< Job 5 >

1 Call out now; is there anyone who will answer you? To which of the holy ones will you turn?
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 For anger kills the foolish man; jealousy kills the silly one.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 I have seen a foolish person taking root, but suddenly I cursed his home.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 His children are far from safety; they are crushed in the city gate. There is no one to rescue them.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 The hungry eat up their harvest; they even take it from among the thorns. The thirsty pant for their wealth.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 For difficulties do not come out from the soil; neither does trouble sprout from the ground.
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 Instead, mankind is born for trouble, just as sparks fly upward.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 But as for me, I would turn to God himself; to him I would commit my cause—
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 he who does great and unsearchable things, marvelous things without number.
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 He gives rain on the earth, and sends water on the fields.
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 He does this in order to set up on high those who are low; to raise to safety those who mourn.
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 He breaks the plans of the crafty people, so that their hands cannot achieve success.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 He traps wise people in their own crafty actions; the plans of twisted people are hurried to their end.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 They encounter darkness in the daytime, and grope at noonday as if it were night.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 But he saves the poor person from the sword in their mouths and the needy person from the hand of mighty people.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 So the poor person has hope, and injustice shuts her own mouth.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 See, blessed is the man whom God corrects; therefore, do not despise the chastening of the Almighty.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 For he wounds and then binds up; he wounds and then his hands heal.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 He will rescue you out of six troubles; indeed, in seven troubles, no evil will touch you.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 In famine he will ransom you from death, and in war from the hands of the sword.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 You will be hidden from the scourge of the tongue; and you will not be afraid of destruction when it comes.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 You will laugh at destruction and famine, and you will not be afraid of beasts of the earth.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 For you will have a covenant with the stones in your field, and the beasts of the field will be at peace with you.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 You will know that your tent is in safety; you will visit your sheepfold and you will not miss anything.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 You will also know that your seed will be great, that your offspring will be like the grass on the ground.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 You will come to your grave at a full age, like a stack of grain bundles that goes up at its time.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 See, we have examined this matter; it is like this; listen to it, and know it for yourself.”
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Job 5 >