< Genesis 10 >

1 These were the descendants of the sons of Noah, that is, Shem, Ham, and Japheth. Sons were born to them after the flood.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
2 The sons of Japheth were Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Meshech, and Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
3 The sons of Gomer were Ashkenaz, Riphath, and Togarmah.
Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
4 The sons of Javan were Elishah, Tarshish, Kittim, and Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
5 From these the coastland peoples separated and went into their lands, every one with its own language, according to their clans, by their nations.
Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
6 The sons of Ham were Cush, Mizraim, Put, and Canaan.
Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
7 The sons of Cush were Seba, Havilah, Sabtah, Raamah, and Sabteka. The sons of Raamah were Sheba and Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
8 Cush became the father of Nimrod, who was the first conqueror on the earth.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
9 He was a mighty hunter before Yahweh. That is why it is said, “Like Nimrod, a mighty hunter before Yahweh.”
Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
10 The first centers of his kingdom were Babel, Erech, Akkad, and Kalneh, in the land of Shinar.
Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
11 Out of that land he went to Assyria and built Nineveh, Rehoboth Ir, Calah,
Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
12 and Resen, which was between Nineveh and Calah. It was a large city.
na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
13 Mizraim became the father of the Ludites, the Anamites, the Lehabites, the Naphtuhites,
Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
14 the Pathrusites, the Kasluhites (from whom the Philistines came), and the Caphtorites.
Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
15 Canaan became the father of Sidon, his firstborn, and of Heth,
Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16 also of the Jebusites, the Amorites, the Girgashites,
pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
17 the Hivites, the Arkites, the Sinites,
Mhivi, Mwarki, Msini,
18 the Arvadites, the Zemarites, and the Hamathites. Afterward the clans of the Canaanites spread out.
Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
19 The border of the Canaanites was from Sidon, in the direction of Gerar, as far as Gaza, and as one goes toward Sodom, Gomorrah, Admah, and Zeboyim, as far as Lasha.
Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
20 These were the sons of Ham, by their clans, by their languages, in their lands, and in their nations.
Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
21 Sons also were born to Shem, the older brother of Japheth. Shem was also the ancestor of all the people of Eber.
Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
22 The sons of Shem were Elam, Ashur, Arphaxad, Lud, and Aram.
Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
23 The sons of Aram were Uz, Hul, Gether, and Meshech.
Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
24 Arphaxad became the father of Shelah, and Shelah became the father of Eber.
Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
25 Eber had two sons. The name of the one was Peleg, for in his days the earth was divided. His brother's name was Joktan.
Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
26 Joktan became the father of Almodad, Sheleph, Hazarmaveth, Jerah,
Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 Hadoram, Uzal, Diklah,
Hadoram, Uzali, Dikla,
28 Obal, Abimael, Sheba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 Ophir, Havilah, and Jobab. All these were the sons of Joktan.
Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 Their territory was from Mesha, all the way to Sephar, the mountain of the east.
Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
31 These were the sons of Shem, according to their clans and their languages, in their lands, according to their nations.
Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
32 These were the clans of the sons of Noah, according to their genealogies, by their nations. From these the nations separated and went over the earth after the flood.
Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.

< Genesis 10 >