< Judges 4 >

1 After Ehud died, the people of Israel once again did what was evil in the sight of Yahweh.
Baada ya Ehudi kufa, watu wa Israeli walifanya tena yaliyo mabaya machoni pa Bwana.
2 Yahweh sold them into the hand of Jabin king of Canaan who reigned in Hazor. The commander of his army was named Sisera, and he lived in Harosheth Haggoyim.
Bwana akawatia mkononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyewala huko Hasori. Kamanda wa jeshi lake aitwaye Sisera, naye aliishi Harosheti ya Mataifa.
3 The people of Israel called out to Yahweh for help, because Sisera had nine hundred iron chariots and he oppressed the people of Israel with force for twenty years.
Wana wa Israeli wakamwomba Bwana awasaidie, kwa sababu Sisera alikuwa na magari ya chuma mia tisa na akawashinda wana wa Israeli kwa nguvu kwa miaka ishirini.
4 Now Deborah, a prophetess (the wife of Lappidoth), was a leading judge in Israel at that time.
Basi Debora, nabii wa kike (mke wa Lapidothi), alikuwa mwamuzi anayeongoza katika Israeli wakati huo.
5 She used to sit under the palm of Deborah between Ramah and Bethel in the hill country of Ephraim, and the people of Israel came to her to settle their disputes.
Naye aliketi chini ya mtende wa Debora kati ya Rama na Betheli katika nchi ya mlima wa Efraimu, na watu wa Israeli walimwendea ili kutatua migogoro yao.
6 She sent for Barak son of Abinoam from Kedesh in Naphtali. She said to him, “Yahweh, the God of Israel, commands you, 'Go to Mount Tabor, and take with you ten thousand men from Naphtali and Zebulun.
Akamtuma Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali. Akamwambia, Bwana, Mungu wa Israeli, anakuamuru, Nenda katika mlima wa Tabori, uende pamoja nawe watu elfu kumi kutoka Naftali na Zabuloni.
7 I will draw out Sisera, the commander of Jabin's army, to meet you by the Kishon River, with his chariots and his army, and I will give you victory over him.'”
Nitamfukuza Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, akutane nawe karibu na mto Kishoni, pamoja na magari yake na jeshi lake, na nitakupa ushindi juu yake. '
8 Barak said to her, “If you go with me, I will go, but if you do not go with me, I will not go.”
Baraka akamwambia, 'Ikiwa utakwenda nami, nitakwenda, lakini ikiwa huendi pamoja nami, sitaenda.'
9 She said, “I will certainly go with you. However, the road on which you are going will not lead to your honor, for Yahweh will sell Sisera into the hand of a woman.” Then Deborah got up and went with Barak to Kedesh.
Alisema, 'Nitakwenda nawe. Hata hivyo, njia unayoienda haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamuuza Sisera mkononi mwa mwanamke. Ndipo Debora akainuka, akaenda pamoja na Baraka Kedeshi.
10 Barak called for the men of Zebulun and Naphtali to come together at Kedesh. Ten thousand men followed him, and Deborah went along with him.
Baraki akawaita wana wa Zebuloni na Naftali kusanyika Kedeshi. Watu elfu kumi walimfuata, na Debora akaenda pamoja naye.
11 Now Heber (the Kenite) had separated himself from the Kenites—they were the descendants of Hobab (Moses' father-in-law)—and he pitched his tent by the oak in Zaanannim near Kedesh.
Heberi (Mkeni) alijitenganisha na Wakeni - walikuwa wazao wa Hobabu (mkwe wa Musa) - na akaweka hema yake mwaloni uliopo huko Saanaimu karibu na Kedesh.
12 When they told Sisera that Barak son of Abinoam had gone up to Mount Tabor,
Walipomwambia Sisera kwamba Baraka, mwana wa Abinoamu, alikuwa amekwenda mlima wa Tabori,
13 Sisera called out all his chariots, nine hundred iron chariots, and all the soldiers who were with him, from Harosheth Haggoyim to the Kishon River.
Sisera akawaita magari yake yote, magari ya farasi mia tisa, na askari wote waliokuwa pamoja naye, kutoka Haroshethi ya Mataifa mpaka Mto Kishoni.
14 Deborah said to Barak, “Go! For this is the day in which Yahweh has given you victory over Sisera. Is not Yahweh leading you?” So Barak went down from Mount Tabor with ten thousand men following him.
Debora akamwambia Baraka, Nenda! Kwa maana hii ndiyo siku ambayo Bwana amekupa ushindi juu ya Sisera. Je! si Bwana anayekuongoza? Basi Baraka akashuka kutoka mlima wa Tabori na watu kumi elfu wakamfuata.
15 Yahweh confused Sisera and all his chariots and all his army with the edge of the sword. And Sisera got down from his chariot and ran away on foot.
Bwana alifanya jeshi la Sisera kuchanganyikiwa, magari yake yote, na jeshi lake lote. Watu wa Baraka waliwashinda na Sisera akaanguka kutoka kwenye gari lake na kukimbia kwa miguu.
16 But Barak pursued the chariots and the army to Harosheth Haggoyim, and the whole army of Sisera was killed by the edge of the sword, and not a man survived.
Lakini Baraka akayafuata magari na jeshi mpaka Haroshethi ya Mataifa, na jeshi lote la Sisera likauawa kwa upanga, wala hakuna mtu aliyeokoka.
17 But Sisera ran away on foot to the tent of Jael, the wife of Heber the Kenite, for there was peace between Jabin the king of Hazor and the family of Heber the Kenite.
Lakini Sisera akakimbia kwa miguu mpaka hema ya Yaeli, mkewe Heberi Mkeni; kwa sababu kulikuwa na amani kati ya Yabini mfalme wa Hazori, na nyumba ya Heberi Mkeni.
18 Jael went out to meet Sisera and said to him, “Turn aside, my master; turn aside to me and do not be afraid.” So he turned aside to her and came into her tent, and she covered him with a blanket.
Jaeli akatoka kumlaki Sisera, akamwambia, karibu, bwana wangu; karibu kwangu, wala usiogope. Basi akakaribia kwake, akaingia hemani kwake, naye akamvika bushuti.
19 He said to her, “Please give me a little water to drink, for I am thirsty.” She opened a leather bag of milk and gave him drink, and then she covered him up again.
Akamwambia, Tafadhali nipe maji kidogo ninywe, kwa maana nina kiu. Alifungua mfuko wa ngozi ya maziwa akampa anywe, kisha akamfunika tena.
20 He said to her, “Stand at the opening of the tent. If someone comes and asks you, 'Is anyone here?', say 'No'.”
Akamwambia, “Simama mlangoni pa hema. Ikiwa mtu atakuja na kukuuliza, 'Je, kuna mtu hapa?', Sema 'Hapana'.”
21 Then Jael (the wife of Heber) took a tent peg and a hammer in her hand and went in secretly to him, for he was in a deep sleep, and she hammered the tent peg into the side of his head until it went down into the ground, and he died.
Kisha Jaeli (mke wa Heberi) akachukua kigingi cha hema na nyundo mkononi mwake akamwendea kwa siri, kwa sababu alikuwa amelala usingizi mzito, naye akakitia kigingi cha hema upande wa kichwa chake akamchoma na kikapenya kushuka chini. Hivyo akafa.
22 As Barak was pursuing Sisera, Jael want out to meet him and said to him, “Come, I will show you the man you are looking for.” So he went in with her, and there lay Sisera dead, with the tent peg in the side of his head.
Baraka alipokuwa akimfuata Sisera, Jaeli alitoka kukutana naye akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Basi akaingia pamoja naye, tazama Sisera amekufa, na kigingi cha hema kando ya kichwa chake.
23 So on that day God defeated Jabin, the king of Canaan, before the people of Israel.
Basi siku hiyo Mungu alimshinda Jabin, mfalme wa Kanaani, mbele ya watu wa Israeli.
24 The might of the people of Israel grew stronger and stronger against Jabin the king of Canaan, until they destroyed him.
Uwezo wa watu wa Israeli ulikua na nguvu zaidi dhidi ya Jabin mfalme wa Kanaani, hata walipomwangamiza.

< Judges 4 >