< Judges 12 >

1 A call went out to the men of Ephraim; they passed through Zaphon and said to Jephthah, “Why did you pass through to fight against the people of Ammon and did not call us to go with you? We will burn your house down over you.”
Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”
2 Jephthah said to them, “I and my people were in a great conflict with the people of Ammon. When I called you, you did not rescue me from them.
Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao.
3 When I saw that you did not rescue me, When I saw that you did not rescue me, I put my life in my own hand and passed through against the people of Ammon, and Yahweh gave me victory. Why have you come to fight against me today?”
Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”
4 Jephthah gathered together all the men of Gilead and he fought against Ephraim. The men of Gilead attacked the men of Ephraim because they said, “You Gileadites are fugitives in Ephraim—in Ephraim and Manasseh.”
Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.”
5 The Gileadites captured the fords of the Jordan leading to Ephraim. When any of the survivors of Ephraim said, “Let me go over the river,” the men of Gilead would say to him, “Are you an Ephraimite?” If he said, “No,”
Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,”
6 then they would say to him, “Say: Shibboleth,” and if he said “Sibboleth” (for he could not pronounce the word correctly), the Gileadites would seize him and kill him at the fords of the Jordan. Forty-two thousand Ephraimites were killed at that time.
walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.
7 Jephthah served as a judge over Israel for six years. Then Jephthah the Gileadite died and was buried in one of the cities of Gilead.
Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.
8 After him, Ibzan of Bethlehem served as a judge over Israel.
Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
9 He had thirty sons. He gave away thirty daughters in marriage, and he brought in thirty daughters of other men for his sons, from the outside. He judged Israel for seven years.
Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
10 Ibzan died and was buried at Bethlehem.
Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
11 After him Elon the Zebulunite served as judge over Israel. He judged Israel for ten years.
Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
12 Elon the Zebulunite died and was buried in Aijalon in the land of Zebulun.
Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
13 After him, Abdon son of Hillel the Pirathonite served as a judge over Israel.
Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
14 He had forty sons and thirty grandsons. They rode on seventy donkeys, and he judged Israel for eight years.
Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
15 Abdon son of Hillel the Pirathonite died and was buried in Pirathon in the land of Ephraim in the hill country of the Amalekites.
Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.

< Judges 12 >