< Ezekiel 12 >
1 The word of Yahweh came to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 “Son of man, you live in the midst of a rebellious house, where they have eyes to see but they do not see; and where they have ears to hear but do not listen, because they are a rebellious house.
“Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.
3 Therefore as for you, son of man, prepare your things for exile, and begin going out by day in their sight, for I will exile you in their sight from your place to another place. Perhaps they will begin to see, though they are a rebellious house.
“Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi.
4 You will bring out your things for an exile in the day in their sight; go out in the evening in their sight in the way that anyone goes into exile.
Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni.
5 Dig a hole through the wall in their sight, and go out through it.
Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.
6 In their sight, lift up your things onto your shoulder, and bring them out in the darkness. Cover your face, for you must not see the land, since I have set you as a sign to the house of Israel.”
Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.”
7 So I did this, just as I was commanded. I brought out my things of exile in the daytime, and in the evening I dug a hole through the wall by hand. I brought my things out in the dark, and lifted them up on my shoulder in their sight.
Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama.
8 Then the word of Yahweh came to me in the morning, saying,
Asubuhi neno la Bwana likanijia kusema:
9 “Son of man, is the house of Israel, that rebellious house, not asking, 'What are you doing?'
“Mwanadamu, je, nyumba ile ya kuasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’
10 Say to them, 'The Lord Yahweh says this: this prophetic action concerns the prince in Jerusalem, and all the house of Israel in whose midst they are.'
“Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Neno hili linamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ambao wako huko.’
11 Say, 'I am a sign to you.' As I have done, so it will be done to them; they will go into exile and into captivity.
Waambie, ‘Mimi ndiye ishara kwenu.’ “Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Watakwenda uhamishoni kama mateka.
12 The prince who is among them will lift up his things upon his shoulder in the dark, and will go out through the wall. They will dig through the wall and bring out their things. He will cover his face, so he will not see the land with his eyes.
“Naye mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani mwake kwenye giza la jioni na kuondoka na tundu litatobolewa ukutani kwa ajili yake ili kupitia hapo. Atafunika uso wake ili kwamba asiweze kuiona nchi.
13 I will spread out my net over him and he will be caught in my snare; then I will bring him to Babylon, the land of the Chaldeans, but he will not see it. He will die there.
Nitatandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa kwenye mtego wangu, nitamleta mpaka Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko.
14 I will also scatter in every direction all of those around him who were to assist him and his entire army, and I will send out a sword after them.
Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote, watumishi wake na majeshi yake yote, nami nitawafuatilia kwa upanga uliofutwa.
15 Then they will know that I am Yahweh, when I scatter them among the nations and disperse them throughout the lands.
“Wao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
16 But I will spare a few men from among them from the sword, famine, and plague, so they may record all of their abominations in the lands where I take them, so they will know that I am Yahweh.”
Lakini nitawaacha wachache wao waokoke na upanga, njaa na tauni, ili kwamba katika mataifa watakakokwenda waweze kutambua matendo ya machukizo waliotenda. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
17 The word of Yahweh came to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
18 “Son of man, eat your bread with trembling, and drink your water with shaking and worry.
“Mwanadamu, tetemeka wakati ulapo chakula chako, tetemeka kwa hofu wakati unywapo maji yako.
19 Then say to the people of the land, 'The Lord Yahweh says this concerning the inhabitants of Jerusalem, and the land of Israel, “They will eat their bread with trembling and drink their water while shaking, since the land will be despoiled of its fullness because of the violence of all those who live there.
Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu hao wanaoishi Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyangʼanywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo.
20 So the cities that were inhabited will be desolate, and the land will become a wasteland; so you will know that I am Yahweh.”'”
Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.’”
21 Again the word of Yahweh came to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
22 “Son of man, what is this proverb that you have in the land of Israel that says, 'The days are prolonged, and every vision fails'?
“Mwanadamu, ni nini hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia?’
23 Therefore, say to them, 'The Lord Yahweh says this: I will put an end to this proverb, and the people of Israel will no longer use it.' Say to them, 'The days have drawn near when every vision will be fulfilled.
Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia wakati kila maono yatakapotimizwa.
24 For there will no longer be any false visions or favorable divinations within the house of Israel.
Kwa maana hapatakuwepo tena na maono ya uongo wala ubashiri wa udanganyifu miongoni mwa watu wa Israeli.
25 For I am Yahweh! I speak, and I carry out the words that I speak. The matter will no longer be delayed. For I will speak this word in your days, rebellious house, and I will carry it out!—this is the Lord Yahweh's declaration.'”
Lakini Mimi Bwana nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa maana katika siku zako, wewe nyumba ya kuasi, nitatimiza kila nisemalo, asema Bwana Mwenyezi.’”
26 Again the word of Yahweh came to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
27 “Son of man! Behold, the house of Israel has said, 'The vision that he sees is for many days from now, and he prophesies of far off times.'
“Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’
28 Therefore say to them, 'The Lord Yahweh says this: My words will not be delayed any longer, but the word that I have spoken will be done—this is the Lord Yahweh's declaration.'”
“Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema Bwana Mwenyezi.’”