< Ezekiel 9 >
1 Then he cried in my hearing with a loud voice, and said, “Let the guards come up to the city, each with his weapon of destruction in his hand.”
Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
2 Then behold! Six men came from the pathway of the upper gate that faces north, each with his weapon of slaughter in his hand. There was a man in their midst dressed in linen with a scribe's equipment at his side. So they went in and stood beside the bronze altar.
Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu, linalotazama kaskazini kila mmoja na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Pamoja nao alikuwepo mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande mmoja. Wakaingia ndani ya Hekalu wakasimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
3 Then the glory of the God of Israel went up from the cherubim where it had been to the threshold of the house. He called to the man dressed in linen who had the scribe's equipment at his side.
Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Bwana akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi aliyekuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja,
4 Yahweh said to him, “Pass through the midst of the city—the midst of Jerusalem—and make a mark on the foreheads of those who groan and sigh about all the abominations being performed in the midst of the city.”
akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
5 Then he spoke to the others within my hearing, “Pass through the city after him and kill. Do not let your eyes have compassion, and do not spare
Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
6 either old man, young man, virgin, little children or women. Kill all of them! But do not approach anyone who has the mark on his head. Begin at my sanctuary!” So they began with the elders who were in front of the house.
Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
7 He said to them, “Defile the house, and fill its courtyards with the dead. Proceed!” So they went out and attacked the city.
Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze kumbi zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda wakaanza kuua watu mjini kote.
8 As they were attacking it, I found myself alone and I fell on my face and cried out and said, “Ah, Lord Yahweh, will you destroy all the remnant of Israel in the outpouring of your wrath on Jerusalem?”
Wakati walikuwa wakiwaua watu, nami nilikuwa nimeachwa peke yangu, nikaanguka kifudifudi, nikapiga kelele nikisema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
9 He said to me, “The iniquity of the house of Israel and Judah is exceedingly great. The land is full of blood and the city full of perversions, since they say, 'Yahweh has forgotten the land,' and 'Yahweh does not see!'
Bwana akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Bwana ameiacha nchi, Bwana hauoni.’
10 So then, my eye will not look with compassion, and I will not spare them. I will instead bring it all on their heads.”
Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwaachilia lakini nitaleta juu ya vichwa vyao, yale waliyoyatenda.”
11 Behold! The man dressed in linen who had the scribe's equipment by his side came back. He reported and said, “I have done all that you have commanded.”
Ndipo mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani safi na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja, akarudi na kutoa taarifa akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”