< Deuteronomy 33 >

1 This is the blessing with which Moses the man of God blessed the people of Israel before his death.
Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
2 He said: Yahweh came from Sinai and rose from Seir upon them. He shined out from Mount Paran, and he came with ten thousands of holy ones. In his right hand were flashes of lightning.
Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
3 Indeed, he loves the peoples; all his holy ones are in your hand, and they bowed down at your feet; they received your words.
Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
4 Moses commanded us a law, an inheritance for the assembly of Jacob.
Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
5 Then there was a king in Jeshurun, when the heads of the people had gathered, all the tribes of Israel together.
Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
6 Let Reuben live and not die, but may his men be few.
Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
7 This is the blessing for Judah. Moses said: Listen, Yahweh, to the voice of Judah, and bring him to his people again. Fight for him; be a help against his enemies.
Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
8 About Levi, Moses said: Your Thummim and your Urim belong your loyal one, the one whom you tested at Massah, with whom you struggled at the waters of Meribah.
Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
9 The man who said about his father and mother, “I have not seen them.” Neither did he acknowledge his brothers, nor did he take account of his own children. For he guarded your word and kept your covenant.
Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
10 He teaches Jacob your decrees and Israel your law. He will put incense before you and whole burnt offerings on your altar.
Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
11 Bless, Yahweh, his possessions, and accept the work of his hands. Shatter the loins of those who rise up against him, and those of the people who hate him, so that they do not rise up again.
Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
12 About Benjamin, Moses said: The one loved by Yahweh lives in security beside him; Yahweh shields him all the day long, and he lives between Yahweh's arms.
Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
13 About Joseph, Moses said: May his land be blessed by Yahweh with the precious things of heaven, with the dew, and with the deep that lies beneath.
Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
14 May his land be blessed with the precious things of the harvest of the sun, with the precious things of the produce of the months,
Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
15 with the finest things of the ancient mountains, and with the precious things of the everlasting hills.
kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
16 May his land be blessed with the precious things of the earth and its abundance, and with the good will of him who was in the bush. Let the blessing come on the head of Joseph, and on the top of the head of him who was prince over his brothers.
Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
17 The firstborn of an ox, majestic is he, and his horns are the horns of a wild ox. With them he will push the peoples, all of them, to the ends of the earth. These are the ten thousands of Ephraim; these are the thousands of Manasseh.
Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
18 About Zebulun, Moses said: Rejoice, Zebulun, in your going out, and you, Issachar, in your tents.
Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
19 They will call the peoples to the mountains. There will they offer sacrifices of righteousness. For they will suck the abundance of the seas, and from the sand on the seashore.
Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
20 About Gad, Moses said: Blessed be he who enlarges Gad. He will live there like a lioness, and he will tear off an arm or a head.
Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
21 He provided the best part for himself, for there was the leader's portion of land reserved. He came with the heads of the people. He carried out the justice of Yahweh and his decrees with Israel.
Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
22 About Dan, Moses said: Dan is a lion cub that leaps out from Bashan.
Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
23 About Naphtali, Moses said: Naphtali, satisfied with favor, and full of the blessing of Yahweh, take possession of the land to the west and south.
Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
24 About Asher, Moses said: Blessed be Asher more than the other sons; let him be acceptable to his brothers, and let him dip his foot in olive oil.
Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
25 May your city bars be iron and bronze; as long as will be your days, so long will your security be.
Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
26 There is no one like God, Jeshurun—the upright one, who rides through the heavens to your help, and in his majesty on the clouds.
Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
27 The eternal God is a refuge, and underneath are the everlasting arms. He thrust out the enemy from before you, and he said, “Destroy!”
Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
28 Israel dwelt in safety. Jacob's spring was secure in a land of grain and new wine; indeed, let his heavens drop dew on him.
Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
29 Your blessings are many, Israel! Who is like you, a people saved by Yahweh, the shield of your help, and the sword of your majesty? Your enemies will come trembling to you; you will trample down their high places.
Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.

< Deuteronomy 33 >