< Genesis 18 >
1 Yahweh appeared to Abraham by the oaks of Mamre, as he sat in the tent doorway in the heat of the day.
Yahwe alimtokea Abraham katika Mialoni ya Mamre, alipokua ameketi mlangoni pa hema wakati wa jua.
2 He looked up and, behold, he saw three men standing across from him. When he saw them, he ran to meet them from the tent door and bowed low to the ground.
Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama mbele yake. Alipo waona, alikimbia kupitia mlango wa hema kuwalaki na kuinama chini hadi ardhini.
3 He said, “Lord, if I have found favor in your eyes, do not pass by and leave your servant.
Akasema, “Bwana, kama nimepata upendelea machoni pako, nakuomba usinipite na kuniacha mtumishi wako.
4 Let a little water be brought, wash your feet, and rest yourselves under the tree.
Naomba maji kidogo yaletwe, mnawe miguu yenu, na mjipumzishe chini ya mti.
5 Let me bring a little food, so that you may refresh yourselves. Afterwards you can go your way, since you have come to your servant.” They replied, “Do as you have said.”
Nami acha nilete chakula kidogo, ili kwamba mjiburudishe wenyewe. Ndipo baadae mwaweza kwenda zenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakasema, “Fanya kama ulivyo sema.”
6 Then Abraham quickly went into the tent to Sarah, and said, “Hurry, get three seahs of fine flour, knead it, and make bread.”
Kisha Abraham akaenda upesi hemani kwa Sara, na akasema, “Harakisha, chukua vipimo vitatu vya unga safi, uukande, na fanya mkate.”
7 Then Abraham ran to the herd, and took a calf that was tender and good, and gave it to the servant, and he hurried to prepare it.
Kisha Abraham akakimbia kundini, akachukua ndama wa ng'ombe aliye laini na mzuri, na akampatia mtumishi na kwa haraka akamwandaa.
8 He took curds and milk, and the calf that had been prepared, and placed the food before them, and he stood by them under the tree while they ate.
Akatwaa siagi na maziwa na ndama aliye kwisha andaliwa, na akaweka chakula mbele yao, naye akasimama karibu nao chini ya mti wakati wanakula.
9 They said to him, “Where is Sarah your wife?” He replied, “There, in the tent.”
Wakamwambia, “Mke wako Sara yuko wapi?” akajibu. “pale hemani.”
10 He said, “I will certainly return to you in the springtime, and see, Sarah your wife will have a son.” Sarah was listening in the tent doorway, which was behind him.
akasema, “Hakika nitarejea kwako majira ya machipuko, na tazama Sara mkeo atakuwa na mtoto wa kiume.” Sara alikuwa akisikiliza mlangoni pa hema iliyokuwa nyuma yake.
11 Now Abraham and Sarah were old, very advanced in age, and Sarah had passed the age when women could bear children.
Abraham na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umeendelea sana, na Sara alikuwa amepita umri ambao mwanamke anaweza kuzaa watoto.
12 So Sarah laughed to herself, saying to herself, “After I am worn-out and my master is old, will I now have this pleasure?”
Kwa hiyo Sara akajicheka mwenyewe, akijisemesha mwenyewe, “baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?”
13 Yahweh said to Abraham, “Why did Sarah laugh and say, 'Will I really bear a child, when I am old'?
Yahwe akamwambia Abraham, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?
14 Is anything too hard for Yahweh? At the time appointed by me, in the spring, I will return to you. About this time next year Sarah will have a son.”
Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe? Itakuwa katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko, nitarejea kwako. Majira haya mwakani Sara atakuwa na mtoto wa kiume.”
15 Then Sarah denied it and said, “I did not laugh,” for she was afraid. He replied, “No, you did laugh.”
Kisha Sara akakataa na kusema, “sikucheka,” kwa kuwa aliogopa. Yahwe akasema, “hapana ulicheka.”
16 Then the men arose to leave and looked down toward Sodom. Abraham went with them to see them on their way.
Kisha wale wanaume walisimama kuondoka na wakatazama chini kuelekea Sodoma. Abraham akafuatana nao kuona njia yao.
17 But Yahweh said, “Should I hide from Abraham what I am about to do,
Lakini Yahwe akasema, Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya,
18 since Abraham will indeed become a great and mighty nation, and all the nations of the earth will be blessed in him?
Ikiwa kwa hakika Abraham atakuwa mkuu na taifa lenye nguvu, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
19 For I have chosen him so that he may instruct his children and his household after him to keep the way of Yahweh, to do righteousness and justice, so that Yahweh may bring upon Abraham what he has said to him.”
Kwa kuwa nimemchagua ili awaelekeze wanawe na nyumba yake baada yake waishike njia ya Yahwe, watende utakatifu na haki, ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake.”
20 Then Yahweh said, “Because the outcry against Sodom and Gomorrah is so great, and because their sin is so serious,
Kisha Yahwe akasema, “Kwa sababu kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu, na kwa kuwa dhambi yao ni kubwa,
21 I will now go down there and see the outcry against her that has come to me, whether they have really done it. If not, I will know.”
sasa nitashuka pale na kuona kilio kilicho nifikia dhidi yake, ikiwa kweli wamefanya au hawakufanya, nitajua.”
22 So the men turned from there, and went toward Sodom, but Abraham remained standing before Yahweh.
Kwa hiyo wale wanaume wakageuka toka pale, na kuelekea Sodoma, lakini Abraham akabaki amesimama mbele ya Yahwe.
23 Then Abraham approached and said, “Will you sweep away the righteous with the wicked?
Kisha Abraham alikaribia na kusema, “Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?
24 Perhaps there are fifty righteous within the city. Will you sweep it away and not spare the place for the sake of the fifty righteous that are there?
Huenda wakawepo wenye haki hamsini katika mji. Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?
25 Far be it from you to do such a thing, killing the righteous with the wicked, so that the righteous should be treated the same as the wicked. Far be it from you! Will not the Judge of all the earth do what is just?”
Hasha usifanye hivyo, kuwauwa watakatifu pamoja na waovu, ili kwamba watakatifu watendewe sawa na waovu. Hasha! Je muhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?”
26 Yahweh said, “If I find in Sodom fifty righteous within the city, then I will spare the whole place for their sake.”
Yahwe akasema, “Katika Sodoma nikipata watakatifu hamsini kwenye mji, nita uacha mji wote kwa ajili ya hao.”
27 Abraham answered and said, “Look, I have undertaken to speak to my Lord, even though I am only dust and ashes!
Abraham akajibu na kusema, “Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu, hata kama mimi ni mavumbi na majivu!
28 What if there are five less than fifty righteous? Will you destroy the whole city for lack of five?” Then he said, “I will not destroy it, if I find there forty-five.”
Itakuwaje ikiwa kuna watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini? Je utaangamiza mji wote kwa upungufu wa hao watano?” Akasema, “Sitaangamiza, ikiwa nitapata watu arobaini na watano pale.”
29 He spoke to him yet again, and said, “What if there are forty found there?” He replied, “I will not do it for the forty's sake.”
Akaongea naye tena, na kusema, “Itakuwaje ikiwa arobaini watapatikana pale?” Akajibu, “Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.”
30 He said, “Please do not be angry, Lord, so I may speak. Perhaps thirty will be found there.” He replied, “I will not do it, if I find thirty there.”
Akasema, Tafadhali usikasirike, Bwana, nikiongea. Pengine thelathini watapatikana pale.” Akajibu, 'Sitafanya, ikiwa nitapata thelathini pale.”
31 He said, “Look, I have undertaken to speak to my Lord! Perhaps twenty will be found there.” He replied, “I will not destroy it for the twenty's sake.”
Akasema, Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu! Pengine ishirini watapatikana pale.” Akajibu, “Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.”
32 He said, “Please do not be angry, Lord, and I will speak this one last time. Perhaps ten will be found there.” Then he said, “I will not destroy it for the ten's sake.”
Akasema, “Tafadhali usikasirike, Bwana, na nitasema jambo hili kwa mara ya mwisho. Huenda kumi wakaonekana kule.” Na akasema, sitaangamiza kwa ajili ya hao kumi.”
33 Yahweh went on his way as soon as he had finished talking with Abraham, and Abraham returned home.
Yahwe akaendelea na njia yake mara tu baada ya kumaliza kuongea na Abraham, na Abraham akarudi nyumbani.