< Jeremiah 34 >
1 The word that came to Jeremiah from Yahweh, when Nebuchadnezzar king of Babylon and all of his army, together with all the kingdoms of the earth, the domains under his power, and all their people were waging war against Jerusalem and all of her cities, saying:
Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 “Yahweh, God of Israel, says this: Go and speak to Zedekiah king of Judah and say to him, 'Yahweh says this: Look, I am about to give this city into the hand of the king of Babylon. He will burn it.
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
3 You will not escape from his hand, for you will certainly be seized and given into his hand. Your eyes will look at the eyes of the king of Babylon; he will speak directly to you as you go to Babylon.'
Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
4 Listen to the word of Yahweh, Zedekiah king of Judah! Yahweh says this concerning you, 'You will not die by the sword.
“‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
5 You will die in peace. As in the funeral burning of your ancestors, the kings who were before you, they will burn your body. They will say, “Woe, master!” They will lament for you. Now I have spoken—this is Yahweh's declaration.'”
utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
6 So Jeremiah the prophet proclaimed to Zedekiah king of Judah all these words in Jerusalem.
Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
7 The army of the king of Babylon made war against Jerusalem and all the remaining cities of Judah: Lachish and Azekah. These cities of Judah remained as fortified cities.
wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
8 The word came to Jeremiah from Yahweh after King Zedekiah had made a covenant with all the people in Jerusalem, to proclaim freedom to them,
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
9 that each man must free his Hebrew slaves, both male and female, so one was to make a slave of a Jew, who was his brother.
Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
10 So all the leaders and people entered into the covenant that each person would free his male and female slaves so that they would not be enslaved any longer. They obeyed and set them free.
Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
11 But after this they changed their minds. They brought back the slaves whom they had freed. They forced them to become slaves again.
Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
12 So the word of Yahweh came to Jeremiah, saying,
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
13 “Yahweh, God of Israel, says this, 'I myself made a covenant with your ancestors on the day that I brought them out from the land of Egypt, out from the house of slavery. That was when I said,
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
14 “At the end of every seven years, each man must send away his brother, his fellow Hebrew who had sold himself to you and served you for six years. Send him away in freedom.” But your ancestors did not listen to me or incline their ears to me.
‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
15 Now you yourselves repented and began to do what is right in my eyes. You proclaimed freedom, each man to his neighbor, and you made a covenant before me in the house that is called by my name.
Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
16 But then you turned and polluted my name; you caused each man to bring back his male and female slaves, the ones whom you had sent out to go where they wished. You forced them to become your slaves again.'
Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
17 Therefore Yahweh says this, 'You yourselves have not listened to me. You should have proclaimed freedom, every one of you, to your brothers and fellow Israelites. So look! I am about to proclaim freedom to you—this is Yahweh's declaration—freedom for the sword, the plague, and famine, for I am going to make you a horrible thing in the sight of every kingdom on earth.
“Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
18 Then I will deal with the people who have broken my covenant, who did not keep the words of the covenant that they established before me when they cut a bull in two and walked between its parts,
Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
19 and then the leaders of Judah and Jerusalem, the eunuchs and the priests, and all the people of the land walked between the parts of the bull.
Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
20 I will give them into the hand of their enemies and into the hand of those who are seeking their lives. Their bodies will be food for the birds of the skies and the beasts on the earth.
nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
21 So I will give Zedekiah king of Judah and his leaders into the hand of their enemies and into the hand of those who are seeking their life, and into the hand of the army of the king of Babylon that has risen up against you.
“Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
22 Look, I am about to give a command—this is Yahweh's declaration—and will bring them back to this city to wage war against it and take it, and to burn it. For I will turn the cities of Judah into ruined places in which there will be no inhabitants.'”
Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”