< Jeremiah 6 >

1 Find safety, people of Benjamin, by leaving Jerusalem. Blow a trumpet in Tekoa. Raise up over Beth Hakkerem a signal, since wickedness is appearing from the north; a great crushing is coming.
“Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini, na uharibifu wa kutisha.
2 The daughter of Zion, the beautiful and delicate woman, will be destroyed.
Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mwororo.
3 The shepherds and their flocks will go to them; they will set up tents against her all around; each man will shepherd with his own hand.
Wachungaji pamoja na makundi yao watakuja dhidi yake; watapiga mahema yao kumzunguka, kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
4 “Dedicate yourselves to the gods for the battle. Arise, let us attack at noon. It is too bad that the daylight is fading away, that the evening shadows are falling.
“Jiandaeni kwa vita dhidi yake! Inukeni tumshambulie mchana! Lakini, ole wetu, mchana unaisha, na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
5 But let us attack at night and destroy her fortresses.”
Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku, na kuharibu ngome zake!”
6 For Yahweh of hosts says this: Cut her trees, and heap up siegeworks against Jerusalem. This is the right city to attack, because it is filled with oppression.
Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma kuzunguka Yerusalemu. Mji huu ni lazima uadhibiwe, umejazwa na uonevu.
7 As a well pours out fresh water, so this city keeps producing wickedness. Violence and disorder are heard within her; sickness and wounds are continually before my face.
Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake, ndivyo anavyomwaga uovu wake. Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake, ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.
8 Accept discipline, Jerusalem, or I will turn away from you and make you into a ruin, an uninhabited land.'”
Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”
9 Yahweh of hosts says this, “They will certainly glean those who are left in Israel like a vineyard. Reach out again with your hand to pick grapes from the vines.
Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli kwa uangalifu kama kwenye mzabibu; pitisha mkono wako kwenye matawi tena, kama yeye avunaye zabibu.”
10 To whom should I declare and warn so they will listen? Look! Their ears are uncircumcised; they are not able to pay attention! Look! The word of Yahweh has come to them to correct them, but they do not want it.”
Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la Bwana ni chukizo kwao, hawalifurahii.
11 But I am filled with Yahweh's fury. I am tired of holding it in. He said, to me, “Pour it out on the children in the streets and on the groups of young men. For every man will be taken away with his wife; and every old person heavy with years.
Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana, nami siwezi kuizuia. “Wamwagie watoto walioko barabarani, na juu ya vijana waume waliokusanyika; mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake, hata nao wazee waliolemewa na miaka.
12 Their houses will be turned over to others, both their fields and their wives together. For I will attack the inhabitants of the land with my hand—this is Yahweh's declaration.
Nyumba zao zitapewa watu wengine, pamoja na mashamba yao na wake zao, nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya wale waishio katika nchi,” asema Bwana.
13 Yahweh declares that from the least to the greatest, all of them are greedy for dishonest gain. From the prophet to the priest, all of them practice deceit.
“Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata faida zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
14 They have healed the wounds of my people lightly, saying, 'Peace, Peace,' when there is no peace.
Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, ‘Amani, amani,’ wakati hakuna amani.
15 Were they ashamed when they practiced abominations? They were not ashamed; they did not know how to blush! So they will fall among the fallen; they will be brought down when they are punished, says Yahweh.
Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo; hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini nitakapowaadhibu,” asema Bwana.
16 Yahweh says this, “Stand at the road crossing and look; ask for the ancient pathways. 'Where is this good way?' Then go on it and find a resting place for yourselves. But the people say, 'We will not go.'
Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Simama kwenye njia panda utazame, ulizia mapito ya zamani, ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’
17 I appointed for you watchmen to listen for the trumpet. But they said, 'We will not listen.'
Niliweka walinzi juu yenu na kusema, ‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’ Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’
18 Therefore, nations, listen! See, you witnesses, what will happen to them.
Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa, angalieni, enyi mashahidi, lile litakalowatokea.
19 Hear, earth! See, I am about to bring disaster to this people—the fruit of their thoughts. They paid no attention to my word or law, but they instead rejected it.”
Sikia, ee nchi: Ninaleta maafa juu ya watu hawa, matunda ya mipango yao, kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu na wameikataa sheria yangu.
20 “What does this frankincense going up from Sheba mean to me? Or these sweet smells from a distant land? Your burnt offerings are not acceptable to me, nor are your sacrifices.
Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba, au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali? Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki, dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”
21 So Yahweh says this, 'See, I am about to place a stumbling block against this people. They will stumble over it—fathers and sons together. Inhabitants and their neighbors will also perish.'
Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa. Baba na wana wao watajikwaa juu yake, majirani na marafiki wataangamia.”
22 Yahweh says this, 'See, a people is coming from the land of the north, a great nation is being stirred up from the farthest parts of the earth.
Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Tazama, jeshi linakuja kutoka nchi ya kaskazini, taifa kubwa linaamshwa kutoka miisho ya dunia.
23 They will pick up bows and spears. They are cruel and have no compassion. Their sound is like the sea roar, and they are riding on horses, set out in order as men for battle, against you, daughter of Zion.'”
Wamejifunga pinde na mkuki, ni wakatili na hawana huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao. Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”
24 We have heard the reports about them and our hands fall limp in distress. Anguish seizes us as a woman giving birth.
Tumesikia taarifa zao, nayo mikono yetu imelegea. Uchungu umetushika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
25 Do not go out to the fields, and do not walk on the roads, for the swords of the enemy and terror are all around.
Usitoke kwenda mashambani au kutembea barabarani, kwa kuwa adui ana upanga, na kuna vitisho kila upande.
26 Daughter of my people, put on sackcloth and roll in ashes; mourn with painful sobs as for an only son, for the destroyer will suddenly come upon us.
Enyi watu wangu, vaeni magunia mjivingirishe kwenye majivu, ombolezeni kwa kilio cha uchungu kama amliliaye mwana pekee, kwa maana ghafula mharabu atatujia.
27 “I have made you, Jeremiah, one who tests my people like one would test metal, so you will inspect and test their ways.
“Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma, nao watu wangu kama mawe yenye madini, ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.
28 They are all the most stubborn of people, who go about slandering others. All of them are bronze and iron, acting corruptly.
Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.
29 The bellows are scorched by the fire that is burning them; the lead is consumed in the flames. The refining continues among them, but it is useless, because the evil is not removed.
Mivuo inavuma kwa nguvu, kinachoungua kwa huo moto ni risasi, lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure; waovu hawaondolewi.
30 They will be called rejected silver, for Yahweh has rejected them.”
Wanaitwa fedha iliyokataliwa, kwa sababu Bwana amewakataa.”

< Jeremiah 6 >