< Hosea 8 >
1 “Place a trumpet at your lips! An eagle is coming over the house of Yahweh because the people have broken my covenant and rebelled against my law.
“Weka tarumbeta katika midomo yako! Tai anakuja juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja agano langu na waliasi dhidi ya sheria yangu.
2 They cry out to me, 'My God, we in Israel know you.'
Wananililia,'Mungu wangu, sisi katika Israeli tunakujua.'
3 But Israel has rejected what is good, and the enemy will pursue him.
Lakini Israeli amekataa mema, na adui atamfuata.
4 They have set up kings, but not by me. They have made princes, but without my knowledge. With their silver and gold they have made idols for themselves, but it was only so they might be cut off.”
Wameweka wafalme, lakini sio kwa shauri langu. Wamewafanya wakuu, lakini sikuwa na habari. Kwa fedha zao na dhahabu wamejifanyia sanamu wenyewe, ili wakatiliwe mbali.”
5 “Your calf has been rejected, Samaria. My anger is burning against these people. For how long will they stay guilty?
“Ndama yako imekataliwa, Samaria. Hasira yangu inawaka juu ya watu hawa. Kwa muda gani watakuwa na hatia?
6 For this idol came from Israel; a workman made it; it is not God! The calf of Samaria will be broken to pieces.
Kwa maana sanamu hii ilitoka Israeli; fundi aliifanya; si Mungu! Ndama ya Samaria itavunjwa vipande vipande.
7 For the people sow the wind and reap the whirlwind. The standing grain has no heads; it yields no flour. If it does come to maturity, foreigners will devour it.
Kwa maana watu hupanda upepo na kuvuna kimbunga. Mbegu zilizosimama hazina vichwa; haitoi unga. Ikiwa itakomaa, wageni watakula.
8 Israel is swallowed up; now they lie among the nations like something useless.
Israeli imemezwa; sasa wanalala kati ya mataifa kama kitu kisicho na maana.
9 For they went up to Assyria like a wild donkey all alone. Ephraim has hired lovers for herself.
Kwa maana walikwenda Ashuru kama punda wa mwitu pekee. Efraimu ameajiri wapenzi kwa ajili yake mwenyewe.
10 Even though they have hired lovers among the nations, I will now gather them together. They will begin to waste away because of the oppression of the king of princes.
Hata ingawa wameajiri wapenzi kati ya mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wao wataanza kupotea kwa sababu ya unyanyasaji wa mfalme wa wakuu.
11 For Ephraim has multiplied altars for sin offerings, but they have become altars for committing sins instead.
Kwa maana Efraimu imeongeza madhabahu kwa sadaka za dhambi, lakini zimekuwa madhabahu kwa kufanya dhambi.
12 I could write down my law for them ten thousand times, but they would view it as something strange to them.
Niliweza kuandika sheria yangu kwao mara elfu kumi, lakini wangeiona kama kitu cha ajabu kwao.
13 As for the sacrifices of my offerings, they sacrifice meat and eat it, but I, Yahweh, do not accept them. Now I will think about their iniquity and punish their sins. They will return to Egypt.
Kwa ajili ya dhabihu za sadaka zangu, hutoa nyama na kuila, lakini mimi, Bwana, siwakubali. Sasa nitafikiri juu ya uovu wao na kuadhibu dhambi zao. Watarudi Misri.
14 Israel has forgotten me, his Maker, and has built palaces. Judah has fortified many cities, but I will send fire on his cities; it will destroy his fortresses.
Israeli amenisahau mimi, Muumba wake, na amejenga majumba. Yuda ameimarisha miji mingi, lakini nitatuma moto juu ya miji yake; itaharibu ngome zake.