< Joshua 21 >

1 Then the tribal leaders of the Levites came to Eleazar the priest, to Joshua son of Nun, and to the leaders of the families of their ancestors within the people of Israel.
Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli
2 They said to them at Shiloh in the land of Canaan, “Yahweh commanded you by the hand of Moses to give to us cities to live in, with the pasturelands for our livestock.”
huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwana aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”
3 So by the command of Yahweh, the people of Israel gave out of their inheritance the following cities, including their pasturelands, to the Levites.
Hivyo kama vile Bwana alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.
4 The casting of lots for the clans of the Kohathites gave this result: The priests—the descendants of Aaron who were from the Levites—received thirteen cities given from the tribe of Judah, from the tribe of the Simeon, and from the tribe of Benjamin.
Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.
5 The rest of the Kohathites were allotted ten cities from the clans of the tribes of Ephraim, Dan, and from the half tribe of Manasseh.
Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.
6 Then the people descended from Gershon were given, by the casting of lots, thirteen cities from the clans of the tribes of Issachar, Asher, Naphtali, and the half tribe of Manasseh in Bashan.
Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.
7 The people who were descendants of Merari, clan by clan, received twelve cities from the tribes of Reuben, Gad, and Zebulun.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
8 So the people of Israel gave, by casting lots, these cities (including their pasturelands) to the Levites, just as Yahweh had commanded by the hand of Moses.
Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.
9 From the tribes of Judah and Simeon, they assigned land to the following cities, here listed by name.
Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina
10 These cities were given to the descendants of Aaron, who were among the clans of the Kohathites, who in turn were from the tribe of Levi. For the first casting of lots had fallen to them.
(miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
11 The Israelites gave them Kiriath Arba (Arba had been the father of Anak), the same place as Hebron, in the hill country of Judah, with the pasturelands around it.
Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)
12 But the fields of the city, including their villages, were already given to Caleb son of Jephunneh, as his possession.
Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
13 To the descendants of Aaron the priest they gave Hebron with its pasturelands—which was a city of refuge for any who killed another unintentionally—and Libnah with its pasturelands,
Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,
14 Jattir with its pasturelands, and Eshtemoa with its pasturelands.
Yatiri, Eshtemoa,
15 They also gave Holon with its pasturelands, Debir with its pasturelands,
Holoni, Debiri,
16 Ain with its pasturelands, Juttah with its pasturelands, and Beth Shemesh with its pasturelands. There were nine cities that were given from these two tribes.
Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.
17 From the tribe of Benjamin were given Gibeon with its pasturelands, Geba with its pasturelands,
Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,
18 Anathoth with its pasturelands, and Almon with its suburbs—four cities.
Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
19 The cities given to the priests, the descendants of Aaron, were thirteen cities in all, including their pasturelands.
Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
20 As for the rest of Kohathites who belong to the Kohathite clans of the Levites—they had cities given to them from the tribe of Ephraim by the casting of lots.
Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:
21 To them were given Shechem with its pasturelands in the hill country of Ephraim—a city of refuge for any who killed a person unintentionally—Gezer with its pasturelands,
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,
22 Kibzaim with its pasturelands, and Beth Horon with its pasturelands—four cities in all.
Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
23 From the tribe of Dan, the clan of Kohath was given Eltekeh with its pasturelands, Gibbethon with its pasturelands,
Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,
24 Aijalon with its pasturelands, and Gath Rimmon with its pasturelands—four cities in all.
Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
25 From the half tribe of Manasseh, the clan of Kohath was given Taanach with its pasturelands and Gath Rimmon with its pasturelands—two cities.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.
26 There were ten cities in all for the rest of the clans of the Kohathites, including their pasturelands.
Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.
27 From the half tribe of Manasseh, to clans of Gershon, these were other Levite clans, and they gave Golan in Bashan with its pasturelands—a city of refuge for anyone who killed another unintentionally, along with Be Eshterah with its pasturelands—two cities in all.
Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
28 To the clans of Gershon they also gave Kishion from the tribe of Issachar, along with its pasturelands, Daberath with its pasturelands,
kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
29 Jarmuth with its pasturelands, and En Gannim with its pasturelands—four cities.
Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
30 From the tribe of Asher, they gave Mishal with its pasturelands, Abdon with its pasturelands,
kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
31 Helkath with its pasturelands, and Rehob with its pasturelands—four cities in all.
Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
32 From the tribe of Naphtali, they gave the clans of Gershon Kedesh in Galilee with its pasturelands—a city of refuge for anyone who killed another unintentionally; Hammoth Dor with its pasturelands, and Kartan with its pasturelands—three cities in all.
Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
33 There were thirteen cities in all, out of the clans of Gershon, including their pasturelands.
Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
34 To the rest of the Levites—the clans of Merari—were given out of the tribe of Zebulun: Jokneam with its pasturelands, Kartah with its pasturelands,
Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
35 Dimnah with its pasturelands, and Nahalal with its pasturelands—four cities in all.
Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
36 To the clans of Merari were given from the tribe of Reuben: Bezer with its pasturelands, Jahaz with its pasturelands,
kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
37 Kedemoth with its pasturelands, and Mephaath with its pasturelands—four cities.
Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
38 Out of the tribe of Gad they were given Ramoth in Gilead with its pasturelands—a city of refuge for any who killed another unintentionally—and Mahanaim with its pasturelands.
kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
39 The clans of Merari were also given Heshbon with its pasturelands, and Jazer with its pasturelands. These were four cities in all.
Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
40 All these were the cities of the several clans of Merari, who were from the tribe of Levi—twelve cities in all were given to them by the casting of lots.
Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
41 The cities of the Levites taken from the middle of the land possessed by the people of Israel were forty-eight cities, including their pasturelands.
Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.
42 These cities each had its surrounding pasturelands. It was this way with all these cities.
Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.
43 So Yahweh gave to Israel all the land that he swore to give to their ancestors. The Israelites took possession of it and settled there.
Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.
44 Then Yahweh gave them rest on every side, just as he had sworn to their ancestors. Not one of their enemies could defeat them. Yahweh gave all their enemies into their hand.
Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
45 Not one thing among all the good promises that Yahweh had spoken to the house of Israel failed to come true. All of them came to be.
Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.

< Joshua 21 >