< Exodus 23 >

1 You must not give a false report about anyone. Do not join with a wicked man to be a dishonest witness.
Haupaswi kutoa taarifa ya uongo kuhusu yeyote. usijiunge na mwanaume muovu kuwa shahidi wa uongo.
2 You must not follow a crowd to do evil, nor may you bear witness while siding with the crowd in order to pervert justice.
Haupaswi kufuata umati kufanya uovu, wala kutoa ushahidi ukiwa na umati ili kupotosha haki.
3 You must not show favoritism to a poor man in his lawsuit.
Haupaswi kumpendelea mwanaume maskini kwenye kesi yake.
4 If you meet your enemy's ox or his donkey going astray, you must bring it back to him.
Ukikutana na ng'ombe wa adui wako au punda wake amepotea, lazima umrudishie.
5 If you see the donkey of someone who hates you fallen to the ground under its load, you must not leave that person. You must surely help him with his donkey.
Ukiona punda wa yule anaye kuchukia ameanguka chini na mzigo wake, hauta muacha huyo mtu. Lazima umsaidie na punda wake
6 Do not thrust aside justice for your poor in his lawsuit.
Haupaswi kupotosha haki kama yapaswa kwenda kwa watu maskini katika kesi ya mwanaume maskini.
7 Do not join others in making false accusations, and do not kill the innocent or righteous, for I will not acquit the wicked.
Usijiunge na wengine kufanya shutuma za uongo, na usiue asiye na hatia wala mwenye haki, kwa kuwa sitamuacha muovu.
8 Never take a bribe, for a bribe blinds those who see, and perverts honest people's words.
Husiwai chukuwa rushwa, kwa kuwa rushwa inawapofusha wanaoona, na kupotosha maneno ya wakweli.
9 You must not oppress a foreigner, since you know the life of a foreigner, for you were foreigners in the land of Egypt.
Haupaswi kumnyanyasa mgeni, kwa kuwa wewe ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri.
10 For six years you will sow seed on your land and gather in its produce.
Kwa miaka sita utapanda mbegu kwenye nchi yako na kukusanya mazao yake.
11 But in the seventh year you will leave it unplowed and fallow, so that the poor among your people may eat. What they leave, the wild animals will eat. You will do the same with your vineyards and olive orchards.
Lakini katika mwezi wa saba utaacha hakujalimwa, ili kwamba maskini miongoni mwenu wale. Wanacho acha, wanyama wa porini watakula. Utafanya hivyo na mashamba yenu ya mizabibu na ya mizaituni.
12 During six days you will do your work, but on the seventh day you must rest. Do this so that your ox and your donkey may have rest, and so that your female slave's son and any foreigner may rest and be refreshed.
Wakati wa siku sita utafanya kazi, lakini siku ta saba utapumzika. Fanya hivi ili ng'ombe na punda wako wapumzike, na ili wana wa watumwa wako wa kike na wageni wapumzike na kupata hauweni.
13 Pay attention to everything that I have said to you. Do not mention the names of other gods, nor let their names be heard from your mouth.
Kuwa makini kwa kila kitu nilicho kwambia. Husitaje majina ya miungu mingine, wala kuruhusu majina yao kusikika kutoka mdomoni mwako.
14 You must travel to hold a festival for me three times every year.
Lazima usafiri kusherehekea mara tatu kwa ajili yangu kila mwaka.
15 You are to observe the Festival of Unleavened Bread. As I commanded you, you will eat unleavened bread for seven days. At that time, you will appear before me in the month of Aviv, which is fixed for this purpose. It was in this month that you came out from Egypt. But you must not appear before me empty-handed.
Lazima uadhimishe sherehe ya Mkate usiotiwa Chachu. Kama nilivyo kuamuru, utakula mkate usiotiwa chachu kwa siku saba. Wakati huo, utajitokeza kwangu mwezi wa Abibu, uliowekwa kwa ajili ya kusudi hili. Ni kwa mwezi huu uliyo toka Misri. Lakini usijitokeze kwangu mikono mitupu.
16 You must observe the Festival of Harvest, the firstfruits of your labors when you sowed seed in the fields. Also you must observe the Festival of Ingathering at the end of the year, when you gather in your produce from the fields.
Lazima uadhimishe Sherehe ya Mavuno, matunda ya kwanza ya kazi yako ulipo panda mbegu shambani. Pia lazima uadhimishe Sherehe ya Ukusanyaji wa mwisho wa mwaka, unapo kusanya mazao yako kutoka shambani.
17 All your males must appear before the Lord Yahweh three times every year.
Wanaume wote wako lazima wajitokeze kwa Bwana Yahweh mara tatu kila mwaka.
18 You must not offer the blood from sacrifices made to me with bread containing yeast. The fat from the sacrifices at my festivals must not remain all night until the morning.
Haupaswi kutoa damu iliyo tolewa dhabihu kwangu na mkate uliyotiwa hamira. Mafuta kutoka kwa dhabihu za sherehe zangu hayapaswi kubaki usiku wote mpaka asubui.
19 You must bring the choicest firstfruits from your land into my house, the house of Yahweh your God. You must not boil a young goat in its mother's milk.
Lazima ulete matunda ya kwanza bora kutoka shambani mwako ndani ya nyumba yangu, nyumba ya Yahweh Mungu wako. Haupaswi kumchemsha mbuzi mtoto akiwa bado ananyonya.
20 I am going to send an angel before you to guard you on the way, and to bring you to the place that I have prepared.
Ninaenda kumleta malaika mbele yako kukuongoza njiani, na kukuleta sehemu niliyo iandaa.
21 Be attentive to him and obey him. Do not provoke him, for he will not pardon your transgressions. My name is on him.
Kuwa makini naye na kumtii.
22 If you indeed obey his voice and do everything that I tell you, then I will be an enemy to your enemies and an adversary to your adversaries.
Husimkasirishe, kwa kuwa hatasamehe makosa yako. Jina langu liko kwake. Kama hakika ukimtii sauti yake na kufanya kila ninacho kwambia, kisha nitakuwa adui kwa adui zako na mpinzani kwa wapinzani wako.
23 My angel will go before you and bring you to the Amorites, Hittites, Perizzites, Canaanites, Hivites, and the Jebusites. I will destroy them.
Malaika mwangu ataenda mbele zako na kukuleta kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanani, Wahivi, na Wayebusi. Nitawaharibu.
24 You must not bow down to their gods, worship them, or do as they do. Instead, you must completely overthrow them and smash their stone pillars in pieces.
Haupaswi kuinamia miungu yao, kuabudu, au kufanya wanavyo fanya. Badala yake, lazima uwapindue kabisa na kuvunja nguzo zao za mawe vipande vipande.
25 You must worship Yahweh your God, and he will bless your bread and water. I will remove sickness from among you.
Lazima umuabudu Yahweh Mungu wako, na atabariki mkate wako na maji. Nitaondoa magonjwa miongoni mwenu.
26 No woman will be barren or will miscarry her young in your land. I will give you long lives.
Hakuna mwanamke atakaye kuwa tasa au mimba kuharibika katika nchi yako. Nitawapa maisha marefu.
27 I will send fear of myself on those into whose land you advance. I will kill all the people whom you meet. I will make all your enemies turn their backs to you in fright.
Nitatuma hofu yangu kwao ambao mnaenda. Nitaua wote mnao kutana nao. Nitafanya maadui zenu wawaogope kwa kugeuza migongo yao kwenu.
28 I will send hornets before you that will drive out the Hivites, Canaanites, and the Hittites from before you.
Nitatuma mavu kwenu watakao fukuza Wahivi, Wakanani, na Wahiti mbele zenu.
29 I will not drive them out from before you in one year, or the land would become abandoned, and the wild animals would become too many for you.
Sitawaondoa kwenu kwa mwaka mmoja, au nchi itakuwa imetelekezwa, na wanyama wa porini watakuwa wengi kwenu.
30 Instead, I will drive them out little by little from before you until you become fruitful and inherit the land.
Badala yake, nitawafukuza kidogo kidogo kutoka kwenu mpaka utakapo kuwa umestawi na kurithi nchi.
31 I will fix your borders from the Sea of Reeds to the Sea of the Philistines, and from the wilderness to the Euphrates River. I will give you victory over the land's inhabitants. You will drive them out before yourselves.
Nitatengeneza mipaka yako kutoka Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kutoka nyikani hadi Mto Frati. Nitakupa ushindi juu ya wakazi wote wa nchi. Utawaondoa kutoka kwako mwenyewe.
32 You must not make a covenant with them or with their gods.
Haupaswi kufanya agano na wao au na miungu yao.
33 They must not live in your land, or they would make you sin against me. If you worship their gods, this will surely become a trap for you.'”
Hawapaswi kuishi nchini mwako, au watakufanya ufanya dhambi dhidi yangu. Ukiabudu miungu yao, hakika watakuwa mtego kwako.'”

< Exodus 23 >