< Ezekiel 11 >
1 Then the Spirit lifted me up and brought me to the eastern gate of Yahweh's house, facing east, and behold, in the doorway of the gate there were twenty-five men. I saw Jaazaniah son of Azzur and Pelatiah son of Benaiah, leaders of the people, among them.
Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
2 God said to me, “Son of man, these are the men who devise iniquity, and who decide wicked plans in this city.
Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
3 They are saying, 'The time to build houses is not now; this city is the pot, and we are the meat.'
Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
4 Therefore prophesy against them. Prophesy, son of man.”
Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
5 Then the Spirit of Yahweh fell on me and he said for me to say: This is what Yahweh says, “That is what you are saying, house of Israel; for I know what goes through your mind.
Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
6 You have multiplied the people you have killed in this city and filled its streets with them.
Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
7 Therefore, the Lord Yahweh says this: The people you have killed, whose bodies you have laid in the midst of Jerusalem, are the meat, and this city is the pot. But you are going to be brought out from the midst of this city.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
8 You have feared the sword, so I am bringing the sword upon you—this is the declaration of the Lord Yahweh.
Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
9 I will bring you out of the midst of the city, and put you into the hands of foreigners, for I will bring judgment against you.
Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
10 You will fall by the sword. I will judge you within the borders of Israel so you will know that I am Yahweh.
Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
11 This city will not be your cooking pot, nor will you be the meat within her midst. I will judge you within the borders of Israel.
Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
12 Then you will know that I am Yahweh, the one whose statutes you have not walked in and whose decrees you have not carried out. Instead, you have carried out the decrees of the nations that surround you.”
Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
13 It came about that as I was prophesying, Pelatiah son of Benaiah, died. So I fell on my face and cried out with a loud voice and said, “Alas, Lord Yahweh, will you completely destroy the remnant of Israel?”
Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
14 The word of Yahweh came to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
15 “Son of man, your brothers! Your brothers! The men of your clan and all the house of Israel! All of them are those of whom it is said by those living in Jerusalem, 'They are far away from Yahweh! This land was given to us as our possession.'
“Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
16 Therefore say, 'The Lord Yahweh says this: Though I have removed them far off among the nations, and though I have scattered them among the lands, yet I have been a sanctuary for them for a little while in the lands where they have gone.'
“Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
17 Therefore say, 'The Lord Yahweh says this: I will gather you from the peoples, and assemble you from the lands where you were scattered, and I will give you the land of Israel.'
“Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
18 Then they will go there and remove every detestable thing and every abomination from that place.
“Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
19 I will give them one heart, and I will put a new spirit within them. I will take out the heart of stone from their flesh and give them a heart of flesh,
Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
20 so that they will walk in my statutes, they will carry out my decrees and do them. Then they will be my people, and I will be their God.
Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
21 But to those who walk with affection toward their detestable things and their abominations, I will bring their conduct on their own heads—this is the Lord Yahweh's declaration.”
Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
22 The cherubim lifted up their wings and the wheels that were beside them, and the glory of the God of Israel was high up over them.
Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
23 Then the glory of Yahweh went up from within the midst of the city and stood on the mountain to the east of the city.
Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
24 The Spirit lifted me up and brought me into Chaldea, to the exiles, in the vision from the Spirit of God, and the vision that I had seen went up from upon me.
Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
25 Then I declared to the exiles all the things of Yahweh that I had seen.
nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.