< Isaiah 48 >
1 Hear this, house of Jacob, who are called by the name Israel, and have come from the sperm of Judah; you who swear by the name of Yahweh and invoke the God of Israel, but not sincerely nor in a righteous manner.
“Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
2 For they call themselves people of the holy city and trust in the God of Israel. Yahweh of hosts is his name.
ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
3 “I have declared the things from long ago; they came out from my mouth, and I made them known; then suddenly I did them, and they came to pass.
Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
4 Because I knew that you were obstinate, your neck muscles tight as iron, and your forehead like bronze,
Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
5 therefore I declared these things to you beforehand; before they happened I informed you, so you could not say, 'My idol has done them,' or 'My carved figure and my cast metal figure has ordained these things.'
Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
6 You heard about these things; look at all this evidence; and you, will you not admit what I said is true? From now on, I am showing you new things, hidden things that you have not known.
Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
7 Now, and not from previously, they come into being, and before today you have not heard about them, so you will not be able to say, 'Yes, I knew about them.'
Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
8 You never heard; you did not know; these things were not unfolded to your ears beforehand. For I knew that you have been very deceitful, and that you have been a rebel from birth.
Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
9 For the sake of my name I will defer my anger, and for my honor I will hold back from destroying you.
Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
10 Look, I refined you, but not as silver; I have purified you in the furnace of affliction.
Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
11 For my own sake, for my own sake I will act; for how can I allow my name to be profaned? I will not give my glory to anyone else.
Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
12 Listen to me, Jacob, and Israel, whom I called: I am he; I am the first, I also am the last.
“Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
13 Yes, my hand laid the foundation of the earth, and my right hand spread out the heavens; when I call to them, they stand up together.
Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
14 Assemble yourselves, all of you, and listen! Who among you has announced these things? Yahweh's ally will accomplish his purpose against Babylon. He will carry out Yahweh's will against the Chaldeans.
“Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
15 I, I have spoken, yes, I have summoned him, I have brought him, and he will succeed.
Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
16 Come near to me, listen to this: From the beginning I have not spoken in secret; when it happens, I am there.” Now the Lord Yahweh has sent me, and his Spirit.
“Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
17 This is what Yahweh, your Redeemer, the Holy One of Israel says, “I am Yahweh your God, who teaches you how to succeed, who leads you by the way that you should go.
Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
18 If only you had obeyed my commandments! Then your peace and prosperity would have flowed like a river, and your salvation like the waves of the sea.
Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
19 Your descendants would have been as numerous as the sand, and the children from your womb as numerous as the grains of sand; their name would not have been cut off nor blotted out from before me.
Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
20 Come out from Babylon! Flee from the Chaldeans! With the sound of a ringing cry announce it! Make this known, make it go out to the ends of the earth! Say, 'Yahweh has redeemed his servant Jacob.'
Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
21 They did not thirst when he led them through the deserts; he made the water to flow out of the rock for them; he split open the rock, and the waters gushed out.
Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
22 There is no peace for the wicked—says Yahweh.”
“Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.