< Isaiah 10 >

1 Woe to those who enact unjust laws and write unfair decrees.
Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
2 They deprive the needy of justice, rob the poor of my people of their rights, plunder widows, and make the fatherless their prey!
kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
3 What will you do on judgment day when the destruction comes from far away? To whom will you flee for help, and where will you leave your wealth?
Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
4 Nothing remains, and you crouch among the prisoners or fall among the killed. In all these things, his anger does not subside; instead, his hand is still stretched out.
Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
5 Woe to the Assyrian, the club of my anger, the rod by whom I wield my fury!
“Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
6 I send him against an arrogant nation and against the people who bear my overflowing wrath. I order him to take the spoil, to take the prey, and to trample them like mud in the streets.
Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
7 But this is not what he intends, nor does he think this way. It is in his heart to destroy and eliminate many nations.
Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
8 For he says, “Are not all my princes kings?
Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
9 Is not Kalno like Carchemish? Is not Hamath like Arpad? Is not Samaria like Damascus?
Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
10 As my hand has overcome idolatrous kingdoms, whose carved figures were greater than those of Jerusalem and Samaria,
Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
11 just as I did to Samaria and her worthless idols, will I not also do the same to Jerusalem and to her idols?”
je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
12 When the Lord has finished his work on Mount Zion and on Jerusalem, I will punish the speech of the arrogant heart of the king of Assyria and his prideful looks.
Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
13 For he says, “By my strength and by my wisdom I acted. I have understanding, and I have removed the boundaries of the peoples. I have stolen their treasures, and like a bull I have brought down the inhabitants.
Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
14 My hand has seized, as from a nest, the wealth of nations, and as one gathers abandoned eggs, I gathered all the earth. None fluttered their wings or opened their mouth or chirped.”
Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
15 Will the ax boast about itself against the one who wields it? Will the saw praise itself more than the one who cuts with it? It is as if a rod could lift up those who raise it, or as if a wooden club could lift up a person.
Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
16 Therefore the Lord Yahweh of hosts will send emaciation among his elite warriors; and under his glory there will be kindled a burning like fire.
Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
17 The light of Israel will become a fire, and his Holy One a flame; it will burn and devour his thorns and briers in one day.
Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
18 Yahweh will consume the glory of his forest and of his fruitful land, both soul and body; it will be like when a sick man's life wastes away.
Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
19 The remnant of the trees of his forest will be so few, that a child could count them.
Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
20 On that day, the remnant of Israel, the family of Jacob that has escaped, will no longer rely on the one who defeated them, but will indeed depend on Yahweh, the Holy One of Israel.
Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
21 A remnant of Jacob will return to the mighty God.
Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
22 For though your people, Israel, are like the sand of the seashore, only a remnant of them will return. Destruction is decreed, as overflowing righteousness demands.
Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
23 For the Lord Yahweh of hosts, is about to carry out the destruction determined throughout the land.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
24 Therefore the Lord Yahweh of hosts says, “My people who live in Zion, do not fear the Assyrian. He will strike you with the rod and raise his staff against you, as the Egyptians did.
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
25 Do not fear him, for in a very short time my anger against you will end, and my anger will lead to his destruction.”
Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
26 Then Yahweh of hosts will wield a whip against them, as when he defeated Midian at the rock of Oreb. He will raise his rod over the sea and lift it up as he did in Egypt.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
27 On that day, his burden is lifted from your shoulder and his yoke from off your neck, and the yoke will be destroyed because of fatness.
Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
28 The enemy has come to Aiath and has passed through Migron; at Michmash he has stored his provisions.
Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
29 They have crossed over the pass and they lodge at Geba. Ramah trembles and Gibeah of Saul has fled.
Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
30 Cry aloud, daughter of Gallim! Give attention, Laishah! You poor Anathoth!
Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
31 Madmenah is fleeing, and the inhabitants of Gebim run for safety.
Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
32 This very day he will halt at Nob and shake his fist at the mountain of the daughter of Zion, the hill of Jerusalem.
Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
33 Behold, the Lord Yahweh of hosts will lop off the boughs with a terrifying crash; the tallest trees will be cut down, and the lofty will be brought low.
Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
34 He will chop down the thickets of the forest with an ax, and Lebanon in his majesty will fall.
Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.

< Isaiah 10 >