< Ezra 8 >

1 These are the leaders of their ancestors' families who left Babylon with me during the reign of King Artaxerxes.
Hawa ndio viongozi wa jamaa pamoja na wale walioandikwa ambao walikuja pamoja nami kutoka Babeli wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:
2 Of the descendants of Phinehas, Gershom. Of the descendants of Ithamar, Daniel. Of the descendants of David, Hattush,
wa wazao wa Finehasi, alikuwa Gershoni; wa wazao wa Ithamari, alikuwa Danieli; wa wazao wa Daudi, alikuwa Hatushi
3 who was of the descendants of Shecaniah, who was from the descendants of Parosh; and Zechariah, and with him there were 150 males listed in the record of his genealogy.
wa wazao wa Shekania; wa wazao wa Paroshi, alikuwa Zekaria, na watu 150 walioandikishwa pamoja naye;
4 Of the descendants of Pahath-Moab, Eliehoenai son of Zerahiah and with him were two hundred males.
wa wazao wa Pahath-Moabu, alikuwa Eliehoenai mwana wa Zerahia na wanaume 200 pamoja naye;
5 Of the descendants of Zattu, Ben Jahaziel and with him were three hundred males.
wa wazao wa Zatu, alikuwa Shekania mwana wa Yahazieli na wanaume 300 pamoja naye;
6 Of the descendants of Adin, Ebed son of Jonathan and with him were listed fifty males.
wa wazao wa Adini, alikuwa Ebedi mwana wa Yonathani na wanaume 50 pamoja naye;
7 Of the descendants of Elam, Jeshaiah son of Athaliah and with him were listed seventy males.
wa wazao wa Elamu, alikuwa Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;
8 Of the descendants of Shephatiah, Zebadiah son of Michael and with him were listed eighty males.
wa wazao wa Shefatia, alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli na wanaume 80 pamoja naye;
9 Of the descendants of Joab, Obadiah son of Jehiel and with him were listed 218 males.
wa wazao wa Yoabu, alikuwa Obadia mwana wa Yehieli na wanaume 218 pamoja naye;
10 Of the descendants of Bani, Shelomith son of Josiphiah and with him were listed 160 males.
wa wazao wa Bani, alikuwa Shelomithi mwana wa Yosifia na wanaume 160 pamoja naye;
11 Of the descendants of Bebai, Zechariah son of Bebai and with him were listed twenty-eight males.
wa wazao wa Bebai, alikuwa Zekaria mwana wa Bebai na wanaume 28 pamoja naye;
12 Of the descendants of Azgad, Johanan son of Hakkatan and with him were listed 110 males.
wa wazao wa Azgadi, alikuwa Yohanani mwana wa Hakatani na wanaume 110 pamoja naye;
13 Those of the descendants of Adonikam came later. These were their names: Eliphelet, Jeuel, and Shemaiah and with them came sixty males.
wa wazao wa Adonikamu, hawa walikuwa wa mwisho ambao majina yao ni Elifeleti, Yeueli, Shemaya na wanaume 60 pamoja nao;
14 Of the descendants of Bigvai, Uthai and Zaccur and with him were listed seventy males.
wa wazao wa Bigwai, walikuwa Uthai na Zakuri na wanaume 70 pamoja nao.
15 I gathered the travelers at the canal that goes to Ahava, and we camped there three days. I examined the people and priests, but could not find any descendants of Levi there.
Niliwakusanya kwenye mto utiririkao kuelekea Ahava, nasi tukapiga kambi pale siku tatu. Wakati nilipokagua kati ya watu na makuhani, sikuwapata Walawi.
16 So I sent for Eliezer, Ariel, Shemaiah, Elnathan, Jarib, and Elnathan and Nathan, Zechariah, and Meshullam—who were leaders—and for Joiarib and Elnathan—who were teachers.
Basi niliwaita Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu waliokuwa viongozi na Yoyaribu na Elnathani waliokuwa wasomi,
17 Next I sent them to Iddo, the leader in Kasiphia. I told them what to say to Iddo and his relatives, the temple servants living in Kasiphia, that is, to send to us servants for the house of God.
nikawatuma kwa Ido kiongozi huko Kasifia. Niliwaambia watakayomwambia Ido na ndugu zake, watumishi wa Hekalu huko Kasifia, ili waweze kutuletea wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
18 So they sent us by our God's good hand a man named Sherebiah, a prudent man. He was a descendant of Mahli son of Levi son of Israel. He came with eighteen sons and brothers.
Kwa sababu mkono wa neema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea Sherebia, mtu mwenye uwezo kutoka wazao wa Mahli mwana wa Lawi, mwana wa Israeli, na wana wa Sherebia pamoja na ndugu zao wanaume kumi na wanane.
19 With him came Hashabiah. There also were Jeshaiah, one of the sons of Merari, with his brothers and their sons, twenty men in all.
Naye Hashabia, pamoja na Yeshaya kutoka wazao wa Merari na ndugu zake na wapwa wake wanaume ishirini.
20 Of those assigned to serve in the temple, whom David and his officials gave to serve the Levites: 220, each of them assigned by name.
Vilevile walileta watumishi wa Hekalu 220, kikundi ambacho Daudi na maafisa walikuwa wamekiweka kusaidia Walawi. Wote walikuwa wameorodheshwa kwa majina.
21 Then I proclaimed a fast at the Ahava Canal to humble ourselves before God, to seek a straight path from him for us, our little ones, and all our possessions.
Kando ya Mto Ahava, hapo nilitangaza kufunga, ili tujinyenyekeshe mbele za Mungu wetu na kumwomba kwa ajili ya kutujalia safari ya amani sisi na watoto wetu, pamoja na mali zetu zote.
22 I was ashamed to ask the king for an army or horsemen to protect us against enemies along the way, since we had said to the king, 'The hand of our God is on all who seek him for good, but his might and wrath are on all who forget him.'
Niliona aibu kumwomba mfalme askari na wapanda farasi wa kutulinda njiani kutokana na adui zetu, kwa sababu tulikwisha kumwambia mfalme, “Mkono wa neema wa Mungu wetu uko juu ya kila mmoja anayemtafuta, lakini hasira yake kubwa ni dhidi ya wote wamwachao.”
23 So we fasted and sought God about this, and we pled to him.
Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hili, naye akajibu maombi yetu.
24 Next I selected twelve men from the priestly officials: Sherebiah, Hashabiah, and ten of their brothers.
Kisha niliwatenga viongozi wa makuhani kumi na wawili, pamoja na Sherebia, Hashabia na ndugu zao kumi,
25 I weighed out for them silver, gold, and the objects and offerings for the house of God that the king, his counselors and officials, and all Israel had freely offered.
nami nikawapimia fedha, dhahabu na vifaa ambavyo mfalme, washauri wake, maafisa wake na Israeli wote waliokuwepo walikuwa wamevitoa sadaka kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
26 So I weighed into their hand 650 talents of silver, one hundred talents of silver objects, one hundred talents of gold,
Niliwapimia talanta 650 za fedha, vifaa vingine vya fedha vya uzito wa talanta mia moja, talanta mia moja za dhahabu,
27 twenty gold bowls that were together valued at one thousand darics, and two well-polished bronze vessels as precious as gold.
mabakuli ishirini ya dhahabu ya thamani ya darkoni elfu moja, na vyombo viwili vya shaba iliyosuguliwa, ya thamani kama dhahabu.
28 Then I said to them, “You are consecrated to Yahweh, and these objects also, and the silver and gold are a freewill offering to Yahweh, the God of your ancestors.
Niliwaambia, “Ninyi pamoja na vyombo hivi ni wakfu kwa Bwana. Fedha na dhahabu ni sadaka ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu.
29 Watch over them and keep them until you weigh them out before the priestly officials, Levites, and leaders of the ancestors' clans of Israel in Jerusalem in the rooms of God's house.”
Vilindeni kwa uangalifu mpaka mtakapovipima ndani ya vyumba vya nyumba ya Bwana katika Yerusalemu mbele ya makuhani, viongozi na Walawi pamoja na wakuu wa jamaa za Israeli.”
30 The priests and the Levites accepted the weighed silver, gold, and the objects in order to take them to Jerusalem, to our God's house.
Ndipo makuhani na Walawi wakapokea fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu ambavyo vilipimwa na kupelekwa katika nyumba ya Mungu wetu mjini Yerusalemu.
31 We went out from the Ahava Canal on the twelfth day of the first month to go to Jerusalem. The hand of our God was on us; he protected us from the hand of the enemy and the ones who wished to ambush us along the road.
Tulianza safari kutoka Mto Ahava kwenda Yerusalemu kwenye siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza. Mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye njiani alitulinda dhidi ya adui na wanyangʼanyi.
32 So we entered Jerusalem and stayed there for three days.
Kwa hiyo tuliwasili Yerusalemu ambapo tulipumzika kwa siku tatu.
33 Then on the fourth day the silver, gold, and objects were weighed out in our God's house into the hand of Meremoth son of Uriah the priest, and with him were Eleazar son of Phinehas, Jozabad son of Jeshua, and Noadiah son of Binnui the Levite.
Katika siku ya nne, ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tulipima fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu, tukakabidhi mikononi mwa kuhani Meremothi mwana wa Uria. Eleazari mwana wa Finehasi alikuwa pamoja naye, pia walikuwako Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.
34 The number and weight of everything was determined. All the weight was written down at that time.
Kila kitu kilihesabiwa kwa idadi na kupimwa kwa uzito, nao uzito wote uliandikwa wakati ule.
35 The ones who came back from the captivity, the people of exile, offered burnt offerings to the God of Israel: twelve bulls for all of Israel, ninety-six rams, seventy-seven lambs, and twelve male goats as a sin offering. All were a burnt offering for Yahweh.
Kisha mateka waliokuwa wamerudi kutoka utumwani wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mungu wa Israeli: mafahali kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, kondoo dume tisini na sita, wana-kondoo sabini na saba na mbuzi dume kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi. Hii yote ilikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa Bwana.
36 Then they gave the king's decrees to the king's high officials and the governors in the Province Beyond the River, and they helped the people and the house of God.
Pia walikabidhi manaibu wa mfalme na watawala wa Ngʼambo ya Mto Frati maagizo ya mfalme, ambao baadaye walitoa msaada kwa watu na kwa nyumba ya Mungu.

< Ezra 8 >