< Galatians 1 >

1 Paul, an apostle—not an apostle from men nor by human agency, but through Jesus Christ and God the Father, who raised him from the dead—
Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
2 and all the brothers with me, to the churches of Galatia:
na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
3 Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ,
Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
4 who gave himself for our sins so that he might deliver us from this present evil age, according to the will of our God and Father, (aiōn g165)
aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
5 to him be the glory forever and ever. Amen. (aiōn g165)
Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
6 I am amazed that you are turning away so quickly from him who called you by the grace of Christ. I am amazed that you are turning to a different gospel.
Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
7 This is not to say that there is another gospel, but there are some men who cause you trouble and want to change the gospel of Christ.
ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
8 But even if we or an angel from heaven should proclaim to you a gospel other than the one we proclaimed to you, let him be cursed.
Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
9 As we have said before, so now I say again, “If someone proclaims to you a gospel other than the one you received, let him be cursed.”
Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
10 For am I now seeking the approval of men or God? Am I seeking to please men? If I am still trying to please men, I am not a servant of Christ.
Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
11 For I want you to know, brothers, that the gospel I proclaimed is not man's gospel.
Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
12 I did not receive it from any man, nor was I taught it. Instead, it was by revelation of Jesus Christ to me.
Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
13 You have heard about my former life in Judaism, how I was persecuting the church of God beyond measure and that I was trying to destroy it.
Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
14 I advanced in Judaism beyond many of those who were my own age, from out of my own people. That is how extremely zealous I was for the traditions of my fathers.
Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
15 But when God, who had set me apart from my mother's womb, and who called me through his grace,
Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
16 was pleased to reveal his Son in me, so that I would proclaim him among the Gentiles, I did not immediately consult with flesh and blood.
alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
17 I did not go up to Jerusalem to those who had become apostles before me. Instead, I went to Arabia and then returned to Damascus.
wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
18 Then after three years I went up to Jerusalem to get to know Cephas and I stayed with him fifteen days.
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
19 But I saw none of the other apostles except James, the Lord's brother.
Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20 In what I write to you, I assure you before God, that I am not lying.
Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
21 Then I went to the regions of Syria and Cilicia.
Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
22 I was still not personally known to the churches of Judea that are in Christ.
Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
23 They only heard it being said, “The man who once persecuted us is now proclaiming the faith he once tried to destroy.”
Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
24 So they glorified God because of me.
Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.

< Galatians 1 >