< Jonah 2 >
1 Then Jonah prayed to Yahweh his God from the fish's stomach.
Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
2 He said, “I called out to Yahweh about my distress and he answered me; from the belly of Sheol I cried out for help! You heard my voice. (Sheol )
Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol )
3 You had thrown me into the depths, into the heart of the seas, and the currents surrounded me; all your waves and billows passed over me.
Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
4 I said, 'I am driven out from before your eyes; yet I will again look toward your holy temple.'
Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
5 The waters closed around me up to my neck; the deep was all around me; seaweed wrapped around my head.
Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
6 I went down to the bases of the mountains; the earth with its bars closed upon me forever. Yet you brought up my life from the pit, Yahweh, my God!
Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
7 When my soul fainted within me, I called Yahweh to mind; then my prayer came to you, to your holy temple.
“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
8 They give attention to useless gods while they forsake loving faithfulness.
“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
9 But as for me, I will sacrifice to you with a voice of thanksgiving; I will fulfill that which I have vowed. Salvation comes from Yahweh!”
Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
10 Then Yahweh spoke to the fish, and it vomited up Jonah upon the dry land.
Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.