< Job 3 >

1 After this, Job opened his mouth and cursed the day he was born.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 He said,
Kisha akasema:
3 “May the day on which I was born perish, the night that said, 'A boy has been conceived.'
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 May that day be dark; may not God from above call it to mind, neither may the sun shine on it.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 May darkness and the shadow of death claim it for their own. May a cloud live over it; may everything that makes the day black truly terrify it.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 As for that night, may thick darkness seize it. May it not rejoice among the days of the year; may it not come into the number of the months.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 See, may that night be barren; may no joyful voice come into it.
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 May they curse that day, those who know how to wake up Leviathan.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 May the stars of that day's dawn be dark. May that day look for light, but find none; neither may it see the eyelids of the dawn,
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 because it did not shut up the doors of my mother's womb, and because it did not hide trouble from my eyes.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Why did I not die when I came out from the womb? Why did I not give up my spirit when my mother bore me?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Why did her knees welcome me? Why did her breasts receive me so that I should suck?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 For now I would have been lying down quietly. I would have slept and been at rest
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 with kings and counselors of the earth, who built up tombs for themselves that are now in ruins.
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 Or I would have been lying with princes who once had gold, who had filled their houses with silver.
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Or perhaps I would have been stillborn, like infants that never see the light.
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 There the wicked cease from trouble; there the weary are at rest.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 There the prisoners are at ease together; they do not hear the voice of the slave driver.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 Both small and great people are there; the servant is free from his master there.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Why is light given to him who is in misery? Why is life given to the one who is bitter in soul,
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 to one who longs for death without it coming; to one who digs for death more than for hidden treasure?
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Why is light given to one who rejoices very much and is glad when he finds the grave?
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 Why is light given to a man whose way is hidden, a man whom God has hedged in?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 For my sighing happens instead of eating; my groaning is poured out like water.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 For the thing that I feared has come on me; what I was afraid of has come to me.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 I am not at ease, I am not quiet, and I have no rest; trouble comes instead.”
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

< Job 3 >