< Haggai 2 >

1 In the seventh month on the twenty-first day of the month, the word of Yahweh came by the hand of Haggai the prophet, saying,
Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno la Bwana lilikuja kupitia nabii Hagai, kusema:
2 “Speak to the governor of Judah, Zerubbabel son of Shealtiel, and to the high priest Joshua son of Jehozadak, and to the remnant of the people. Say,
“Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize,
3 'Who is left among you who saw this house in its former glory? How do you see it now? Is it not like nothing in your eyes?
‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu?
4 Now, be strong, Zerubbabel!—this is Yahweh's declaration— and be strong, high priest Joshua son of Jehozadak; and be strong, all you people in the land!—this is Yahweh's declaration— and work, for I am with you!—this is the declaration of Yahweh of hosts.
Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asema Bwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asema Bwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
5 This is the covenant that I established with you when you came out of Egypt, and my Spirit remains with you. Do not fear!
‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’
6 For Yahweh of hosts says this: In a little while I will once again shake the heavens and the earth, the sea and the dry land!
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu.
7 I will shake every nation, and every nation will bring their precious things to me, and I will fill this house with glory, says Yahweh of hosts.
Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
8 The silver and gold are mine!—this is the declaration of Yahweh of hosts.
‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 The glory of this house will be greater in the future than at the beginning, says Yahweh of hosts, and I will give peace in this place!—this is the declaration of Yahweh of hosts.”
‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
10 On the twenty-fourth day of the ninth month, in the second year of Darius, the word of Yahweh came by Haggai the prophet, saying,
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilikuja kwa nabii Hagai:
11 “Yahweh of hosts says this: Ask the priests concerning the law, and say,
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema:
12 'If a man carries meat that is set apart to Yahweh in the fold of his garment, and the fold touches bread or stew, wine or oil, or any kind of food, does it become holy?'” The priests answered and said, “No.”
Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’” Makuhani wakajibu, “La hasha.”
13 Then Haggai said, “If someone who is unclean because of death touches any of these things, do they become unclean?” The priests answered and said, “Yes, they become unclean.”
Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?” Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”
14 So Haggai answered and said, “So it is with this people and this nation before me!—this is Yahweh's declaration—and so it is with everything done by their hands. What they offer to me is unclean!
Kisha Hagai akasema, “‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asema Bwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.
15 So now, think in your minds about the past leading up to this very day. Before stone was placed upon stone in the temple of Yahweh,
“‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu la Bwana.
16 how was it then? When you came to a heap of twenty measures of grain, there were only ten; and when you came to the wine vat to draw out fifty measures, there were only twenty.
Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu.
17 I afflicted you and all the work of your hands with blight and mildew, but you still did not turn to me—this is Yahweh's declaration.
Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asema Bwana.
18 Consider from this day forward, from the twenty-fourth day of the ninth month, from the day that the foundation of Yahweh's temple was laid. Consider it!
‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa. Tafakarini:
19 Is there still seed in the storehouse? The vine, the fig tree, the pomegranate, and the olive tree have not produced! But from this day will I bless you!”
Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda. “‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’”
20 Then the word of Yahweh came a second time to Haggai on the twenty-fourth day of the month and said,
Neno la Bwana likamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema:
21 “Speak to the governor of Judah, Zerubbabel, and say, 'I will shake the heavens and the earth.
“Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi.
22 For I will overthrow the throne of kingdoms and destroy the strength of the kingdoms of the nations! I will overthrow the chariots and their riders; the horses and their riders will fall down, each one because of his brother's sword.
Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.
23 On that day—this is the declaration of Yahweh of hosts—I will take you, Zerubbabel son of Shealtiel, as my servant—this is Yahweh's declaration. I will make you like a signet ring, for I have chosen you! —this is the declaration of Yahweh of hosts!'”
“‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asema Bwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”

< Haggai 2 >