< Exodus 12 >

1 Yahweh spoke to Moses and Aaron in the land of Egypt. He said,
Yahweh akasema na Musa na Aruni katika nchi ya Misri. Alisema,
2 “For you, this month will be the start of months, the first month of the year to you.
“Kwako wewe, mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi, mwezi wa kwanza wa mwaka kwako.
3 Tell the assembly of Israel, 'On the tenth day of this month they must each take a lamb or young goat for themselves, each family doing this, a lamb for each household.
Liambie kusanyiko la Israeli, 'Siku ya kumi mwezi huu kila mtu lazima achukuwe mwana kondoo au mbuzi mdogo wa kwake, kila familia ifanye hivi, mwana kondoo kwa kila nyumba.
4 If the household is too small for a lamb, the man and his next door neighbor are to take lamb or young goat meat that will be enough for the number of the people. It should be enough for everyone to eat, so they must take enough meat to feed them all.
Kama hiyo nyumba ni ndogo sana kwa mwana kondoo, mwanaume na jirani yake wachukuwe mwana kondoo au nyama ya mbuzi mdogo ambayo itatosha watu. Lazima iwe yatosha kwa kila mtu kula, kwaiyo lazima wachukuwe nyama ya kutosha kulisha wote.
5 Your lamb or young goat must be without blemish, a one-year-old male. You may take one of the sheep or goats.
Mwana kondoo wako au mbuzi wako mdogo lazima asiwe na upungufu, dume mwenye mwaka mmoja. Unaweza kuchukuwa mmoja wa kondoo au mbuzi.
6 You must keep it until the fourteenth day of that month. Then the whole assembly of Israel must kill these animals at twilight.
Lazima umtunze mpaka siku ya kumi na nne ya huo mwezi. Kisha kusanyiko lote la Israeli lazima liwaue hawa wanyama jioni.
7 You must take some of the blood and put it on the two side doorposts and on the tops of the doorframes of the houses in which you will eat the meat.
Lazima uchukuwe baadhi ya damu na uweke kwenye sehemu mbili za mihimili ya milango na juu ya fremu za milango ambapo utalia hizo nyama.
8 You must eat the meat that night, after first roasting it over a fire. Eat it with bread made without yeast, along with bitter herbs.
Lazima ule hizo nyama usiku, baada ya kuchoma kwenye moto. Kula na mkate ulio andaliwa kwa hamira, pamoja na mimea michungu.
9 Do not eat it raw or boiled in water. Instead, roast it over fire with its head, legs and inner parts.
Usiile mbichi au imechemshwa kwenye maji. Badala yake, choma kwenye moto na kichwa chake, miguu na sehemu za ndani.
10 You must not let any of it be left over until morning. You must burn whatever is left over in the morning.
Usiache ata kidogo kubaki mpaka asubui. Lazima uchome chochote kilicho baki asubui.
11 This is how you must eat it: with your belt fastened, your shoes on your feet, and your staff in your hand. You must eat it hurriedly. It is Yahweh's Passover.
Hivi ndivyo wa paswa kula: ukiwa umefunga mkanda wako, umevaa viatu vyako, na gongo lako mkononi mwako. Lazima ule kwa haraka. Ni Pasaka ya Yahweh.
12 Yahweh says this: I will go through the land of Egypt in that night and attack all the firstborn of man and animal in the land of Egypt. I will bring punishment on all the gods of Egypt. I am Yahweh.
Yahweh anasema hili: Nitaenda katika nchi ya Misri usiku na kushambulia wazaliwa wote wa kwanza wa wanadamu na wanyama katika nchi ya Misri. Nitaleta pigo kwa miungu yote ya Misri. Mimi ni Yahweh.
13 The blood will be a sign on your houses for my coming to you. When I see the blood, I will pass over you when I attack the land of Egypt. This plague will not come on you and destroy you.
Damu itakuwa ishara kwenye nyumba zenu ya kuja kwangu. Nitakapo ona damu, nitapita nitakapo shambulia nchi ya Misri. Ili pigo halitawajia na kuwaharibu.
14 This day will become a memorial day for you, which you must observe as a festival for Yahweh. It will always be a law for you, throughout your people's generations, that you must observe this day.
Hii siku itakuwa kumbukumbu kwenu, ambayo lazima muadhimishe kama sherehe ya Yahweh. Itakuwa sheria kwenu pia, kwenye vizazi vyote vya watu wenu, ambayo mwapaswa kuadhimisha leo.
15 You will eat bread without yeast during seven days. On the first day you will remove the yeast from your houses. Whoever eats leavened bread from the first day until the seventh day, that person must be cut off from Israel.
Utakula mkate bila hamira wakati wa siku saba. Siku ya kwanza utaondoa hamira kwenye nyumba zenu. Yeyote atakaye kula mkate uliyotiwa chachu kwanzia siku ya kwanza mpaka siku ya saba, huyo mtu lazima akatwe kutoka Israeli.
16 On the first day there will be an assembly that is set apart to me, and on the seventh day there will be another such gathering. No work will be done on these days, except the cooking for everyone to eat. That must be the only work that may be done by you.
Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko lililo tengwa kwa ajili yangu, na siku ya saba kutakuwa na kusanyiko kama hilo. Hakuna kazi itakayo fanywa hizi siku, zaidi ya kupika kila mmoja ale. Hiyo ndio kazi pekee itakayo fanywa na wewe.
17 You must observe this Festival of Unleavened Bread because it is on this day that I will have brought your people, armed group by armed group, out of the land of Egypt. So you must observe this day throughout your people's generations. This will always be a law for you.
Lazima uadhimishe hii Sherehe ya Mkate Usiotiwa Chachu kwasababu ni siku hii ambayo nitawaleta watu wako, makundi yaliyo na silaha, kwa makundi yaliyo na silaha, kutoka nchi ya Misri. Lazima uadhimishe hii siku kwa vizazi vyote vya watu wako. Hii itakuwa sheria kwako.
18 You must eat unleavened bread from twilight of the fourteenth day in the first month of the year, until twilight of the twenty-first day of the month.
Lazima ule mkate usiotiwa chachu kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza wa mwaka, mpaka jioni ya siku ya ishirini na moja ya mwezi.
19 During these seven days, no yeast must be found in your houses. Whoever eats bread made with yeast must be cut off from the community of Israel, whether that person is a foreigner or someone born in your land.
Wakati wa hizi siku, nyumbani mwenu kusipatikane na hamira. Yeyote atakaye kula mkate ulio andaliwa na hamira lazima akatwe kutoka jamii ya Israeli, huyo mtu awe ni mgeni au mtu aliye zaliwa nchini mwenu.
20 You must eat nothing made with yeast. Wherever you live, you must eat bread made without yeast.'”
Hautakula chochote kilicho andaliwa na hamira. Popote utapo ishi, lazima ule mkate usio na hamira.”'
21 Then Moses summoned all the elders of Israel and said to them, “Go and select lambs or kids that will be enough to feed your families and kill the Passover lamb.
Kisha Musa akawaita viongozi wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni na mchague mwana kondoo au mbuzi watakao tosha kulisha familia zenu na muue mwana kondoo wa pasaka.
22 Then take a bunch of hyssop and dip it in the blood that will be in a basin. Apply the blood in the basin to the top of the doorframe and the two doorposts. None of you is to go out of the door of his house until the morning.
Kisha chukua jani la hisopu na uchovye kwenye damu itakayo kuwa kwenye beseni. Paka damu iliyo kwenye beseni juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango. Hakuna ata mmoja atakaye toka nje ya mlango wake mpaka asubui.
23 For Yahweh will pass through to attack the Egyptians. When he sees the blood on the top of the doorframe and on the two doorposts, he will pass over your door and not permit the destroyer to come into your houses to attack you.
Kwa kuwa Yahweh atapita kushambulia Wamisri. Atakapo ona damu juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango, atapita mlango wako na ata ruhusu mharibifu kuja nyumbani kwenu kuwashambulia.
24 You must observe this event. This will always be a law for you and your descendants.
Lazima uadhimishe hili tukio. Hili litakuwa daima sheria kwako na kwa uzao wenu.
25 When you enter the land that Yahweh will give you, just as he has promised to do, you must observe this act of worship.
Utakapo ingia nchi Yahweh atakayo kupa, kama alivyo ahidi kufanya, lazima uadhimishe hili tendo la ibada.
26 When your children ask you, 'What does this act of worship mean?'
Watoto wako watakapo kuuliza, 'Hili tendo la ibada lina maana gani?'
27 then you must say, 'It is the sacrifice of Yahweh's Passover, because Yahweh passed over the Israelites' houses in Egypt when he attacked the Egyptians. He set our households free.'” Then the people bowed down and worshiped Yahweh.
kisha lazima useme, 'Ni sadaka ya Pasaka ya Yahweh, kwasababu Yahweh kapita nyumba za Waisraeli Misri alipo washambulia Wamisri. Aliweka nyumba zetu huru.”' Kisha watu wakamsujudia Yahweh.
28 The Israelites went and did exactly as Yahweh had commanded Moses and Aaron.
Waisraeli wakaenda na kufanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
29 It happened at midnight that Yahweh attacked all the firstborn in the land of Egypt, from the firstborn of Pharaoh, who sat on his throne, to the firstborn of the person in prison and all the firstborn of cattle.
Ikawa usiku wa manane kuwa Yahweh akawashambulia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, aliye keti kiti chake cha enzi, mzaliwa wa kwanza wa mtu aliye gerezani na wazaliwa wote wa kwanza wa mifugo.
30 Pharaoh got up in the night—he, all his servants, and all the Egyptians. There was loud lamenting in Egypt, for there was not a house where there was not someone dead.
Farao akaamka usiku - yeye, watumishi wake, na Wamisri. Palikuwa na kelele za maombolezo Misri, kwa kuwa hakukuwa na nyumba ambayo hamna mtu hakufa.
31 Pharaoh summoned Moses and Aaron in the night and said, “Get up, get out from among my people, you and the Israelites. Go, worship Yahweh, as you have said you wanted to do.
Farao akamuita Musa na Aruni usiku na kusema, “Inuka, tokeni miongoni mwa watu wangu, nyie pamoja na Waisraeli. Nenda, mmuabudu Yahweh, kama mlivyo sema mnataka kufanya.
32 Take your flocks and your herds, as you have said, and go, and also bless me.”
Chukuweni ng'ombe zenu na kondoo zenu, kama mlivyo sema, na muende, na pia mnibariki.”
33 The Egyptians were in a great hurry to send them out of the land, for they said, “We will all die.”
Wamisri walikuwa na haraka ya kuwa ondoa nchini, kwa kuwa walisema, “Sisi ni watu tuliokufa.”
34 So the people took their dough without adding any yeast. Their kneading bowls were already tied up in their clothes and on their shoulders.
Watu wakachukuwa ngano yao pasipo kuongeza hamira yeyote. Bakuli zao zakukandia ngano zilifungiwa kwenye nguo zao na kwenye mabega yao.
35 Now the people of Israel did as Moses told them. They asked the Egyptians for articles of silver, articles of gold, and clothing.
Watu Waisraeli walifanya kama Musa alivyo waambia. Waliwaomba Wamisri vitu vya fedha, vitu vya dhahabu, na nguo.
36 Yahweh made the Egyptians eager to please the Israelites. So the Egyptians gave them whatever they asked for. In this way, the Israelites plundered the Egyptians.
Yahweh aliwafanya Wamisri na shauku ya kuwapendeza Waisraeli. Hivyo Wamisri waliwapa chochote walicho waomba. Katika hili, Waisraeli waliwachukulia vingi Wamisri.
37 The Israelites journeyed from Rameses to Succoth. They numbered about 600,000 men on foot, in addition to the women and children.
Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesi kwenda Sakothi. Walikuwa na idadi ya wanaume 600, 000 kwa miguu, kuongezea kwa wanawake na watoto.
38 A mixed multitude also went with them, together with flocks and herds, a very large number of livestock.
Mchanganyiko wa kundi la wasio Waisraeli pia walienda nao, pamoja na ng'ombe na kondoo, idadi kumbwa ya mifugo.
39 They baked bread without yeast in the dough that they brought from Egypt. It was without yeast because they had been driven out of Egypt and could not delay to prepare food.
Walioka mikate na unga wa ngano wenye hamira walio utoa Misri. Ulikuwa hauna hamira kwasababu waliondolewa Misri na hawakuweza chelewa kuandaa chakula.
40 The Israelites had lived in Egypt for 430 years.
Waisraeli waliishi Misri kwa miaka 430.
41 At the end of 430 years, on that very day, all of Yahweh's armed groups went out from the land of Egypt.
Baada ya miaka 430, siku hiyo hiyo, majeshi yote ya Yahweh yalio jiami waliondoka kutoka nchi ya Misri.
42 This was a night to stay awake, for Yahweh to bring them out from the land of Egypt. This was Yahweh's night to be observed by all the Israelites throughout their people's generations.
Huu ulikuwa usiku wakuwa macho, ili Yahweh awatoe kutoka nchi ya Misri. Huu ulikuwa usiku wa Yahweh wa kuadhimishwa na Waisraeli wote na watu wa vizazi vyao vyote.
43 Yahweh said to Moses and Aaron, “Here is the rule for the Passover: No foreigner may share in eating it.
Yahweh akamwambia Musa na Aruni, “Hii ni sheria ya Pasaka: hakuna mgeni anaye ruhusiwa kuila.
44 However, every Israelite's slave, bought with money, may eat it after you have circumcised him.
Walakini, kila mtumwa wa Misraeli, aliye nunuliwa kwa pesa, anaeza kula baada ya kutahiriwa.
45 Foreigners and hired servants must not eat any of the food.
Wageni na watumishi waajiriwa hawapaswi kula chakula chochote.
46 The food must be eaten in one house. You must not carry any of the meat out of the house, and you must not break any bone of it.
Chakula chapaswa kuliwa ndani ya nyumba moja. Hauruhusiwi kubeba nyama yeyote nje ya nyumba, na hauruhusiwi kuvunja mfumba wowote.
47 All the community of Israel must observe the festival.
Jamii zote za Israeli za paswa kuadhimisha sherehe.
48 If a foreigner lives with you and wants to observe the Passover to Yahweh, all his male relatives must be circumcised. Then he may come and observe it. He will become like the people who were born in the land. However, no uncircumcised person may eat any of the food.
Kama mgeni anaishi na wewe na anataka kuadhimisha Pasaka kwa Yahweh, ndugu zake wote wa kiume wapaswa kutahiriwa. Kisha anaeza kuja na kuadhimisha. Atakuwa kama watu walio zaliwa kwenye nchi. Walakini, hakuna mtu asiye tahiriwa anaruhusiwa kula chakula chochote.
49 This same law will apply to both the native born and to the foreigner who lives among you.”
Sheria hii hii itahusika kwa mzaliwa wa asili na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50 So all the Israelites did exactly as Yahweh had commanded Moses and Aaron.
Waisraeli wote walifanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
51 It came about that very day that Yahweh brought Israel out of the land of Egypt by their armed groups.
Ikaja kuwa siku hiyo Yahweh akawaleta Israeli kutoka nchi ya Misri kwa makundi yalio jiami.

< Exodus 12 >