< Ephesians 5 >

1 Therefore be imitators of God, as dearly loved children.
Kwa hiyo muwe watu wa kumfuata Mungu, kama watoto wake wapendwao.
2 And walk in love, as also Christ loved us and gave himself up for us, a fragrant offering and sacrifice to God.
Mtembee katika pendo, vilevile kama Kristo alivyotupenda sisi, alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu. Yeye alikuwa sadaka na dhabihu, kuwa harufu nzuri ya kumfurahisha Mungu.
3 But there must not be even a suggestion among you of sexual immorality or any kind of impurity or of greed, for these are improper for God's holy people.
Zinaa au uchafu wowote na tamaa mbaya lazima visitajwe kati yenu, kama inavyotakiwa kwa waaminio,
4 Let there be no filthiness, no foolish talk, and no crude jokes—all of which are improper. Instead there should be thanksgiving.
wala machukizo yasitajwe, mazungumzo ya kipumbavu, au mizaha ya udhalilishaji, ambayo siyo sawa, badala yake iwepo shukrani.
5 For you can be sure of this, that no sexually immoral, impure, or greedy person—that is, an idolater—has any inheritance in the kingdom of Christ and God.
Mnaweza kuwa na uhakika ya kwamba kuna zinaa, uchafu, wala atamaniye, huyo nimwabudu sanamu, hana urithi wowote katika ufalme wa Kristo na Mungu.
6 Let no one deceive you with empty words, for because of these things the anger of God is coming upon the sons of disobedience.
Mtu yote asikudanganye kwa maneno matupu, kwa sababu ya mambo haya hasira ya Mungu inakuja juu ya wana wasiotii.
7 Therefore, do not join in with them.
Hivyo usishiriki pamoja nao.
8 For you were once darkness, but now you are light in the Lord. Walk as children of light
Kwa kuwa ninyi mwanzo mlikuwa giza, lakini sasa mmekuwa nuru katika Bwana. Hivyo tembeeni kama watoto wa nuru.
9 (for the fruit of the light consists in all goodness, righteousness, and truth),
Kwa kuwa matunda ya nuru yanajumuisha uzuri wote, haki na ukweli.
10 and find out what is pleasing to the Lord.
Tafuta kile kinacho furahisha kwa Bwana.
11 Do not associate with the unfruitful works of darkness, but rather expose them.
Usiwepo ushiriki katika kazi za giza zisizo na matunda, badala yake ziweke wazi.
12 For it is shameful even to mention the things they do in secret.
Kwa sababu mambo yanayofanywa na wao sirini ni aibu sana hata kuyaelezea.
13 But when anything is illuminated by the light, it becomes visible.
Mambo yote, yanapofichuliwa na nuru, huwa wazi,
14 For anything that becomes visible is light. Therefore it says, “Awake, you sleeper, and arise from the dead, and Christ will shine on you.”
kwa kuwa Kila kitu kilichofichuliwa kinakuwa nuruni. Hivyo husema hivi, “Amka, wewe uliyelala, na inuka kutoka wafu na Kristo atang'aa juu yako.”
15 Look carefully how you live—not as unwise but as wise.
Hivyo iweni makini jinsi mtembeavyo, siyo kama watu wasio werevu bali kama werevu.
16 Redeem the time because the days are evil.
Ukomboeni muda kwa kuwa siku ni za uovu.
17 Therefore, do not be foolish, but understand what the will of the Lord is.
Msiwe wajinga, badala yake, fahamuni nini mapenzi ya Bwana.
18 And do not get drunk with wine, for that leads to reckless behavior. Instead, be filled with the Holy Spirit,
Msilewe kwa mvinyo, huongoza kwenye uharibifu, badala yake mjazwe na Roho Mtakatifu.
19 speaking to each other in psalms and hymns and spiritual songs, singing and making melody to the Lord with all your heart,
Zungumzeni na kila mmoja wenu kwa zaburi, na sifa, na nyimbo za rohoni. Imbeni na sifuni kwa moyo kwa Bwana.
20 always giving thanks for everything, in the name of our Lord Jesus Christ to God the Father,
Daima toa shukrani kwa mambo yote katika jina la Kristo Yesu Bwana wetu kwa Mungu Baba.
21 submitting yourselves to one another in reverence for Christ.
Jitoeni wenyewe kila mmoja kwa mwingine kwa heshima ya Kristo.
22 Wives, submit to your husbands, as to the Lord.
Wake, jitoeni kwa waume zenu, kama kwa Bwana.
23 For the husband is the head of the wife as Christ also is the head of the church, and Christ himself is its savior.
Kwa sababu mume ni kichwa cha mke, kama Kristo alivyo kichwa cha kanisa. Ni mwokozi wa mwili.
24 But as the church submits to Christ, so also wives must submit to their husbands in everything.
Lakini kama kanisa lilivyo chini ya Kristo, vilevile wake lazima wafanye hivyo kwa waume zao katika kila jambo.
25 Husbands, love your wives, as Christ loved the church and gave himself up for her.
Waume, wapendeni wake zenu kama vile Kristo alivyolipenda kanisa na akajitoa mwenyewe kwa ajili yake.
26 Christ gave himself for the church so that he might make her holy, having cleansed her by the washing of water with the word,
Alifanya hivyo ili liwe takatifu. Alilitakasa kwa kuliosha na maji katika neno.
27 so that he might present her to himself as glorious, without stain or wrinkle or any such thing, but holy and without fault.
Alifanya hivi ili kwamba aweze kujiwasilishia mwenyewe kanisa tukufu, pasipo na doa wala waa au kitu kifananacho na haya, badala yake ni takatifu lisilo na kosa.
28 In the same way husbands ought to love their own wives as their own bodies. He who loves his own wife loves himself.
Kwa njia ile ile, waume wanatakiwa kuwapenda wake zao kama miili yao. Yule ampendae mke wake anajipenda mwenyewe.
29 For no one ever hated his own body, but nourishes and treats it with care, just as Christ nourishes and treats the church with care,
Hakuna hata mmoja anayechukia mwili wake. Badala yake, huurutubisha na kuupenda, kama Kristo pia alivyolipenda kanisa.
30 because we are members of his body.
Kwa kuwa sisi ni washiriki wa mwili wake.
31 “For this reason a man will leave his father and mother and will be joined to his wife, and the two will become one flesh.”
“Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na ataungana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja”.
32 This hidden truth is great—but I am speaking about Christ and the church.
huu ulikuwa umefichika. Lakini ninasema kuhusu Kristo na kanisa.
33 Nevertheless, each of you also must love his own wife as himself, and the wife must respect her husband.
Walakini, kila mmoja wenu lazima ampende mke wake kama mwenyewe, na mke lazima amheshimu mumewe.

< Ephesians 5 >