< Job 40 >
1 Yahweh continued to speak to Job; he said,
Bwana akamwambia Ayubu:
2 “Should anyone who wishes to criticize try to correct the Almighty? He who argues with God, let him answer.”
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Then Job answered Yahweh and said,
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 “See, I am insignificant; how can I answer you? I put my hand over my mouth.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 I spoke once, and I will not answer; indeed, twice, but I will proceed no further.”
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Then Yahweh answered Job out of a fierce storm and said,
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 “Now gird up your loins like a man, for I will ask you questions, and you must answer me.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Will you actually say that I am unjust? Will you condemn me so you may claim you are right?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Do you have an arm like God's? Can you thunder with a voice like him?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Now clothe yourself in glory and dignity; array yourself in honor and majesty.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Scatter around the excess of your anger; look at everyone who is proud and bring him down.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Look at everyone who is proud and bring him low; trample down wicked people where they stand.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Bury them in the earth together; imprison their faces in the hidden place.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Then will I also acknowledge about you that your own right hand can save you.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Look now at the behemoth, which I made when I made you; he eats grass like an ox.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 See now, his strength is in his loins; his power is in his belly's muscles.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 He makes his tail like a cedar; the sinews of his thighs are joined together.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 His bones are like tubes of bronze; his legs are like bars of iron.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 He is the chief of the creatures of God. Only God, who made him, can defeat him.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 For the hills provide him with food; the beasts of the field play nearby.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 He lies under the lotus plants in the shelter of the reeds, in the marshes.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 The lotus plants cover him with their shade; the willows of the brook are all around him.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 See, if a river floods its banks, he does not tremble; he is confident, though the Jordan should surge up to his mouth.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Can anyone capture him with a hook, or pierce his nose through with a snare?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?