< Job 33 >

1 So now, Job, I beg you, hear my speech; listen to all my words.
Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
2 See now, I have opened my mouth; my tongue has spoken in my mouth.
Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
3 My words come from the uprightness of my heart; my lips speak pure knowledge.
Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
4 The Spirit of God has made me; the breath of the Almighty has given me life.
Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
5 If you can, answer me; set your words in order before me and stand up.
Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
6 See, I am just as you are in God's sight; I also have been formed out of the clay.
Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
7 See, terror of me will not make you afraid; neither will my pressure be heavy upon you.
Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
8 You have certainly spoken in my hearing; I have heard the sound of your words saying,
Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
9 'I am clean and without transgression; I am innocent, and there is no sin in me.
'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
10 See, God finds opportunities to attack me; he regards me as his enemy.
Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
11 He puts my feet in stocks; he watches all my paths.'
Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
12 See, in this you are not right—I will answer you, for God is greater than man.
Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
13 Why do you struggle against him? He does not account for any of his doings.
Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
14 For God speaks once— yes, twice, though man does not notice it.
Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
15 In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falls upon men, in slumber on the bed—
Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
16 then God opens the ears of men, and frightens them with threats,
basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
17 in order to pull man back from his sinful purposes, and keep pride from him.
kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
18 God keeps man's life back from the pit, his life from crossing over to death.
Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
19 Man is punished also with pain on his bed, with constant agony in his bones,
Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
20 so that his life abhors food, and his soul abhors delicacies.
ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
21 His flesh is consumed away so that it cannot be seen; his bones, once not seen, now stick out.
Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
22 Indeed, his soul draws close to the pit, his life to those who wish to destroy it.
Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
23 But if there is an angel who can be a mediator for him, a mediator, one from among the thousands of angels, to show him what is right to do,
Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
24 and if the angel is kind to him and says to God, 'Save this person from going down to the pit; I have found a ransom for him,'
na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
25 then his flesh will become fresher than a child's; he will return to the days of his youthful strength.
kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
26 He will pray to God, and God will be kind to him, so that he sees God's face with joy. God will give the person his triumph.
Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
27 Then that person will sing in front of other people and say, 'I sinned and perverted that which was right, but my sin was not punished.
Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
28 God has rescued my soul from going down into the pit; my life will continue to see light.'
Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
29 See, God does all these things with a person, twice, yes, even three times,
Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
30 to bring his soul back from the pit, so that he may be enlightened with the light of life.
kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
31 Pay attention, Job, and listen to me; be silent and I will speak.
Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
32 If you have anything to say, answer me; speak, for I wish to prove that you are in the right.
Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
33 If not, then listen to me; remain silent, and I will teach you wisdom.”
Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”

< Job 33 >