< Jeremiah 50 >
1 This is the word that Yahweh declared about Babylon, the land of the Chaldeans, by the hand of Jeremiah the prophet,
Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
2 “Report to the nations and cause them to listen. Lift up a signal and cause them to listen. Do not conceal it. Say, 'Babylon is taken. Bel is made ashamed. Marduk is dismayed. Its idols are put to shame; its images are dismayed.'
“Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
3 A nation from the north will arise against it, and make her land a desolation. No one will live in it; both man and beast will flee away.
Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
4 In those days and at that time—this is Yahweh's declaration—the people of Israel and the people of Judah will come together to go with weeping and seek Yahweh their God.
“Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
5 They will ask the way to Zion and will set off toward it, saying, We will go and join ourselves to Yahweh in an everlasting covenant that will not be forgotten.”
Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
6 My people have been a lost flock. Their shepherds have led them astray in the mountains; they have turned them around from hill to hill. They went, they forgot the place where they had lived.
“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
7 Everyone who went out to them devoured them. Their adversaries said, 'We are not guilty, because they sinned against Yahweh, their true home—Yahweh, the hope of their ancestors.'
Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
8 Leave from the midst of Babylon; go out from the land of the Chaldeans; be like male goats that leave before the rest of the flock does.
“Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
9 For see, I am about to set in motion and raise up a group of great nations from the north against Babylon. They will arrange themselves against her. Babylon will be captured from there. Their arrows are like a skilled warrior who does not return empty-handed.
Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
10 Chaldea will become plunder. All those who plunder it will be satisfied—this is Yahweh's declaration.
Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
11 You rejoice, you celebrate the plundering of my inheritance; you jump around like a calf stamping in its pasture; you neigh like a powerful horse.
“Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
12 So your mother will be greatly ashamed; the one who bore you will be embarrassed. See, she will be the least of nations, a wilderness, a dry land, and a desert.
mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
13 Because of Yahweh's anger, Babylon will not be inhabited, but will be a complete devastation. Everyone who passes by will shudder because of Babylon and will hiss because all of its wounds.
Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
14 Arrange yourselves against Babylon all around her. Everyone who bends a bow must shoot at her. Do not keep back any of your arrows, for she has sinned against Yahweh.
“Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
15 Raise a shout against her all around! She has surrendered; her towers have fallen; her walls are torn down, for this is Yahweh's vengeance. Take vengeance on her! Do to her just as she has done!
Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
16 Destroy both the farmer who sows seed and the one who uses a sickle at the time of harvest in Babylon. Let each person turn back to his own people from the oppressor's sword; let them flee to their own land.
Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
17 Israel is a sheep scattered and driven away by lions. First the king of Assyria devoured him; then after this, Nebuchadnezzar king of Babylon broke his bones.
“Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
18 Therefore Yahweh of hosts, the God of Israel, says this: See, I am about to punish the king of Babylon and his land, just as I punished the king of Assyria.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
19 I will restore Israel to his homeland; he will graze on Carmel and Bashan. Then he will be satisfied in the hill country of Ephraim and Gilead.
Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
20 In those days and at that time, says Yahweh, iniquity will be looked for in Israel, but none will be found. I will inquire about the sins of Judah, but none will be found, for I will forgive the remnant that I spare.”
Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
21 “Arise against the land of Merathaim, against it and the ones inhabiting Pekod. Put them to the sword and set them apart for destruction—this is Yahweh's declaration—do everything that I am commanding you.
“Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
22 The sounds of battle and enormous destruction are in the land.
Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
23 How the hammer of all the lands has been cut apart and destroyed. How Babylon has become a destroyed place among the nations.
Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
24 I have set a trap for you and you were taken, Babylon, and you did not know it! You were found and captured, because you opposed Yahweh.
Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
25 Yahweh has opened his armory and is bringing out the weapons for carrying out his anger. There is work for the Lord Yahweh of hosts in the land of the Chaldeans.
Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
26 Attack her from far away. Open her granaries and pile her up like heaps of grain. Set her apart for destruction. Leave no remnant of her.
Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
27 Kill all her bulls. Send them down to the place of slaughter. Woe to them, for their day has come—the time for their punishment.
Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
28 There is the sound of those fleeing, of those who are survivors, from the land of Babylon. These will report the vengeance of Yahweh our God for Zion, and vengeance for his temple.”
Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
29 “Summon the archers against Babylon—all those who bend their bows. Camp against her, and let no one escape. Repay her for what she has done. Do to her by the measure she has used. For she had defied Yahweh, the Holy One of Israel.
“Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
30 So her young men will fall in the city squares, and all her fighting men will be destroyed on that day —this is Yahweh's declaration.”
Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
31 “See, I am against you, proud one—this is the declaration of the Lord Yahweh of hosts— for your day has come, proud one, the time when I will punish you.
“Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
32 So the proud ones will stumble and fall. No one will raise them up. I will light a fire in their cities; it will devour everything around him.
Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
33 Yahweh of hosts says this: The people of Israel are oppressed, together with the people of Judah. All the ones who captured them still hold them; they refuse to let them go.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
34 The one who rescues them is strong. Yahweh of hosts is his name. He will truly plead their case, in order to bring rest to the land, and to bring strife to the ones inhabiting Babylon.
Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
35 A sword is against the Chaldeans—this is Yahweh's declaration— and against the inhabitants of Babylon, her leaders, and her wise men.
“Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
36 A sword against those who say empty words! They will become fools! A sword against her soldiers! They will be filled with terror.
Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
37 A sword is coming against their horses, their chariots and all of the people who are in the midst of Babylon, so they will become like women. A sword is coming against her storerooms, and they will be plundered.
Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
38 A drought is coming on her waters, so they will become dry. For she is a land of worthless idols, and they act like people made insane by their dreadful idols.
Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
39 So desert beasts with the jackals will inhabit there, and the young of ostriches will live in her. For all time, she will no longer be inhabited. From generation to generation, she will not be lived in.
“Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
40 Just as God overthrew Sodom and Gomorrah and their neighbors—this is Yahweh's declaration— no one will live there; no person will stay in her.”
Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
41 “See, a people is coming from the north; a great nation and many kings are being stirred up from the farthest parts of the earth.
“Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
42 They will pick up bows and spears. They are cruel and have no compassion. Their sound is like the sea roar, and they are riding on horses, set out in order as men for battle, against you, daughter of Babylon.
Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
43 The king of Babylon heard the reports about them and his hands fell limp in distress. Anguish seized him like a woman giving birth.
Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
44 Behold! He goes up like a lion from the heights of the Jordan to the enduring grazing place For I will quickly cause them to run from it, and I will put someone who will be chosen in charge of it. For who is like me, and who will summon me? What shepherd is able to resist me?
Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
45 So listen to the plans that Yahweh has decided against Babylon, the plans that he has planned against the land of the Chaldeans. They will certainly be dragged away, even the smallest flock. Their pasturelands will be turned into ruined places.
Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
46 At the sound of conquered Babylon the earth shakes, and their shout of distress is heard among the nations.”
Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.