< Jeremiah 30 >

1 The word that came to Jeremiah from Yahweh, saying,
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 “This is what Yahweh, God of Israel, says, 'Write in a scroll all the words that I have spoken to you.
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe.
3 For look, days are coming—this is Yahweh's declaration—when I will restore the fortunes of my people, Israel and Judah. I, Yahweh, have said it. For I will bring them back to the land that I gave their ancestors, and they will possess it.'”
Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni, na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asema Bwana.”
4 These are the words that Yahweh declared concerning Israel and Judah,
Haya ndiyo maneno Bwana aliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda:
5 “For Yahweh says this, 'We have heard a trembling voice of dread and not of peace.
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Vilio vya woga vinasikika: hofu kuu, wala si amani.
6 Ask and see if a man bears a child. Why do I see every young man with his hand on his loins like a woman bearing a child? Why have all their faces become pale?
Ulizeni na mkaone: Je, mwanaume aweza kuzaa watoto? Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu ameweka mikono yake tumboni kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa, kila uso ukigeuka rangi kabisa?
7 Woe! For that day will be great, with none like it. It will be a time of anxiety for Jacob, but he will be rescued from it.
Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha! Hakutakuwa na nyingine mfano wake. Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo, lakini ataokolewa kutoka hiyo.
8 For it will be in that day—this is the declaration of Yahweh of hosts—that I will break the yoke off your neck, and I will shatter your chains, so foreigners will no longer enslave you.
“‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao na kuvipasua vifungo vyao; wageni hawatawafanya tena watumwa.
9 But they will worship Yahweh their God and serve David their king, whom I will make king over them.
Badala yake, watamtumikia Bwana, Mungu wao na Daudi mfalme wao, nitakayemwinua kwa ajili yao.
10 So you, my servant Jacob, do not fear—this is Yahweh's declaration—and do not be dismayed, Israel. For see, I am about to bring you back from far away, and your descendants from the land of captivity. Jacob will return and be at peace; he will be secure, and there will be no more terror.
“‘Hivyo usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli,’ asema Bwana. ‘Hakika, nitakuokoa kutoka mbali, wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na usalama, wala hakuna atakayemtia hofu.
11 For I am with you—this is Yahweh's declaration—to save you. Then I will bring a complete end to all the nations where I have scattered you. But I will certainly not put an end to you, though I discipline you justly and will certainly not leave you unpunished.'
Mimi niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,’ asema Bwana. ‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambamo miongoni mwao nimewatawanya, sitawaangamiza ninyi kabisa. Nitawaadhibu, lakini kwa haki. Sitawaacha kabisa bila adhabu.’
12 For Yahweh says this, 'Your injury is incurable; your wound is infected.
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Kidonda chako hakina dawa, jeraha lako haliponyeki.
13 There is no one to plead your case; there is no remedy for your wound to heal you.
Hakuna yeyote wa kukutetea shauri lako, hakuna dawa ya kidonda chako, wewe hutapona.
14 All of your lovers have forgotten you. They will not look for you, for I have wounded you with the wound of an enemy and the discipline of a cruel master because of your many iniquities and your innumerable sins.
Wale walioungana nawe wote wamekusahau, hawajali chochote kukuhusu wewe. Nimekupiga kama vile adui angelifanya, na kukuadhibu kama vile mtu mkatili angelifanya, kwa sababu hatia yako ni kubwa mno na dhambi zako ni nyingi sana.
15 Why do you call for help for your injury? Your pain is incurable. Because of your many iniquities, your innumerable sins, I have done these things to you.
Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako, yale maumivu yako yasiyoponyeka? Kwa sababu ya uovu wako mkubwa na dhambi zako nyingi nimekufanyia mambo haya.
16 So everyone who consumes you will be consumed, and all of your adversaries will go into captivity. For the ones who have plundered you will become plunder, and I will make all of the ones despoiling you a spoil.
“‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa; adui zako wote watakwenda uhamishoni. Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara; wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.
17 For I will bring healing on you; I will heal you of your wounds—this is Yahweh's declaration— I will do this because they called you: Outcast. No one cares for this Zion.'”
Lakini nitakurudishia afya yako na kuyaponya majeraha yako,’ asema Bwana, ‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa, Sayuni ambaye hakuna yeyote anayekujali.’
18 Yahweh says this, “See, I am about to bring back the fortunes of Jacob's tents and have compassion on his homes. Then a city will be built on the heap of ruins, and a stronghold will exist again where it used to be.
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo, na kuhurumia maskani yake. Mji utajengwa tena juu ya magofu yake, nalo jumba la kifalme litasimama mahali pake halisi.
19 Then a song of praise and a sound of merriment will go out from them, for I will increase them and not diminish them; I will honor them so they will not be humbled.
Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao na sauti ya furaha. Nitaiongeza idadi yao wala hawatapungua, nitawapa heshima na hawatadharauliwa.
20 Then their people will be like before, and their assembly will be established before me when I punish all the ones who are now tormenting them.
Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa siku za zamani, nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu; nitawaadhibu wale wote wawaoneao.
21 Their leader will come from among them. He will emerge from their midst when I draw him near and when he approaches me. If I do not do this, who would dare come close to me?—this is Yahweh's declaration.
Mmoja wao atakuwa kiongozi wao; mtawala wao atainuka miongoni mwao. Nitamleta karibu nami, naye atanikaribia mimi, kwa maana ni nani yule atakayejitolea kuwa karibu nami?’ asema Bwana.
22 Then you will be my people, and I will be your God.
‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.’”
23 See, the tempest of Yahweh, his fury, has gone out. It is a continual tempest. It will whirl on the heads of the wicked people.
Tazama, tufani ya Bwana italipuka kwa ghadhabu, upepo wa kisulisuli uendao kasi utashuka juu ya vichwa vya waovu.
24 Yahweh's wrath will not return until it has carried out and brought into being his heart's intentions. In the final days, you will understand it.”
Hasira kali ya Bwana haitarudi nyuma mpaka atakapotimiza makusudi yote ya moyo wake. Siku zijazo mtayaelewa haya.

< Jeremiah 30 >