atakayekunywa damu ni lazima akatiliwe mbali.”
15 Every person who eats an animal that has died or that has been torn by wild animals, whether that person is native born or a foreigner living among you, he must wash his clothes and bathe himself in water, and he will be unclean until the evening. Then he will be clean.
“‘Mtu yeyote, awe mzawa au mgeni, ambaye atakula mzoga wa kitu chochote ama kilichouawa na wanyama mwitu ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni, kisha atakuwa safi.
16 But if he does not wash his clothes or bathe his body, then he must carry his guilt.'”
Lakini kama hakufua nguo zake na kuoga, atakuwa na hatia kwa kosa hilo.’”

< Leviticus 17 >