< Jeremiah 17 >
1 “The sin of Judah is written with an iron stylus having a diamond point. It is engraved on the tablet of their hearts and on the horns of your altars.
“Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma, imeandikwa kwa ncha ya almasi, kwenye vibao vya mioyo yao na kwenye pembe za madhabahu zao.
2 Even their children remember their altars and their Asherah poles that were beside the spreading trees and on the high hills.
Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao na nguzo za Ashera, kandokando ya miti iliyotanda na juu ya vilima virefu.
3 My mountain in the open country, and your wealth and all your treasures I will give away as plunder, together with your high places, because of the sin you committed in all your territories.
Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara, pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.
4 You will lose the inheritance that I gave to you. I will enslave you to your enemies in a land that you do not know, for you have ignited a fire in my wrath, which will burn forever.”
Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza urithi niliokupa. Nitakufanya mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa umeiwasha hasira yangu, nayo itawaka milele.”
5 Yahweh says, “The person who trusts in mankind is accursed; he makes flesh his strength but turns his heart away from Yahweh.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu, ategemeaye mwenye mwili kwa ajili ya nguvu zake, ambaye moyo wake umemwacha Bwana.
6 For he will be like a small bush in the Arabah and will not see anything good coming. He will stay in the stony places in the wilderness, barren land without inhabitants.
Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.
7 But the person who trusts in Yahweh is blessed, for Yahweh is his reason for confidence.
“Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana, ambaye matumaini yake ni katika Bwana.
8 For he will be like a tree planted by water, its roots will spread out by the stream. It will not fear the heat when it comes, for its leaves are always green. It is not anxious in a year of drought, and it will not stop producing fruit.
Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji. Hauogopi wakati wa joto ujapo; majani yake ni mabichi daima. Hauna hofu katika mwaka wa ukame na hautaacha kuzaa matunda.”
9 The heart is more deceitful than anything else. It is sick; who can understand it?
Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, ni mwovu kupita kiasi. Ni nani awezaye kuujua?
10 I am Yahweh, the one who searches through the mind, who tests the hearts. I give to each person according to his ways, according to the fruit of his deeds.
“Mimi Bwana huchunguza moyo na kuzijaribu nia, ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake, kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”
11 A partridge hatches an egg that she did not lay. Someone may become rich unjustly, but when half his days are over, those riches will abandon him, and in the end he will be a fool.”
Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga, ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki. Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha, na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.
12 “The place of our temple is a glorious throne, elevated from the beginning.
Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo, ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.
13 Yahweh is the hope of Israel. All who abandon you will be put to shame; those in the land who turn away from you will be written in the earth, for they have forsaken Yahweh, the fountain of living waters.
Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli, wote wakuachao wataaibika. Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini kwa sababu wamemwacha Bwana, chemchemi ya maji yaliyo hai.
14 Heal me, Yahweh, and I will be healed! Rescue me, and I will be rescued. For you are my song of praise.
Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe nami nitaokoka, kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.
15 See, they are saying to me, 'Where is the word of Yahweh? Let it come!'
Wao huendelea kuniambia, “Liko wapi neno la Bwana? Sasa na litimie!”
16 As for me, I did not run from being a shepherd following you. I did not long for the day of disaster. You know the proclamations that came from my lips. They were made in your presence.
Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako; unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa. Kile kipitacho midomoni mwangu ki wazi mbele yako.
17 Do not be a terror to me. You are my refuge on the day of calamity.
Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu; wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.
18 May my pursuers be ashamed, but do not let me be ashamed. May they be dismayed, but do not let me be dismayed. Send the day of disaster against them and shatter them with a double share of destruction.”
Watesi wangu na waaibishwe, lakini nilinde mimi nisiaibike; wao na watiwe hofu kuu, lakini unilinde mimi na hofu kuu. Waletee siku ya maafa; waangamize kwa maangamizi maradufu.
19 Yahweh said this to me: “Go and stand in the gate of the people where the kings of Judah enter and where they exit, then in all the other gates of Jerusalem.
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu.
20 Say to them, 'Hear the word of Yahweh, kings of Judah and all you people of Judah, and every resident of Jerusalem who comes in through these gates.
Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya.
21 Yahweh says this: “Be careful for the sake of your lives and do not carry a burden on the Sabbath day to bring it to the gates of Jerusalem.
Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu.
22 Do not bring a load out from your house on the Sabbath day. Do not do any work, but set apart the Sabbath day, just as I commanded your ancestors to do.”'
Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu.
23 They did not listen or pay attention, but stiffened their neck so they would not hear me nor accept discipline.
Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu.
24 It will happen that if you truly listen to me—this is Yahweh's declaration—and do not bring a load to the gates of this city on the Sabbath day but instead set apart the Sabbath day to Yahweh and not do any work on it,
Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo,
25 then kings, princes, and those who sit on David's throne will come to the gates of this city in chariots and with horses, they and their leaders, men of Judah and inhabitants of Jerusalem, and this city will be inhabited forever.
ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima.
26 They will come from the cities of Judah and from all around Jerusalem, from the land of Benjamin and the lowlands, from the mountains, and from the Negev, bringing burnt offerings and sacrifices, grain offerings and frankincense, thank offerings to the house of Yahweh.
Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana.
27 But if you do not listen to me—to set apart the Sabbath day and to not carry heavy loads and to not enter the gates of Jerusalem on the Sabbath day—then I will light a fire in its gates, and it will consume the fortresses of Jerusalem, and it cannot be put out.”
Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’”