< Esther 6 >

1 That night the king could not sleep. He commanded servants to bring the records of the events of his reign, and they were being read aloud to the king.
Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
2 It was found recorded there that Mordecai had told about Bigthana and Teresh, two of the king's officials who guarded the entrance, who had tried to harm King Ahasuerus.
Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
3 The king asked, “What was done to give honor or recognition to Mordecai for doing this?” Then the king's young men who served him said, “Nothing was done for him.”
Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
4 The king said, “Who is in the courtyard?” Now Haman had entered the outer courtyard of the king's house to speak to him about hanging Mordecai on the gallows he set up for him.
Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
5 The king's servants said to him, “Haman is standing in the courtyard.” The king said, “Let him come in.”
Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
6 When Haman entered, the king said to him, “What should be done for the man whom the king takes pleasure in honoring?” Now Haman said in his heart, “Whom would the king take pleasure in honoring more than me?”
Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
7 Haman said to the king, “For the man whom the king takes pleasure in honoring,
Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
8 let royal robes be brought, robes that the king has worn, and a horse that the king has ridden and on whose head is the royal crest.
aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
9 Then let the robes and the horse be given to one of the king's most noble officials. Let them dress the man whom the king takes pleasure in honoring, and let them lead him on the horse through the city streets. Let them proclaim before him, 'This is what is done to the one whom the king takes pleasure in honoring!'”
Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
10 Then the king said to Haman, “Hurry, take the robes and the horse, as you have said, and do this for Mordecai the Jew who sits at the king's gate. Do not fail in a single matter of what you have said.”
Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
11 Then Haman took the robe and the horse. He dressed Mordecai and led him on the horse through the city streets. He proclaimed before him, “This is what is done for a man whom the king takes pleasure in honoring!”
Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
12 Mordecai returned to the king's gate. But Haman hurried to his house, mourning, with his head covered.
Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
13 Haman told Zeresh his wife and all his friends everything that happened to him. Then his men who were known for their wisdom, and Zeresh his wife, said to him, “If Mordecai, before whom you have begun to fall, is Jewish, you will not overcome him, but you will certainly fall before him.”
naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
14 While they were talking with him, the king's officials arrived. They hurried to bring Haman to the feast that Esther had prepared.
Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.

< Esther 6 >