< Exodus 20 >

1 God spoke all these words:
Ndipo Mungu akasema maneno haya yote:
2 “I am Yahweh your God, who brought you out of the land of Egypt, out of the house of slavery.
“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.
3 You must have no other gods before me.
Usiwe na miungu mingine ila mimi.
4 You must not make for yourself a carved figure nor the likeness of anything that is in heaven above, or that is in the earth beneath, or that is in the water below.
Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni, au duniani chini, au ndani ya maji.
5 You must not bow down to them or worship them, for I, Yahweh your God, am a jealous God. I punish the ancestors' wickedness by bringing punishment on the descendants, to the third and the fourth generation of those who hate me.
Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 But I show covenant faithfulness to thousands of those who love me and keep my commandments.
lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
7 You must not take the name of Yahweh your God, in vain, for I will not hold guiltless anyone who takes my name in vain.
Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
8 Remember the Sabbath day, to set it apart to me.
Ikumbuke siku ya Sabato, uitakase.
9 You must labor and do all your work for six days.
Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote,
10 But the seventh day is a Sabbath for Yahweh your God. On it you must not do any work, you, or your son, or your daughter, or your male servant, or your female servant, or your cattle, or the foreigner who is within your gates.
lakini siku ya saba ni Sabato kwa Bwana Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wako wa kiume au wa kike, wala wanyama wako, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
11 For in six days Yahweh made the heavens and earth, the sea, and everything that is in them, and rested on the seventh day. Therefore Yahweh blessed the Sabbath day and set it apart.
Kwa kuwa kwa siku sita, Bwana aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo Bwana akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.
12 Honor your father and your mother, so that you may live a long time in the land that Yahweh your God is giving you.
Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.
13 You must not murder anyone.
Usiue.
14 You must not commit adultery.
Usizini.
15 You must not steal from anyone.
Usiibe.
16 You must not give false testimony against your neighbor.
Usimshuhudie jirani yako uongo.
17 You must not covet your neighbor's house; you must not covet your neighbor's wife, his male servant, his female servant, his ox, his donkey, or anything that belongs to your neighbor.”
Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wa kiume au wa kike, wala ngʼombe wake au punda wake, wala chochote kile alicho nacho jirani yako.”
18 All the people saw the thundering and the lightning, and heard the voice of the trumpet, and saw the mountain smoking. When the people saw it, they trembled and stood far off.
Watu walipoona ngurumo na radi, na kusikia mlio wa tarumbeta, na kuuona mlima katika moshi, walitetemeka kwa woga. Wakasimama mbali
19 They said to Moses, “Speak to us, and we will listen; but do not let God speak to us, or we will die.”
na wakamwambia Mose, “Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini usimwache Mungu aseme nasi, la sivyo tutakufa.”
20 Moses said to the people, “Do not be afraid, for God has come to test you so that the honor of him may be in you, and so that you do not sin.”
Mose akawaambia watu, “Msiogope! Mungu amekuja kuwajaribu, ili kwamba hofu ya Mungu iwakalie, msitende dhambi.”
21 So the people stood far off, and Moses approached the thick darkness where God was.
Watu wakabaki mbali, wakati Mose alipolisogelea lile giza nene mahali pale Mungu alipokuwa.
22 Yahweh said to Moses, “This is what you must tell the Israelites: 'You yourselves have seen that I have talked with you from heaven.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli hivi: ‘Mmejionea wenyewe kwamba nimesema nanyi kutoka mbinguni:
23 You will not make for yourselves other gods alongside me, gods of silver or gods of gold.
Msijifanyizie miungu yoyote na kuilinganisha nami, msijitengenezee miungu ya fedha wala miungu ya dhahabu.
24 You must make an earthen altar for me, and you must sacrifice on it your burnt offerings, fellowship offerings, sheep, and oxen. In every place where I cause my name to be honored, I will come to you and bless you.
“‘Utanitengenezea madhabahu ya udongo, na juu yake utoe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani, kondoo zako, mbuzi na ngʼombe zako. Popote nitakapofanya Jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki.
25 If you make me an altar of stone, you must not build it of cut stones, for if you use your tools on it, you will have defiled it.
Ikiwa unanitengenezea madhabahu ya mawe, usiijenge kwa mawe ya kuchonga, maana mkitumia chombo cha kuchongea mtaitia unajisi.
26 You must not go up to my altar on steps, so that your nakedness is not exposed.'”
Msitumie ngazi kupandia kwenye madhabahu yangu, uchi wako usije ukadhihirika kwa chini.’

< Exodus 20 >