< Exodus 8 >
1 Then Yahweh spoke to Moses, “Go to Pharaoh and tell him, 'Yahweh says this: “Let my people go so that they may worship me.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
2 If you refuse to let them go, I will afflict all your country with frogs.
Kama ukikataa kuwaruhusu kuondoka, basi nitaipiga nchi yako yote kwa kuwaletea vyura.
3 The river will swarm with frogs. They will come up and go into your house, your bedroom, and your bed. They will go into your servants' houses. They will go onto your people, into your ovens, and into your kneading bowls.
Mto Naili utafurika vyura. Watakuja kwenye jumba lako la kifalme na katika chumba chako cha kulala na kitandani mwako, katika nyumba za maafisa wako na kwa watu wako, vyura hao wataingia katika meko yenu na kwenye vyombo vya kukandia unga.
4 The frogs will attack you, your people, and all your servants.”'”
Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako na maafisa wako wote.’”
5 Yahweh said to Moses, “Say to Aaron, 'Reach out with your hand and your staff over the rivers, the streams, and the pools, and bring the frogs up over the land of Egypt.'”
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha mkono wako ukiwa na ile fimbo yako juu ya vijito, mifereji na madimbwi, fanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’”
6 Aaron reached out with his hand over Egypt's waters, and the frogs came up and covered the land of Egypt.
Ndipo Aroni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, nao vyura wakatokea na kuifunika nchi.
7 But the magicians did the same with their magic; they brought up frogs over the land of Egypt.
Lakini waganga wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao, nao pia wakafanya vyura kuja juu ya nchi ya Misri.
8 Then Pharaoh called for Moses and Aaron and said, “Pray to Yahweh for him to take away the frogs from me and my people. Then I will let the people go, that they may sacrifice to him.”
Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kusema, “Mwombeni Bwana awaondoe vyura kutoka kwangu na kwa watu wangu, nami nitawaachia watu wenu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
9 Moses said to Pharaoh, “You can have the privilege of telling me when I should pray for you, your servants, and your people, so that the frogs may be removed from you and your houses and stay only in the river.”
Mose akamwambia Farao, “Ninakupa heshima ya kuamua ni wakati gani wa kukuombea wewe, maafisa wako na watu wako ili kwamba vyura watoke kwenu na kwenye nyumba zenu. Isipokuwa wale walio katika Mto Naili.”
10 Pharaoh said, “Tomorrow.” Moses said, “Let it be as you say, so that you may know that there is no one like Yahweh, our God.
Farao akasema, “Kesho.” Mose akamjibu, “Itakuwa kama unavyosema, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote kama Bwana Mungu wetu.
11 The frogs will go from you, your houses, your servants, and your people. They will stay only in the river.”
Vyura wataondoka kwako na katika nyumba zako, kwa maafisa wako na kwa watu wako, ila watabakia katika Mto Naili tu.”
12 Moses and Aaron went out from Pharaoh. Then Moses cried out to Yahweh concerning the frogs that he had brought on Pharaoh.
Baada ya Mose na Aroni kuondoka kwa Farao, Mose akamlilia Bwana kuhusu vyura aliokuwa amewaleta kwa Farao.
13 Yahweh did as Moses asked: The frogs died in the houses, courts, and fields.
Naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Vyura wakafia ndani ya nyumba, viwanjani na mashambani.
14 The people gathered them together in heaps, and the land stank.
Wakayakusanya malundo, nchi nzima ikanuka.
15 But when Pharaoh saw that there was relief, he hardened his heart and did not listen to Moses and Aaron, just as Yahweh had said that he would do.
Lakini Farao alipoona pametokea nafuu, akaushupaza moyo wake na hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
16 Yahweh said to Moses, “Say to Aaron, 'Reach out with your staff and strike the dust on the ground, that it may become gnats throughout all the land of Egypt.'”
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha fimbo yako uyapige mavumbi ya ardhi,’ nayo nchi yote ya Misri mavumbi yatakuwa viroboto.”
17 They did so: Aaron reached out with his hand and his staff. He struck the dust on the ground. Gnats came onto man and beast. All the dust on the ground became gnats throughout the whole land of Egypt.
Wakafanya hivyo, Aroni aliponyoosha mkono wake wenye fimbo na kuyapiga mavumbi ya nchi, viroboto wakawajia watu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi ya Misri yakawa viroboto.
18 The magicians tried with their magic to produce gnats, but they could not. There were gnats on man and beast.
Lakini waganga walipojaribu kutengeneza viroboto kwa siri ya uganga wao, hawakuweza. Nao viroboto walikuwa juu ya watu na wanyama.
19 Then the magicians said to Pharaoh, “This is the finger of God.” But Pharaoh's heart was hardened, so he refused to listen to them. It was just as Yahweh had said Pharaoh would do.
Waganga wale wakamwambia Farao, “Hiki ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ukawa mgumu naye hakuwasikiliza, kama vile Bwana alivyosema.
20 Yahweh said to Moses, “Get up early in the morning and stand in front of Pharaoh as he goes out to the river. Say to him, 'Yahweh says this: “Let my people go so that they may worship me.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi na usimame mbele ya Farao wakati anapokwenda mtoni nawe umwambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
21 But if you do not let my people go, I will send swarms of flies on you, your servants, and your people, and into your houses. The Egyptians' houses will be full of swarms of flies, and even the ground on which they stand will be full of flies.
Kama hutawaachia watu wangu waondoke nitakupelekea makundi ya mainzi juu yako, kwa maafisa wako, kwa watu wako na kwenye nyumba zenu. Nyumba za Wamisri zitajazwa mainzi, hata na ardhi yote ya Misri.
22 But on that day I will treat the land of Goshen differently, the land in which my people are living, so that no swarms of flies will be there. This will happen so that you may know that I am Yahweh in the midst of this land.
“‘Lakini siku ile nitafanya kitu tofauti katika nchi ya Gosheni, ambapo watu wangu wanaishi, hapatakuwepo na makundi ya mainzi, ili mpate kujua kwamba Mimi, Bwana, niko katika nchi hii.
23 I will make a distinction between my people and your people. This sign of my power will take place tomorrow.”'”
Nitaweka tofauti kati ya watu wangu na watu wenu. Ishara hii ya ajabu itatokea kesho.’”
24 Yahweh did so, and thick swarms of flies came into Pharaoh's house and into his servants' houses. Throughout the whole land of Egypt, the land was ruined because of the swarms of flies.
Naye Bwana akafanya hivyo. Makundi makubwa ya mainzi yalimiminika katika jumba la kifalme la Farao na katika nyumba za maafisa wake, pia nchi yote ya Misri ikaharibiwa na mainzi.
25 Pharaoh called for Moses and for Aaron and said, “Go, sacrifice to your God in our own land.”
Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kuwaambia, “Nendeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu katika nchi hii.”
26 Moses said, “It is not right for us to do so, for the sacrifices we make to Yahweh our God are something disgusting to the Egyptians. If we make sacrifices right before their eyes that are disgusting to the Egyptians, will they not stone us?
Lakini Mose akamwambia, “Hilo halitakuwa sawa. Dhabihu tutakazomtolea Bwana Mungu wetu zitakuwa chukizo kwa Wamisri. Kama tukitoa dhabihu ambazo ni chukizo mbele yao, je, hawatatupiga mawe?
27 No, it is a three days' journey into the wilderness that we must make, in order to sacrifice to Yahweh our God, as he commands us.”
Ni lazima twende mwendo wa siku tatu mpaka tufike jangwani ili tumtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, kama alivyotuagiza.”
28 Pharaoh said, “I will allow you to go and sacrifice to Yahweh your God in the wilderness. Only you must not go very far away. Pray for me.”
Farao akamwambia, “Nitawaruhusu mwende kumtolea Bwana Mungu wenu dhabihu huko jangwani, lakini hamna ruhusa kwenda mbali sana. Sasa mniombee.”
29 Moses said, “As soon as I go out from you, I will pray to Yahweh that the swarms of flies may leave you, Pharaoh, and your servants and people tomorrow. But you must not deal deceitfully any more by not letting our people go to sacrifice to Yahweh.”
Mose akajibu, “Mara tu nitakapoondoka, nitamwomba Bwana na kesho mainzi yataondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake. Hakikisha tu kwamba Farao hatatenda kwa udanganyifu tena kwa kutokuwaachia watu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
30 Moses went out from Pharaoh and prayed to Yahweh.
Ndipo Mose akamwacha Farao na kumwomba Bwana,
31 Yahweh did as Moses asked; and he removed the swarms of flies from Pharaoh, his servants, and his people. Not one remained.
naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Mainzi yakaondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake, wala hakuna hata inzi aliyebakia.
32 But Pharaoh hardened his heart this time also, and he did not let the people go.
Lakini wakati huu pia Farao akaushupaza moyo wake, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.