< Joshua 11 >
1 When Jabin, king of Hazor, heard this, he sent a message to Jobab, king of Madon, to the king of Shimron, and to the king of Akshaph.
Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
2 He also sent the message to the kings who were in the northern hill country, in the Jordan River valley south of Kinnereth, in the lowlands, and in Naphoth Dor to the west.
na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
3 He also sent a message to the Canaanites to the east and west, the Amorites, the Hittites, the Perizzites, the Jebusites in the hill country, and the Hivites by Mount Hermon in the land of Mizpah.
kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
4 All their armies came out with them, a great number of soldiers, in number like the sand on the seashore. They had a great number of horses and chariots.
Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
5 All these kings met at the appointed time, and they camped at the waters of Merom to wage war with Israel.
Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
6 Yahweh said to Joshua, “Do not be afraid in their presence, because tomorrow at this time I am giving them all to Israel as dead men. You will hamstring their horses, and you will burn their chariots.”
Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
7 Joshua and all the men of war came. They arrived suddenly at the waters of Merom, and attacked the enemy.
Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
8 Yahweh gave the enemy into the hand of Israel, and they struck them and pursued them to Sidon, Misrephoth Maim, and to the Valley of Mizpah to the east. They struck them until not even one survivor of them was left.
naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
9 Joshua did to them just as Yahweh told him. He hamstrung the horses and burned the chariots.
Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
10 Joshua turned back at that time and captured Hazor. He struck its king with the sword. (Hazor had been head of all these kingdoms.)
Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
11 They struck with the sword every living creature that was there, and he set them apart to be destroyed, so there was not any living creature left alive. Then he burned Hazor.
Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
12 Joshua captured all the cities of these kings. He also captured all their kings and struck them with the edge of the sword. He completely destroyed them with the edge of the sword, just as Moses the servant of Yahweh had commanded.
Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
13 Israel did not burn any of the cities built on mounds, except Hazor. It alone Joshua burned.
Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
14 The army of Israel took all the plunder from these cities along with the livestock for themselves. They killed every human being with the edge of the sword until all were dead. They left alive no creature that breathed.
Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
15 Just as Yahweh had commanded his servant Moses, in the same way, Moses commanded Joshua, and so Joshua did it. He left nothing undone of all that Yahweh commanded Moses to do.
Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
16 Joshua took all that land, the hill country, all the Negev, all the land of Goshen, the foothills, the Jordan River valley, the hill country of Israel, and the lowlands.
Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
17 From Mount Halak near Edom, and going north as far as Baal Gad in the valley near Lebanon below Mount Hermon, he captured all their kings and killed them.
kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
18 Joshua waged war for a long time with all the kings.
Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
19 Not one city made peace with the army of Israel except the Hivites who lived in Gibeon. Israel captured all the rest of the cities in battle.
Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
20 For it was Yahweh who hardened their hearts so they would wage war against Israel, so that he might completely destroy them without mercy, just as he had instructed Moses.
Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
21 Then Joshua came at that time and he destroyed the Anakim. He did this in the hill country, at Hebron, Debir, Anab, and in all the hill country of Judah, and in all the hill country of Israel. Joshua completely destroyed them and their cities.
Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
22 None of the Anakim were left in the land of Israel except at Gaza, Gath, and Ashdod.
Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
23 So Joshua captured the whole land, just as Yahweh said to Moses. Joshua gave it as an inheritance to Israel, assigned to each of their tribes. Then the land had rest from the wars.
Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.