< Job 6 >
1 Then Job answered and said,
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 “Oh, if only my anguish were weighed; if only all my calamity were laid in the balance!
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
3 For now it would be heavier than the sand of the seas. That is why my words were reckless.
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arrows of the Almighty are in me, my spirit drinks up the poison; the terrors of God have arranged themselves in array against me.
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
5 Does the wild donkey bray in despair when he has grass? Or does the ox low in hunger when it has fodder?
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
6 Can that which has no taste be eaten without salt? Or is there any taste in the white of an egg?
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
7 I refuse to touch them; they are like disgusting food to me.
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
8 Oh, that I might have my request; oh, that God would grant me the thing I long for:
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
9 that it would please God to crush me once, that he would let loose his hand and cut me off from this life!
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
10 May this still be my consolation— even if I exult in pain that does not lessen: that I have not denied the words of the Holy One.
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11 What is my strength, that I should try to wait? What is my end, that I should prolong my life?
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
12 Is my strength the strength of stones? Or is my flesh made of bronze?
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
13 Is it not true that I have no help in myself, and that wisdom has been driven out of me?
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
14 To the person who is about to faint, faithfulness should be shown by his friend; even to him who forsakes the fear of the Almighty.
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
15 But my brothers have been as faithful to me as a desert streambed, as channels of water that pass away to nothing,
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
16 which are darkened because of ice over them, and because of the snow that hides itself in them.
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
17 When they thaw out, they vanish; when it is hot, they melt out of their place.
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
18 The caravans that travel by their way turn aside for water; they wander into barren land and then perish.
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
19 Caravans from Tema looked there, while companies of Sheba hoped in them.
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
20 They were disappointed because they had been confident of finding water. They went there, but they were deceived.
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
21 For now you friends are nothing to me; you see my dreadful situation and are afraid.
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
22 Did I say to you, 'Give something to me?' Or, 'Offer me a gift from your wealth?'
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
23 Or, 'Save me from my adversary's hand?' Or, 'Ransom me from the hand of my oppressors?'
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
24 Teach me, and I will hold my peace; make me understand where I have been wrong.
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
25 How painful are truthful words! But your arguments, how do they actually rebuke me?
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
26 Do you plan to ignore my words, treating the words of a desperate man like the wind?
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
27 Indeed, you cast lots for a fatherless child, and haggle over your friend like merchandise.
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
28 Now, therefore, please look at me, for surely I would not lie to your face.
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
29 Relent, I beg you; let there be no injustice with you; Indeed, relent, for my cause is just.
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
30 Is there evil on my tongue? Cannot my mouth detect malicious things?
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?