< Judges 16 >

1 Samson went to Gaza and saw a prostitute there, and he went to bed with her.
Siku moja Samsoni alienda Gaza, akamwona mwanamke kahaba, naye akaingia kwake.
2 The Gazites were told, “Samson has come here.” The Gazites surrounded the place and in secret, they waited for him all night at the city gate. They kept silent all night. They had said, “Let us wait until daylight, and then let us kill him.”
Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja huku!” Hivyo wakapazingira mahali pale nao wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji. Wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, “Tumvizie hadi mapambazuko, ndipo tutamuua.”
3 Samson lay in bed until midnight. At midnight he got up and he took hold of the city gate and its two posts. He pulled them up out of the ground, bar and all, put them on his shoulders, and carried them up to the top of the hill, in front of Hebron.
Samsoni akalala mpaka usiku wa manane. Akaondoka katikati ya usiku, akashika milango ya lango la mji pamoja na miimo yake miwili, akaingʼoa, makomeo yake na vyote. Akaviweka mabegani mwake na kuvipeleka mpaka kwenye kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.
4 After this, Samson came to love a woman who lived in the Valley of Sorek. Her name was Delilah.
Baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika Bonde la Soreki aliyeitwa Delila.
5 The rulers of the Philistines came up to her, and said to her, “Trick Samson to see where his great strength lies, and by what means we may overpower him, that we may bind him in order to humiliate him. Do this, and each one of us will give you 1,100 pieces of silver.”
Viongozi wa Wafilisti wakamwendea yule mwanamke na kumwambia, “Umbembeleze ili upate kujua siri za nguvu zake zilizo nyingi na jinsi tutakavyoweza kumshinda ili tuweze kumfunga na kumtiisha. Nasi kila mmoja wetu tutakupa shekeli 1,100 za fedha.”
6 Then Delilah said to Samson, “Please, tell me how is it that you are so strong, and how could anyone bind you, so you might be controlled?”
Hivyo Delila akamwambia Samsoni, “Naomba niambie siri ya hizi nguvu zako nyingi na jinsi utakavyoweza kufungwa ili kukutiisha.”
7 Samson said to her, “If they tie me with seven fresh bowstrings that have not been dried, then I will become weak and be like any other man.”
Samsoni akamjibu, “Kama wakinifunga kwa kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakapokuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
8 Then the rulers of the Philistines brought up to Delilah seven fresh bowstrings that had not been dried, and she tied Samson up with them.
Viongozi wa Wafilisti wakamletea yule mwanamke kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, akamfunga nazo Samsoni.
9 Now she had men hiding in secret, staying in her inner room. She said to him, “The Philistines are upon you, Samson!” But he broke the bowstrings like a thread of yarn when it touches the fire. So the secret of his strength was not discovered.
Wakati watu wakiwa wanamvizia katika chumba cha ndani, yule mwanamke akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini yeye akazikata zile kamba za upinde, kama vile uzi wa pamba unapoguswa na moto. Hivyo siri ya nguvu zake haikujulikana.
10 Then Delilah said to Samson, “This is how you have deceived me and told me lies. Please, tell me how you can be overpowered.”
Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Tafadhali niambie waweza kufungwa kwa kitu gani?”
11 He said to her, “If they tie me up with new ropes which have never been used for work, I will become weak and like any other man.”
Akamwambia, “Wakinifunga kwa uthabiti kwa kamba mpya ambazo hazijatumika, basi nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
12 So Delilah took new ropes and tied him up with them, and said to him, “The Philistines are upon you, Samson!” The men lying in wait were in the inner room. But Samson tore off the ropes from his arms like they were a piece of thread.
Hivyo Delila akachukua kamba mpya na kumfunga nazo. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Wale watu waliokuwa wanamvizia walikuwa katika chumba cha ndani. Lakini akazikata zile kamba zilizokuwa zimefunga mikono yake kama akatavyo uzi.
13 Delilah said to Samson, “Until now you have deceived me and told me lies. Tell me how you may be overpowered.” Samson said to her, “If you weave seven locks of my hair into a fabric on a loom, and then nail that to the loom, I will be like any other man.”
Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa, umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Nieleze ni jinsi gani utakavyoweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, “Kama ukivisuka hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo na kukaza kwa msumari, ndipo nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.” Hivyo Samsoni alipokuwa amelala, Delila akachukua vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake na kuvifunga kwenye mtande wa nguo,
14 While he slept, Delilah wove seven locks of his hair into the fabric on the loom and nailed it to the loom, and she said to him, “The Philistines are upon you, Samson!” He woke from his sleep and he pulled out the fabric and the pin from the loom.
na kuvikaza kwa msumari. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini akaamka kutoka usingizini na kuungʼoa ule msumari na ule mtande.
15 She said to him, “How can you say, 'I love you,' when you do not share your secrets with me? You have mocked me these three times and have not told me how you have such great strength.”
Ndipo Delila akamwambia, “Wawezaje kusema, ‘Nakupenda,’ wakati moyo wako haupo pamoja nami? Umenifanyia mzaha mara hizi tatu na hujaniambia siri ya hizi nguvu zako nyingi.”
16 Every day she pressed him hard with her words, and she pressured him so much that he wished he would die.
Hatimaye, baada ya kuwa anamsumbua kwa maneno siku kwa siku na kumuudhi, roho yake ikataabika hata kufa.
17 So Samson told her everything and said to her, “I have never had a razor cut the hair on my head, for I have been a Nazirite for God from my mother's womb. If my head is shaved, then my strength will leave me, and I will become weak and be like every other man.”
Hivyo akamwambia yule mwanamke siri yake yote, akamwambia, “Wembe haujapita kamwe kichwani mwangu, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu. Kama nywele za kichwa changu zikinyolewa, nguvu zangu zitanitoka, na nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote!”
18 When Delilah saw that he had told her the truth about everything, she sent and called for the rulers of the Philistines, saying, “Come up again, for he has told me everything.” Then the rulers of the Philistines went up to her, bringing the silver in their hands.
Delila alipoona kuwa amemweleza siri yake yote, akatuma ujumbe kwa viongozi wa Wafilisti na kusema, “Njooni tena mara nyingine, maana amenieleza siri yake yote.” Basi viongozi wa Wafilisti wakaja kwa Delila, wakiwa na fedha mikononi mwao.
19 She had him fall asleep in her lap. She called for a man to shave off the seven locks of his head, and she began to subdue him, for his strength had left him.
Delila akamfanya alale usingizi magotini pake, akamwita mtu akamnyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake. Akaanza kumsumbua ili aamke nazo nguvu zake zikamtoka.
20 She said, “The Philistines are upon you, Samson!” He woke up out of his sleep and said, “I will get out like the other times and shake myself free.” But he did not know that Yahweh had left him.
Yule mwanamke akamwita, “Samsoni, hao Wafilisti wanakujia!” Akaamka toka usingizini akasema, “Nitatoka nje kama hapo awali, nitawakungʼutia mbali na kuwa huru.” Lakini hakujua kuwa Bwana amemwacha.
21 The Philistines captured him and put out his eyes. They brought him down to Gaza and bound him with bronze shackles. He turned the millstone at the prison house.
Basi Wafilisti wakamkamata, wakamngʼoa macho yake, wakamchukua wakamteremsha mpaka Gaza. Wakiwa wamemfunga kwa pingu za shaba, wakamweka ili asage ngano huko gerezani.
22 But the hair on his head began to grow again after it had been shaved.
Wakati huo nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa.
23 The rulers of the Philistines gathered together to offer a great sacrifice to Dagon their god, and to rejoice. They said, “Our god has conquered Samson, our enemy, and put him in our grasp.”
Basi viongozi wa Wafilisti wakakusanyika pamoja ili kutoa kafara kwa mungu wao Dagoni na kufanya karamu, wakisema, “Mungu wetu amemtia adui yetu Samsoni mikononi mwetu.”
24 When the people saw him, they praised their god, for they said, “Our god has conquered our enemy and given him to us—the destroyer of our country, who killed many of us.”
Watu walipomwona Samsoni wakamsifu mungu wao, wakisema: “Sasa mungu wetu amemtia adui yetu mikononi mwetu, yule aliyeharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.”
25 When they were celebrating, they said, “Call for Samson, that he may make us laugh.” They called for Samson out of the prison and he made them laugh. They made him stand between the pillars.
Mioyo yao ilipokuwa imefurahishwa wakasema, “Mleteni Samsoni aje acheze ili tufurahi.” Basi wakamleta Samsoni kutoka mle gerezani naye akacheza mbele yao. Wakamweka kati ya nguzo mbili.
26 Samson said to the boy who held his hand, “Permit me to touch the pillars on which the building rests, so that I can lean against them.”
Samsoni akamwambia mtumishi aliyeshika mkono wake, “Niweke mahali ambapo ninaweza kuzigusa nguzo ambazo zinategemeza jengo ili nipate kuziegemea.”
27 Now the house was full of men and women. All the rulers of the Philistines were there. There were on the roof about three thousand men and women, who were looking on while Samson was entertaining them.
Basi lile jengo lilikuwa na wingi wa watu waume kwa wake; viongozi wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na kwenye sakafu ya juu walikuwepo watu 3,000 waume kwa wake, waliokuwa wakimtazama Samsoni wakati anacheza.
28 Samson called to Yahweh and said, “Lord Yahweh, call me to mind! Please strengthen me only this once, God, so that I may have revenge in one blow on the Philistines for taking my two eyes.”
Ndipo Samsoni akamwomba Bwana, akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, unikumbuke. Ee Mungu, nakusihi ukanitie nguvu mara hii moja tena, ili kwa tendo hili nipate kulipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.”
29 Samson held on to the two middle pillars on which the building rested, and he leaned against them, one pillar with his right hand, and the other with his left.
Ndipo Samsoni akazikaribia zile nguzo mbili za katikati ambazo lile jengo lilikuwa linazitegemea. Akazishika moja kwa mkono wa kuume na nyingine mkono wa kushoto.
30 Samson said, “Let me die with the Philistines!” He stretched out with his strength and the building fell on the rulers and on all the people who were in it. So the dead that he killed when he died were more than those he killed during his life.
Samsoni akasema, “Nife pamoja na Wafilisti!” Ndipo akazisukuma zile nguzo kwa nguvu zake zote, lile jengo likaanguka juu ya viongozi na watu wote waliokuwamo mle ndani yake. Hivyo akawaua watu wengi wakati wa kufa kwake kuliko siku za uhai wake.
31 Then his brothers and all the house of his father came down. They took him, brought him back and buried him between Zorah and Eshtaol in the burial place of Manoah, his father. Samson had judged Israel for twenty years.
Basi ndugu zake na jamaa yote ya baba yake wakateremka kwenda kumchukua. Wakampandisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli kwenye kaburi la Manoa baba yake. Naye Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.

< Judges 16 >