< Isaiah 30 >

1 “Woe to the rebellious children,” this is Yahweh's declaration. “They make plans, but not from me; they make alliances with other nations, but they were not directed by my Spirit, so they add sin to sin.
Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
2 They set out to go down into Egypt, but have not asked for my direction. They seek protection from Pharaoh and take refuge in the shadow of Egypt.
wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
3 Therefore Pharaoh's protection will be your shame, and the refuge in Egypt's shade, your humiliation,
Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
4 although their princes are at Zoan, and their messengers have come to Hanes.
Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
5 They will all be ashamed because of a people who cannot help them, who are neither help nor aid, but a shame, and even a disgrace.”
kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
6 A declaration about the beasts of the Negev: Through the land of trouble and danger, of the lioness and the lion, the viper and fiery flying serpent, they carry their riches on the backs of donkeys, and their treasures on the camels' humps, to a people who cannot help them.
Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
7 For Egypt's help is worthless; therefore I have called her Rahab, who sits still.
kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
8 Now go, write it in their presence on a tablet, and inscribe it on a scroll, that it may be preserved for the time to come as a testimony.
Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
9 For these are a rebellious people, lying children, children who will not hear the instruction of Yahweh.
Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
10 They say to the seers, “Do not see;” and to the prophets, “Do not prophesy the truth to us; speak flattering words to us, prophesy illusions.
Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
11 Turn aside from the way, stray off the path; cause the Holy One of Israel to cease speaking before our face.”
Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
12 Therefore the Holy One of Israel says, “Because you reject this word and trust in oppression and deceit and lean on it,
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
13 so this sin will be to you like a broken part ready to fall, like a bulge in a high wall whose fall will happen suddenly, in an instant.”
dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
14 He will break it as a potter's vessel is broken; he will not spare it, so that there will not be found among its pieces a shard with which to scrape fire from the hearth, or to scoop up water out of the cistern.
Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
15 For this is what the Lord Yahweh, the Holy One of Israel says, “In returning and resting you will be saved; in quietness and in trust will be your strength. But you were not willing.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
16 You said, 'No, for we will flee on horses,' so you will flee; and, 'We will ride upon swift horses,' so those who pursue you will be swift.
Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
17 One thousand will flee at the threat of one; at the threat of five you will flee until your remnant will be like a flagstaff on the top of a mountain, or like a flag on a hill.”
Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
18 Yet Yahweh is waiting to be gracious to you, therefore he is ready to show you mercy. For Yahweh is a God of justice; blessed are all those who wait for him.
Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
19 For a people will live in Zion, in Jerusalem, and you will weep no more. He will surely be gracious to you at the sound of your cry. When he hears it, he will answer you.
Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
20 Though Yahweh gives you the bread of adversity and the water of affliction, even so, your teacher will not hide himself anymore, but you will see your teacher with your own eyes.
Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
21 Your ears will hear a word behind you saying, “This is the way, walk in it,” when you turn to the right or when you turn to the left.
Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
22 You will desecrate your carved figures overlaid with silver and your gold cast figures. You will throw them away like a menstrual rag. You will say to them, “Get out of here.”
Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
23 He will give the rain for your seed when you sow the ground, and bread with abundance from the ground, and the crops will be abundant. In that day your cattle will graze in broad pastures.
Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
24 The oxen and the donkeys, who plow the ground, will eat seasoned feed that has been winnowed with a shovel and a fork.
Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
25 On every high mountain and on every high hill, there will be flowing brooks and streams of waters, in the day of the great slaughter when the towers fall.
Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
26 The light of the moon will be like the light of the sun, and the light of the sun will be seven times brighter, like the sunlight of seven days. Yahweh will bind up the breaking of his people and heal the bruises of his wounding them.
Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
27 Look, the name of Yahweh comes from a distant place, burning with his anger and in dense smoke. His lips are full of fury, and his tongue is like a devouring fire.
Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
28 His breath is like an overflowing torrent that reaches up to the middle of the neck, to sift the nations with the sieve of destruction. His breath is a bridle in the jaws of the peoples to cause them to wander away.
Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
29 You will have a song as in the night when a holy feast is observed, and gladness of heart, as when one goes with a flute to the mountain of Yahweh, to the Rock of Israel.
Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
30 Yahweh will make the splendor of his voice heard and show the motion of his arm in storming anger and flames of fire, with windstorm, rainstorm, and hailstones.
Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
31 For at the voice of Yahweh, Assyria will be shattered; he will strike them with a staff.
Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
32 Every stroke of the appointed rod that Yahweh will lay on them will be accompanied with the music of tambourines and harps as he battles and fights with them.
Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
33 For a place of burning was prepared long ago. Indeed, it is prepared for the king, and God has made it deep and wide. The pile is ready with a fire and much wood. The breath of Yahweh, like a stream of brimstone, will set it on fire.
Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.

< Isaiah 30 >