< Ezekiel 21 >
1 Then the word of Yahweh came to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 “Son of man, set your face toward Jerusalem, and speak against the sanctuaries; prophesy against the land of Israel.
“Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
3 Say to the land of Israel, 'Yahweh says this: Behold! I am against you! I will draw my sword from its sheath and cut off both the righteous person and the wicked person from you!
uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
4 In order for me to cut off both the righteous and the wicked from you, my sword will go out from its sheath against all flesh from the south to the north.
Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
5 Then all flesh will know that I, Yahweh, have drawn my sword from its sheath. It will no longer hold back!'
Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
6 As for you, son of man, groan as your loins break! In bitterness groan before their eyes!
“Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
7 Then it will happen that they will ask you, 'For what reason are you groaning?' Then you will say, 'Because of the news that is coming, for every heart will faint away, and every hand will falter! Every spirit will grow faint, and every knee will flow like water. Behold! It is coming and it will be like this!—this is the Lord Yahweh's declaration.'”
Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
8 Then the word of Yahweh came to me, saying,
Neno la Bwana likanijia, kusema:
9 “Son of man, prophesy and say, 'The Lord says this: “Say: A sword! A sword! It will be sharpened and polished!
“Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
10 It will be sharpened in order to engage in great slaughter! It will be polished in order to be like lightning! Should we rejoice in my son's scepter? The coming sword hates every such rod!
umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
11 So the sword will be given to be polished, and then to be grasped by the hand! The sword is sharpened and it is polished and it is to be given into the hand of the one who kills!”'”
“‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
12 Call for help and lament, son of man! For that sword has come against my people! It is against all the leaders of Israel. They are thrown against the sword with my people. Therefore, slap your thigh!
Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
13 For there is a trial, but what if the scepter does not last?—this is the Lord Yahweh's declaration.
“‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
14 Now you, son of man, prophesy and hit your two hands together, for the sword will attack even a third time! A sword for the ones to be slaughtered! It is a sword for the many to be slaughtered, piercing them everywhere!
“Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
15 In order to melt their hearts and to multiply their fallen, I have set the sword for slaughter at all their gates. Ah! It is made like lightning, it is grasped for slaughter.
Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
16 You, sword! Strike to the right! Strike to the left! Go wherever your face is turned.
Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
17 For I will also hit my two hands together, and then I will bring my fury to rest! I, Yahweh, declare it!”
Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
18 The word of Yahweh came to me again, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
19 “Now you, son of man, assign two roads for the sword of the king of Babylon to come. The two roads will start in the same land, and a signpost will mark one of them as leading to a city.
“Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
20 Mark one road for the Babylonian army to come to Rabbah, the city of the Ammonites. Mark the other to lead the army to Judah and the city of Jerusalem, which is fortified.
Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
21 For the king of Babylon will stop at the crossroads, at the junction, in order to practice divination. He will shake some arrows and ask direction from some idols and he will examine a liver.
Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
22 In his right hand will be an omen about Jerusalem, to set battering rams against it, to open his mouth to order the slaughter, to sound a war cry, to set battering rams against the gates, to build a ramp, and to erect siege towers.
Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
23 It will seem to be a useless omen in the eyes of the ones in Jerusalem, those who had sworn an oath to the Babylonians! But the king will accuse them of violating their treaty in order to besiege them!
Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
24 Therefore the Lord Yahweh says this: Because you have made your guilt to be remembered, making your transgressions to be revealed, so that in all your actions your sins will be seen— because you have done this you will be taken in hand.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
25 As for you, profane and wicked ruler of Israel, whose day of punishment has come, and whose time of committing iniquity has ended,
“‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
26 the Lord Yahweh says this to you: Remove the turban and take off the crown! Things will no longer be the same! Exalt the lowly and humble the exalted!
hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
27 A ruin! A ruin! I will make it a ruin! It will not be restored until the one comes who is assigned to execute judgment.
Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
28 So you, son of man, prophesy and say, 'The Lord Yahweh says this to the people of Ammon concerning their coming disgrace: A sword, a sword is drawn! It is sharpened for the slaughter in order to devour, so it will be like lightning!
“Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
29 While prophets see empty visions for you, while they perform rituals to come up with lies for you, this sword will lie on the necks of the wicked who are about to be killed, whose day of punishment has come and whose time of iniquity is about to end.
Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 Return the sword to its sheath. In the place of your creation, in the land of your origin, I will judge you!
Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
31 I will pour out my indignation on you! I will fan the fire of my rage against you and put you into the hand of cruel men, craftsmen of destruction!
Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
32 You will become fuel for the fire! Your blood will be in the midst of the land. You will not be remembered, for I, Yahweh have declared this!'”
Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”