< Genesis 45 >
1 Then Joseph could not control himself before all the servants who stood by him. He said loudly, “Everyone must leave me.” So no servant stood by him when Joseph made himself known to his brothers.
Hapo Yosefu hakuweza kujizuia zaidi mbele ya wote waliokuwa wamesimama karibu naye, akapaza sauti, akasema, “Mwondoeni kila mtu mbele yangu!” Kwa hiyo hapakuwepo mtu yeyote pamoja na Yosefu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
2 He wept loudly, the Egyptians heard it, and the house of Pharaoh heard of it.
Naye akalia kwa sauti kubwa kiasi kwamba Wamisri walimsikia, hata watu wa nyumbani mwa Farao wakapata hizo habari.
3 Joseph said to his brothers, “I am Joseph. Is my father still alive?” His brothers could not answer him, for they were shocked in his presence.
Yosefu akawaambia ndugu zake, “Mimi ni Yosefu! Je, baba yangu angali hai bado?” Lakini ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwa sababu walipatwa na hofu kuu mbele yake.
4 Then Joseph said to his brothers, “Come near to me, please.” They came near. He said, “I am Joseph your brother, whom you sold into Egypt.
Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake, “Sogeeni karibu nami.” Waliposogea, akasema, “Mimi ni ndugu yenu Yosefu, yule ambaye mlimuuza Misri!
5 Do not be grieved or angry with yourselves that you sold me here, for God sent me ahead of you to preserve life.
Sasa, msihuzunike wala msijichukie wenyewe kwa kuniuza huku, kwa sababu ilikuwa ni ili kuokoa maisha ya watu ndiyo sababu Mungu alinituma niwatangulie ninyi.
6 For these two years the famine has been in the land, and there are still five years in which there will be neither plowing nor harvest.
Kwa miaka miwili sasa imekuwepo njaa katika nchi, pia kwa miaka mitano ijayo hapatakuwepo kulima wala kuvuna.
7 God sent me ahead of you to preserve you as a remnant in the earth, and to keep you alive by a great deliverance.
Lakini Mungu alinitanguliza mbele yenu ili kuhifadhi mabaki kwa ajili yenu katika nchi, na kuokoa maisha yenu kwa wokovu mkuu.
8 So now it was not you who sent me here but God, and he has made me a father to Pharaoh, master of all his house, and ruler of all the land of Egypt.
“Kwa hiyo basi, si ninyi mlionileta huku, bali ni Mungu. Alinifanya kuwa baba kwa Farao, bwana wa watu wa nyumbani mwake wote, na mtawala wa Misri yote.
9 Hurry and go up to my father and say to him, 'This is what your son Joseph says, “God has made me master of all Egypt. Come down to me, do not delay.
Sasa rudini haraka kwa baba yangu na mwambieni, ‘Hili ndilo mwanao Yosefu asemalo: Mungu amenifanya mimi kuwa bwana wa Misri yote. Shuka uje kwangu, wala usikawie.
10 You will live in the land of Goshen, and you will be near me, you and your children and your children's children, and your flocks and your herds, and all that you have.
Nawe utaishi katika nchi ya Gosheni na kuwa karibu nami, wewe, watoto wako na wajukuu wako, makundi yako ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na vyote ulivyo navyo.
11 I will provide for you there, for there are still five years of famine, so that you do not come to poverty, you, your household, and all that you have.”'
Nitawatunza huko, kwa sababu bado iko miaka mingine mitano inayokuja ya njaa. La sivyo, wewe na nyumba yako na wote ulio nao mtakuwa fukara.’
12 Look, your eyes see, and the eyes of my brother Benjamin, that it is my mouth that speaks to you.
“Mnaweza kujionea wenyewe, hata ndugu yangu Benyamini, kwamba hakika ni mimi ninayezungumza nanyi.
13 You will tell my father about all my honor in Egypt and of all that you have seen. You will hurry and bring my father down here.”
Mwambieni baba yangu juu ya heshima yote niliyopewa huku Misri, na kuhusu kila kitu mlichokiona. Mleteni baba yangu huku haraka.”
14 He hugged his brother Benjamin's neck and wept, and Benjamin wept on his neck.
Ndipo akamkumbatia Benyamini ndugu yake na kulia, naye Benyamini akamkumbatia akilia.
15 He kissed all his brothers and wept over them. After that his brothers talked with him.
Pia akawabusu ndugu zake wote, huku akilia. Baada ya hayo ndugu zake wakazungumza naye.
16 The news of the matter was told in Pharaoh's house: “Joseph's brothers have come.” It pleased Pharaoh and his servants very much.
Habari zilipofika kwenye jumba la Farao kwamba ndugu zake Yosefu wamefika, Farao na maafisa wake wote wakafurahi.
17 Pharaoh said to Joseph, “Say to your brothers, 'Do this: Load your animals and go to the land of Canaan.
Farao akamwambia Yosefu, “Waambie ndugu zako, ‘Fanyeni hivi: Pakieni wanyama wenu mrudi mpaka nchi ya Kanaani,
18 Get your father and your households and come to me. I will give you the good of the land of Egypt, and you will eat the fat of the land.'
mkamlete baba yenu na jamaa zenu kwangu. Nitawapa sehemu nzuri sana ya nchi ya Misri nanyi mtafurahia unono wa nchi.’
19 Now you are commanded, 'Do this, take carts out of the land of Egypt for your children and for your wives. Get your father and come.
“Mnaagizwa pia kuwaambia, ‘Fanyeni hivi: Chukueni magari ya kukokotwa kutoka Misri, kwa ajili ya watoto wenu na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje.
20 Do not be concerned about your possessions, for the good of all the land of Egypt is yours.'”
Msijali kamwe kuhusu mali zenu, kwa sababu mema yote ya Misri yatakuwa yenu.’”
21 The sons of Israel did so. Joseph gave them carts, according to the command of Pharaoh, and gave them provisions for the journey.
Hivyo wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yosefu akawapa magari ya kukokotwa, kama Farao alivyoagiza, pia akawapa mahitaji kwa ajili ya safari yao.
22 To all of them he gave each man changes of clothing, but to Benjamin he gave three hundred pieces of silver and five changes of clothing.
Kila mmoja mavazi mapya, lakini Benyamini akampa shekeli 300 za fedha, na jozi tano za nguo.
23 For his father he sent this: ten donkeys loaded with the good things of Egypt; and ten female donkeys loaded with grain, bread, and other supplies for his father for the journey.
Hivi ndivyo vitu alivyotuma kwa baba yake: punda kumi waliochukua vitu vizuri vya Misri, punda wake kumi waliobeba nafaka, mikate na mahitaji mengine ya safari.
24 So he sent his brothers away and they left. He said to them, “See that you do not quarrel on the journey.”
Akaagana na ndugu zake walipokuwa wakiondoka, akawaambia, “Msigombane njiani!”
25 They went up out of Egypt and came to the land of Canaan, to Jacob their father.
Basi wakatoka Misri na kufika kwa baba yao Yakobo katika nchi ya Kanaani.
26 They told him saying “Joseph is still alive, and he is ruler over all the land of Egypt.” His heart was astonished, for he could not believe what they told him.
Wakamwambia baba yao, “Yosefu angali hai! Ukweli ni kwamba yeye ndiye mtawala wa Misri yote.” Yakobo akapigwa na bumbuazi; hakuwasadiki.
27 They told him all the words of Joseph that he had said to them. When Jacob saw the carts that Joseph had sent to carry him, the spirit of Jacob their father revived.
Lakini walipokwisha kumweleza kila kitu ambacho Yosefu alikuwa amewaambia, na alipoona magari ya kukokotwa Yosefu aliyokuwa amempelekea ya kumchukua aende Misri, roho ya baba yao Yakobo ikahuishwa.
28 Israel said, “It is enough. Joseph my son is still alive. I will go and see him before I die.”
Ndipo Israeli akasema, “Nimesadiki! Mwanangu Yosefu bado yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”